NSSF inapofananishwa na jini Mnyonya damu!

NSSF inapofananishwa na jini Mnyonya damu!

Ta Muganyizi

R I P
Joined
Oct 19, 2010
Posts
5,355
Reaction score
2,737
Wapo Watanzania wengi kwenye sekta binafsi wanaofanya kazi kwa muda mfupi ambao hawakujaaliwa kupata ajiria za muda mrefu serikalini au mashirika ya umma.

Wanapomaliza mikataba yao au mazingira ya kazi kuwa magumu huamua kurudi nyumbani huku wakitegemea kibubu chao (NSSF) kuwa msaada wa kuwasaidia kusongesha maisha. Cha ajabu kibubu chako mwenyewe kinakugomea na kukuwekea masharti kibao kuhusu hela yako.

Sasa kwa hali halisi.....baadhi ya watu walioko kwenye mfuko huo wanajiuliza, mbona kiingiacho kutoka kinakuwa shida. Zinanyonywa na nini hela za wanachama? Kama kweli hela zipo kwa nini aliyeziweka asizipate?

Ni sawa na kuweka kibubu chini ya kitanda ukawa unatupia miambili miambili, ila siku unazihitaji unapewa masharti kibao eti mara mpaka uzeeke, mara nini sijui.

Kama hela iliyowekwa imo kweli fanyeni utaratibu muwape wenyewe. Sio muwanyonye damu hata kwa kidogo walichochangia. Picha inayokuja haraka ni kuwa hela imeliwa na kibubu!!!!! Haipo. Kama ipo wapeni wenyewe.
 
!
!
Zile Hela Huwa Mkiweka Kuna Mtu Huzichukua Na Kuzigawagawa Kwa Wananchi Barabarani Wakati Wa Ziara. Nyingine Huendeleza Kijijini Kwao Hukoooo Kuna Uwanja Wa Ndege.... Sina Uhakika Lakini Inaweza Kuwait Tofauti
 
Yaani nssf cjui INA mpango gani na sisi watanzania majira hakuna back tueni hizi miambili zetu tufanye tubiashara bac
 
Nashangaa sana mbali ya NSSF kuwa ni mfuko wenye sehemu ya matibabu ya wanafamilia yako bado utasikia kuna NHIF na kitu kile kile. Bado unasikia kuna bima ya afya ya mtoto n.k, haya yote ya nini wakati yote ni kwa shughuri ile ile?

Hapo wewe ni mwanaume, kama mkeo naye ni mtumishi nako kuko hivyo hivyo, anakatwa naye kwa familia ile ile na kwa kitu kile kile AFYA. Sasa hivi hii pesa ya mama na baba ya watoto wao, ni kwanini tena mnataka mtoto wao awe na akaunti yake ya kulipia tena 54,000 kwa mwaka? Za wazazi wake zinafanya nini na zinakwenda wapi?
 
Hata bima nayo tatizo. Unajiunga kwa kubembelezwa bima ikiiva hupati hela. Mizunguko yake haina mwisho kama roundabout ya barabara. Hiiii nchi ya maziwa na asali. Ni hatareeeee na ngumu kumeza. Hongra awamu ya tano. Thi is lesson kwa wanachama.
 
Watanzania wanakaangwa kwa Mafuta yao wenyewe kama Nguruwe

Yeye ni Rais wa Ujenzi..amesahau jamii kabisa

Na 2020 Kura ataiba, wala hajali kabisa malalamiko ya wananchi

lengo kuu la CCM ni kutawala, na kuwala na sio Maendeleo yenu watanzania
 
Back
Top Bottom