Njia za kutumia katika kuchagua wazo bora la Mradi/Biashara

The Consult

JF-Expert Member
Jan 20, 2017
220
252
Group%20of%20happy%20business%20people-Article-201403311817.jpg

Kiuhalisia mawazo ya mradi/biashara yapo mengi sana na huwezi kutekeleza kila wazo ambalo umelipata ima kwa njia fikirishi (brainstorming) au njia nyingine, hii hutokana na ufinyu wa rasilimali (scarcity of resources) ukilinganisha na mahitaji yaliyopo.
Hivyo timu ya mradi (project team) inapaswa kuorodhesha mawazo yote ya mradi/biashara na kisha kuanza kufanyia uchambuzi (analysis) ili kujua ni wazo lipi linafaa na lenye thamani kiutekelezaji (worthing project/business idea)
Vigezo vya awali kabisa vya kuzingatia katika uchambuzi wa mawazo ya mradi/biashara yako ni;
  • Kiwango cha bajeti (budget constraint), hapa utaangalia kiasi cha pesa kilichopo, kwa ulinganisho na kiasi kinachohitajika kwa ajili ya utekelezaji wa wazo la mradi/biashara husika.
  • Urandano na mpango mkakati wa taasisi/kampuni (Strategic plan alignmet), hapa utaangalia ni kwa kiasi gani wazo husika la mradi linaendana na mpango mkakati wa taasisi yako/kampuni yako.
  • Upatikanaji wa taaluma/ujuzi stahiki, hapa utaangalia ujuzi unaohitajika ili wazo la mradi/biashara liweze kutekelezeka, na uwepo wa ujuzi/taaluma hiyo katika taasisi/kampuni yako
Vigezo hivi vitakusaidia kupunguza idadi ya mawazo ya mradi/biashara na kubakia na machache. Baada ya kubaki na mawazo machache ya mradi/biashara (na hapa hushauriwa kubakia na angalau mawazo 3-5) utapaswa tena kufanya uchambuzi wa kina (vigorous selection) wa mawazo hayo ili ubakie na wazo moja.

Katika hatua hii, kuna vigezo vya aina mbili ambavyo hutumika kuchuja mawazo ya mradi/biashara; vigezo vya kifedha (financial criteria) na vigezo visivyozingatia fedha (non-financial criteria).

Vigezo/njia za kifedha katika kuchagua wazo bora la mradi/biashara (financial criteria) kitaalamu hujulikana kama; project financials, financial analysis, business case, au cost/benefit analysis. Njia hizi hujumuisha;
  1. Net Present Value (NPV), njia hii hukusaidia kujua kiasi cha pesa ambacho mradi wako/biashara yako itakuletea baada ya utekelezaji. (Kwa maana nyingine unaangalia thamani ya fedha ya sasa kwa fedha itakayopatikana wakati ujao, present value of all future cash flows)
  2. Internal Rate Of Return (IRR); njia hii hukusaidia kuonyesha kwa uharaka upi mradi utarudisha fedha iliyowekezwa (How rapidly will the money returned?)
  3. Pay back period/time to money; njia hii hukusaidia kuonyesha ni lini/wakati gani mtaji uliowekezwa katika mradi/biashara utarudi kisha uanze kuingiza faida.
  4. Cash hole; njia hii hukusaidia kujua kipindi katika utekelezaji wa mradi/biashara yako ambapo utakuwa umefanya uwekezaji mkubwa.

The Consult; +255 (0) 719 518 367
Dar es Salaam
Tanzania

Kwa huduma za;

  • Uandaaji wa michanganuo ya miradi na mipango mkakati (Project Proposals & Strategic Plans)
  • Utoaji wa ushauri na mafunzo (consultancy & trainings) katika maeneo ya Usimamizi wa Miradi na Mipango Mkakati.
Utafuatwa popote ulipo.
Karibu

Your Success is My Desire
 
I think SWOT analysis can also be applied to choose out the best idea. I agree with you on IRR as the fastest tool to judge the right idea.
 
Group%20of%20happy%20business%20people-Article-201403311817.jpg

Kiuhalisia mawazo ya mradi/biashara yapo mengi sana na huwezi kutekeleza kila wazo ambalo umelipata ima kwa njia fikirishi (brainstorming) au njia nyingine, hii hutokana na ufinyu wa rasilimali (scarcity of resources) ukilinganisha na mahitaji yaliyopo.
Hivyo timu ya mradi (project team) inapaswa kuorodhesha mawazo yote ya mradi/biashara na kisha kuanza kufanyia uchambuzi (analysis) ili kujua ni wazo lipi linafaa na lenye thamani kiutekelezaji (worthing project/business idea)
Vigezo vya awali kabisa vya kuzingatia katika uchambuzi wa mawazo ya mradi/biashara yako ni;
  • Kiwango cha bajeti (budget constraint), hapa utaangalia kiasi cha pesa kilichopo, kwa ulinganisho na kiasi kinachohitajika kwa ajili ya utekelezaji wa wazo la mradi/biashara husika.
  • Urandano na mpango mkakati wa taasisi/kampuni (Strategic plan alignmet), hapa utaangalia ni kwa kiasi gani wazo husika la mradi linaendana na mpango mkakati wa taasisi yako/kampuni yako.
  • Upatikanaji wa taaluma/ujuzi stahiki, hapa utaangalia ujuzi unaohitajika ili wazo la mradi/biashara liweze kutekelezeka, na uwepo wa ujuzi/taaluma hiyo katika taasisi/kampuni yako
Vigezo hivi vitakusaidia kupunguza idadi ya mawazo ya mradi/biashara na kubakia na machache. Baada ya kubaki na mawazo machache ya mradi/biashara (na hapa hushauriwa kubakia na angalau mawazo 3-5) utapaswa tena kufanya uchambuzi wa kina (vigorous selection) wa mawazo hayo ili ubakie na wazo moja.

