Nitazibaje pengo la marehemu mchumba wangu?

Ni kweli mke mwema hutoka kwa Mungu ila ni lazima umtafute.
 
Bado uko kwenye majonzi...Kila utakaye mpata utamuna hafai... Tulia kwanza... !!
 
Asante kwa ushauri ila hawezi kuja mwenyewe bila kumtafuta.
Pole Sana Mkuu! Naona umeshikilia msimamo wa kuwa ni lazima utafute ndio apatikane. Kabla ya hapo ulisha-date mtu mwingine?? Ni dhahiri bado uko kwenye majonzi yanayokupelekea uamini kuwa yeye ndio kipimo cha mchumba/mke mwema. Kila binadamu ni unique...hakuna wa kufanana na mwingine. Jipe muda na uache kuchambua kila unayekutana nae. Just go out and have fun and the rest will unfold at the right time.
 
Siwezi kupata kama yeye haswa ila bora hata waendane hata kidogo.
Huwezi kupata kama yeye. Utatafuta hadi uzee wako. Wala wa kuendana nae hayupo. My principle is that there shall always be 1 Mother Theresa ; 1 Malcom X ; 1 Nelson Mandela etc. One can only be the best that he/she can be! Maisha yako ni lazima yaendelee na yataendelea kama utaacha kutafuta replacement ya huyo mchumba wako. Muombee apumzike kwa Amani ili na wewe uendelee na maisha yako
 


pole kwa msiba
endelea na maombi mkumbushe Mungu kupitia kifungu hichi Mwanzo 2:20-25
ila sijajua ni dini gani? omba kwa imani kila mtu mume ana mke wake aliyeandaliwa usihofu
 
huwezi kupata mtu anayefanana wewe shida huyo marehemu umemgeuza sanamu kwa hiyo unatamani huku yeye akiwa ndio mfano yeye amekufa unajuaje angekuua wewe
 

Kwanza Pole Ndugu Yangu/kaka Angu!!.
naelewa unavyojisikia kwasasa,hisia zako nazielewa fika!!.hata mimi nilimpoteza niliempenda kwa takribani miaka mitatu akafariki mwaka jana,aliumwa!!.nilijisikia na bado najisikia kama wewe hadi leo,cha muhmu ni kumuombea apumzike kwa amani kila kitu kitaenda sawa usijipe stress,japo ndo hatatokea tena kama huyo.
 
ni vigumu sana pengo lake kuzibika ila endelea kuwa mvumilivu ukifanya papara unaweza pata asiekufaa jitahidi ipo siku utapata atakaekufaa kama marehemu au zaidi ya marehemu.

Pole sana mkuu
 

nicheja me me nlfanana nae marehemu.......sema sasa na hyo mimba aliyokuwa chia na we we umepoteza vgezo vyangu...........
 
Kwahiyo nyie kwenu wanaume mnatiwa mimba? Hiyo tabia yenu sio nzuri,nitawaombea wewe na familia yako muache huo mchezo mchafu.
nicheja me me nlfanana nae marehemu.......sema sasa na hyo mimba aliyokuwa chia na we we umepoteza vgezo vyangu...........
 
Pole kakangu Mungu aendelee kukufariji lakini epuka kufanya ulinganisho tumeumbwa tofauti!
Hivi umesoma hiyo habari ukaielewa mkuu, ebu angalia kwenye red, kweli huyo ni kaka?
 
Pole sana kwa huo msiba mkubwa. Si rahisi kumpata mwingine ambaye ataweza kutimiza vigezo vyote alivyokuwa navyo marehemu. Hivyo amua ni vigezo vipi ambavyo kwako vina umuhimu mkubwa kuwepo katika mahusiano ya kimapenzi ili kuweza kufanya maamuzi ya kumchagua mume mtarajiwa.

Hili la kuwa na BF/GF ambaye vigezo vyake viko juu sana, ikitokea bahati mbaya hawakuoana basi ndio kunakuwa na uwezekano mkubwa wa kuendeleza mahusiano nje ya ndoa. Mume/Mke moyoni mwake anatamani mkewe/mumewe angekuwa yule mwenye vigezo vya juu kabisa aliyewahi kuwa naye miaka ya nyuma lakini bahati mbaya hawako pamoja. Na mawasliano siku hizi yalivyo rahisi basi mmoja anaweza kumtafuta mwenzie na kuanza kukumbushana penzi lao. Kila la heri katika kutafuta kile ukitakacho.


 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…