[HASHTAG]#UpdatesKimataifa[/HASHTAG]
Urusi tayari imesogea kwenye Mpaka wake na Korea kaskazini na kufunga silaha Nzito za kutungua Ndege Pamoja na kudaka Makombora Ya Marekani Dhidi ya Korea kaskazini.
Urusi imekiri kuwepo kwa uchokozi wa Marekani katika Rasi ya Korea.
URUSI ni nchi kubwa sana na imeanzia ulaya na kuishia ASIA.katika lugha nyingine naweza sema kuwa ni nchi moja ambayo ndani yake kuna mabara mawili,bala ya ULAYA na ASIA.
Mji wa URUSI ambao huigawa nchi iyo katika mabara hayo mawili ni YEKATERINBURG.
Miongoni mwa miji ya urusi iliyopo bara la ASIA ni VLADIVASTOK,TOMSK,SAHARINSKI YA KUSINI,,KHABAROVSK,YAKUTSK NK, ambayo kwa pamoja huitwa MASHARIKI YA MBALI YA URUSI( far eastern)
Sasa mji wa VLADIVASTOK ndo miongoni mwa miji ambayo ipo mipakani na umepakana na nchi nyingi tu.
Mji huu umepakana JAPAN ( kwa upande wa bahari),CHINA NA KOREA( kwa upande wa ardhi).
Hivyo basi kwa kuwa mji huu kwa upande wa ardhi umepakana na CHINA na KOREA KASKAZINI,ni wazi kuwa URUSI lazima aweke vifaa vyake vya kisasa katika mpaka huo ili kwamba ikitokea kuna vita kati ya nchi flani na KOREA KASKAZINI basi waweza kujihami na makombora ambayo yatalengwa kwenda upande wa URUSI kwani km 17 kutoka kwenye mpaka wa URUSI na KOREA KASKAZINI kuna makazi ya WARUSI wapatao 700 na kutoka kwenye mpaka mbaka mji wa VLADIVASTOK sio mbali sana.
Kumbuka ya kuwa VLADIVASTOK ni mji wa kijeshi wa urusi na kuna kambia kubwa sana ya
Majeshi ya URUSI, kwa vikosi vya Maji,pia mji huu ni muhimu sana kwa urusi kwani ndo anaotumia katika maswala ya kiulinzi dhidi ya JAPAN,CHINA NA KOREA.
VLADIVASTOK pia ni mji wa siri kwani ulikuwepo URUSI tangu zamani ila haukuwapo kwenye ramani ya nchi hiyo.kwa mara ya kwanza mji huu umeanza kuwekwa kwenye ramani mwaka 1991,so bado ni mji muhimu sana kwa URUSI.
Hivyo basi swala la MRUSI kuweka MITAMBO yake ya kukinga anga dhidi ya shambulio lolote( AIR DEFENCE MISSILE SYSTEM) halimaanishi kuwa yupo upande wa KOREA KASKAZINI bali ni kujilinda tu.
Nawasilisha.