Nyerere hakung'atuka

Tuliamini saana katika propaganda hizi kupitia RTD. Eti umoja na kaunganisha watu. Hawa watu kuanzia chama cha TAA walikuwa wanaunganishwa na nani? Kukaa na kujilinganisha na wahutu na watutsi, si kujitendea haki. Nchi hii ina makabila zaidi ya 100. Sio makabila mawili. Babu zetu tayari walikuwa wameoa kwenye makabila tofauti kabla hata ya Nyerere kupata uhuru. Yeye aliwaunganisha nini? Kwnini mifano ni Rwanda, Burundi na Kenye, wale wasiochapana wameunganishwa na nani?
 
Ukiwa kiongozi wa nchi ni lazima ujadiliwe. Na ndio maana tunamzungumzia "baba wa Taifa". Kwenye mada nasema wazi. Nyerere hakutoa fursa kwa mawazo ya wengine. Aliamini katika ya kwake na alipoona hayatekelezeki akakimbia. Ukizungumzia katiba, yeye ndiye alikuwa muhusika mkuu wa muundaji wa hiyo katiba. Hakukuwa na demokrasia. Aliondoka kwa sababu his demise was inevitable. Alibisha saana mapinduzi ya sera za kiuchumi za mwanzoni mwa miaka 1980. Akang'ang'ania kutekeleza za kwake nchi ikawa haikopesheki na haiwezi kuzalisha na njaa ilikuwa kawaida. Nyerere akaondoka. Mbaya zaidi ukisoma Development Studies (DS) kwa mlimani, utakuwa na yenyewe imechachuliwa eti masharti ya World Bank na IMF.
 
Ndo maana nasema hivi, wanaomlaumu MWALIMU wajilaumu wao kwanza, alifanya yake kwa uwezo aliojaaliwa na Manani na amepumzika kwa amani na Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina.
Alifanya ya kwake kumbe alitakiwa kufanya ya Taifa. Waulize kina Mtei na Kambona na wengineo. Ukitoa maoni kuhusu sera zake, unageuka adui.
 
Alifanya ya kwake kumbe alitakiwa kufanya ya Taifa. Waulize kina Mtei na Kambona na wengineo. Ukitoa maoni kuhusu sera zake, unageuka adui.

Huo ni msemo na si kama unavyouchukulia wewe. Hakuna mkamilifu chini ya Jua na anayefanya mengi kwa ajili ya wengi basi hukumbukwa na wengi, bado Nyerere anaishi japo alishatangulia mbele ya haki. Mtei namjua na Kambona pia, niulize hata na Sarakikya kabisa, ila kumbuka ndani ya hii dunia hata ufanye mazuri mangapi huwezi kosa wapinzani, ni kwa hekma tu na busara na sometimes kaubabe kiduchu kinahitajika kuwa-nulify maadui zako, hasa wa ndani.
 
Mkakati wa kumfanya MTAKATIFU unaendelea.Na huwezi kuwa MTAKATIFU kama hujafanya kazi ya Kanisa.sasa hapa sijui iyakuwaje.
 
Mkakati wa kumfanya MTAKATIFU unaendelea.Na huwezi kuwa MTAKATIFU kama hujafanya kazi ya Kanisa.sasa hapa sijui iyakuwaje.
Kwahiyo ugumu wa kumjadili Nyerere unatokana na mkakati wa kumfanya Mtakatifu?
 
Kwahiyo ugumu wa kumjadili Nyerere unatokana na mkakati wa kumfanya Mtakatifu?
Naaam...hakuna haja ya kumjadili.Haitasaidia kitu chochote na ni kuntia doa ktk mkakati wa kumfanya Mtakatifu kwa kazi aliyoifanyia nchi.
 
Mkuu usipate tabu na mleta mada. Huyu mtu ana ID mbili na mdini sanaaa!
 
unao uhuru wa kusema utakacho, ninao uhuru wa kufikiri na kuandika nitakacho, na ni tabia yetu wabongo kutopenda kuthamini vya kwetu hivyo siwezi kukushangaa hata kidogo, leo hii Magufuli anasifiwa na waandishi wa habari wa kimataifa lakini hapa hapa nyumbani watu wanakwambia hajafanya kitu! hivyo siwezi kukushangaa unapojaribu kujenga hoja kuwa nyerere hakufanya kitu, ni maoni na ni upeo wako unaokupa jeuri ya kuandika chochote utakacho, kwangu mwalimu nyerere atabakia kuwa mmoja wa viongozi halisi wenye vision waliowahi kutokea barani Afrika. Mataifa mengine yamezama kwenye udini, ukabila na majungu ya ukanda, nyerere alipiga vita uhayawani huo tangu miaka ya 60 mwanzoni, wewe unajaribu kuniambia kuwa hajafanya lolote la maana, jaribu uwe na shukrani japo inaweza isitoke moyoni.
 
Udini, ukanda na ukabila ni matokeo ya uhohehahe na ukosefu wa elimu unaowafanya wachache wajinufaishe kwa mitafaruku ya wengi. Historia za kikabila za nchi tunazozitaja kama mfano ni za muda mrefu kabla ya uhuru. Tuangalie nchi tulizopata nazo uhuru ziko wapi. Au nchi alizoiga nyerere Mfumo wa ujamaa na kujitegemea ziliishia wapi. Ni nini kilifanya nchi yetu isiwe hata na kituo cha television wakati zanzibar na Kenya wakipiga hatua. Yapo aliyofanikiwa kama TAZARA kushirikiana na China ila mengi yanaendelea kubaki propaganda.
 
Nyerere amefanya mengi hilo la TAZARA ni mmoja tu, aliua uchifu tangu enzi za uhuru, na faida zake ni kujenga hali ya umoja. Mchagga anakwenda kusoma A level kule Mtwara, Mgogo anakwenda kusoma A level kule Bukoba. Unajua kinachowatesa Nigeria mpaka leo hii?, ni kushindwa kuondoa uchifu katika maisha yao, leo hii Hausa halali nyumba moja na mtu wa kabila la Igbo, Muigbo halali nyumba moja na myoruba. Nyerere aliweka msisitizo wa umoja, aliweka msisitizo wa kuwatumikia walio wengi. Hakutaka watanzania wajisahau na kujikweza. Anabakia na udhaifu wa kibinadamu lakini kwenye hekima na busara yupo kwenye viwango vya juu sana, ukubali au uamue kukataa hiyo ni juu yako wewe na nafsi yako.
 
"Mimi nang'atuka lakini naendelea kuamini kuwa bila CCM madhubuti, nchi yetu itayumba" J.K. Nyerere 1987.

"HAPA KAZI TU"
 
Mkuu nakushauri ukimbie tu., Ni vigumu sana kupata sapoti ya watu, kama hoja yako ni kumponda Nyerere.
 
Hayupo tena ktk mgongo wa ardhi.
Sadaqta! Kiwiliwili cha Nyerere ndio hakipo hai, lakini fikira ,udini, mawazo na JINAMIZI lake lipo palepale! linaendelea kututafuna tu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…