NSSF na kauli mbiu ya miaka 55

NSSF na kauli mbiu ya miaka 55

namesake4

New Member
Joined
Jul 5, 2025
Posts
4
Reaction score
0
Mimi kama mdau na mnufaika wa mafao napata changamoto.

Niliacha kazi na nikaandika barua kwamba nakwenda kujiendeleza na masomo nikitegemea kutumia mafao yangu katika elimu kama kujilipia ada na kadhalika nafika nssf nauliza utaratibu naambiwa wewe huwezi kupata nssf hadi ufikishe miaka 55.

Kulingana na huu utaratibu nimelazimika kuacha kujiendeleza kielimu na kurudi mtaani angali pia sina kazi wala biashara.
Ndugu zangu kuna maswali kadhaa yananijia kichwani

1. Je ninauhakika gani kama nitafika miaka hiyo kwa hali ninayopitia wakati huu

2. Je, taasisi hii imewahi kufanya uchunguzi wowote juu ya changamoto wanazopitia wafanyakazi ambazo zinawafanya kuacha kazi?

3. Je, mafao hayo yanauhusiano gani na elimu na miaka 55?
Nadhani tusibaki kushikilia jambo hili la miaka 55 maana ni uonevu na unyanyasaji raia wanapitia changamoto nyingi mtaani na wanajua fika kwamba wana pesa sehemu.
 
Kufatilia mafao NSSF ni changamoto sana.taratibu zao hazieleweki.hata mimi nakabiliwa na changamoto hiyo hiyo kuwa nisubiri hadi nifikishe miaka 55yrs.wakati nasuburi nitimize hiyo miaka 55 nitakuwa naishi kwa tabu wakati pesa zangu zipo tu NsSf wanazungusha.
 
Kufatilia mafao NSSF ni changamoto sana.taratibu zao hazieleweki.hata mimi nakabiliwa na changamoto hiyo hiyo kuwa nisubiri hadi nifikishe miaka 55yrs.wakati nasuburi nitimize hiyo miaka 55 nitakuwa naishi kwa tabu wakati pesa zangu zipo tu NsSf wanazungusha.
Serikali inabidi iliangalie hili kwa jicho la tatu kwasababu majambazi na watu watakaofanya kazi za hovyo mtaani wanazidi ilihali mtu angepata nssf yake angeweza kuanzisha hata biashara yoyote na maisha yakasonga
 
Back
Top Bottom