Katika hatua hii, kuna vigezo vya aina mbili ambavyo hutumika kuchuja mawazo ya mradi/biashara; vigezo vya kifedha (financial criteria) na vigezo visivyozingatia fedha (non-financial criteria).

Vigezo/njia za kifedha katika kuchagua wazo bora la mradi/biashara (financial criteria) kitaalamu hujulikana kama; project financials, financial analysis, business case, au cost/benefit analysis. Njia hizi hujumuisha;
  1. Net Present Value (NPV), njia hii hukusaidia kujua kiasi cha pesa ambacho mradi wako/biashara yako itakuletea baada ya utekelezaji. (Kwa maana nyingine unaangalia thamani ya fedha ya sasa kwa fedha itakayopatikana wakati ujao, present value of all future cash flows)
  2. Internal Rate Of Return (IRR); njia hii hukusaidia kuonyesha kwa uharaka upi mradi utarudisha fedha iliyowekezwa (How rapidly will the money returned?)
  3. Pay back period/time to money; njia hii hukusaidia kuonyesha ni lini/wakati gani mtaji uliowekezwa katika mradi/biashara utarudi kisha uanze kuingiza faida.
  4. Cash hole; njia hii hukusaidia kujua kipindi katika utekelezaji wa mradi/biashara yako ambapo utakuwa umefanya uwekezaji mkubwa.

The Consult; +255 (0) 719 518 367
Dar es Salaam
Tanzania

Kwa huduma za;

  • Uandaaji wa michanganuo ya miradi na mipango mkakati (Project Proposals & Strategic Plans)
  • Utoaji wa ushauri na mafunzo (consultancy & trainings) katika maeneo ya Usimamizi wa Miradi na Mipango Mkakati.
Utafuatwa popote ulipo.
Karibu

Your Success is My Desire
Gharama zenu?
 
Gharama zangu (kiulinganifu ni ndogo sana) na hutegemea ukubwa wa kazi, pia gharama za mradi husika.
Karibu sana Mkuu
Mkuu, weka gharama zako wazi hata kama ni katika mfumo wa asilimia flani ya thamani ya project husika!
 
Mkuu, weka gharama zako wazi hata kama ni katika mfumo wa asilimia flani ya thamani ya project husika!
Mkuu
Gharama ya andiko la mradi kwa ajili ya kuombea ruzuku (grants) natoza 0.9% mpaka 1% ya jumla ya gharama ya mradi (Project Grand Total)
Karibu Sana Mkuu.
 
I think SWOT analysis can also be applied to choose out the best idea. I agree with you on IRR as the fastest tool to judge the right idea.
I am of the idea that in order to win popular/majority community participation during implementation at grass-root level, LFA, PRA, O&OD may be the best Approach in Identifying a Project.
 
I am of the idea that in order to win popular/majority community participation during implementation at grass-root level, LFA, PRA, O&OD may be the best Approach in Identifying a Project.
Definately. However, using PRA for personal project is a big challenge! You need to convene people with risky of early disclosure of your idea to opportunists !
 
I am of the idea that in order to win popular/majority community participation during implementation at grass-root level, LFA, PRA, O&OD may be the best Approach in Identifying a Project.
Hakika, umeeleza jambo la msingi sana Chief.
 
Hivi vi thread vya wajasiariamali vizuri sana lakini wachangiaji wachache .

Kiranga's law of JF participation states that the rate of technical contribution required in a thread is indirectly proportional to the rate of contribution

cc amu
 
Hivi vi thread vya wajasiariamali vizuri sana lakini wachangiaji wachache .

Kiranga's law of JF participation states that the rate of technical contribution required in a thread is indirectly proportional to the rate of contribution

cc amu
thanks Kiranga wangu hapa ni papana sana na mleta mada kastick kajisehemu kamoja tu kaacha papana sana, labda ataendelea zaidi
 
Monitor, kampuni iliyoanzishwa na watu machachari kutoka Harvard akiwepo nguli wa strategies, Michael Porter ilijikuta inatangazwa mufilisi.

Ujasiriamali wa darasani na kwenye uhalisia unatofauti kubwa, wajasiriamali ni watu wa vitendo. Ushauri wenu ni mzuri lakini haumfanyi mtu kufanikiwa. Kuna vigezo na mambo mengi sana ya kuzingatiwa.
 
Nawashauri hawa wanaotoa mafunzo waanzishe biashara mbalimbali na zikishasimama ndio watuuzie hizo biashara(kampuni);nadhani kwa mtazamo huo tutakuwa na biashara nyingi sana na tatizo la ajira litakuwa limeisha
 
Back
Top Bottom