Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,459
- 29,156
Mfano labda kwa gari ulioiulizia ingawa siijui but ki mfano mfano tu yaweza kama ifuatavyo,kiongozi tufafanulie kidogo hiyo laki mbili kivp?maana kuna siku niliona gari flasn used japan bei ilikuwa kama $500 nilipoeasiliana na kampuni moja hivi inayofanya hayo mambo wakaniambia total ya gharama ni m 8.naomba ufafanuzi zaidi.
Bei ya kununulia kule= Bei uliyopewa = FOB= $500
Ukaguzi/Inspection = $300
Usafiri/Freight = $800
Bima/Insurance = $80
TOTAL/CIF = $1,650.
Kama watuma kupitia benki labda utachajiwa $50 sending fees, inakua $1,700. Ukizidisha kwa rate yetu labda kununua dola utanunua kwa 2,330 utapata kama 4,000,000/- hivi estimate.
Likifika hapa bongo,
Kodi + Usajili = 5,000,000/
Wakala (Mleta mada) = 200,000 - 300,000/,
Kuna Wharfage, DO Charges hapo, tuseme jumla hata 9,500,000/- yaweza kufika.
Huu ni mfano tu jins inavyokua, ila uhalisia wa gharama itategemea na vitu mbalimbali kama vile
1) Aina ya Gari
2) Mwaka wa Matengenezo
3) Ukubwa wa Injini
4) Rate ya kununulia Dola siku hiyo
5) Makato ya Benki kwenye kutuma hela nje
6) Gharama za wakala. Wengine wanachaji mpaka 400,000. Pia hapa kua makini chochote atakachokuanbia amelipa ujiridhishe nacho. Mwengine anakuambia fees yake ni ndogo kumbe kwengine amekubambikia gharama kibao feki kufidia.