Naingia moja kwa zote kwenye mada. Nina wasichana wawili mmoja ana kipato namaanisha kazi, msichana wa pili yuko kijijini mkulima, niko kwenye wakati mgumu nahutaji kuoa kati yao.
Na mimi sina kazi naunga unga tu kimjini siku zinaenda.Sasa basi huwa napata msaada wa kifedha kwa huyu msichana mwenye kazi. Pili msichana wa kijijini ananitegemea sana japo halipi kivile ila huyu aliye na kipato anaridhisha sasa.
Naingia moja kwa zote kwenye mada. Nina wasichana wawili mmoja ana kipato namaanisha kazi, msichana wa pili yuko kijijini mkulima, niko kwenye wakati mgumu nahutaji kuoa kati yao.
Kwa hakika hukuanza nao uhusiano katika siku moja, yupo alietangulia.
Muoe wa pili kwa sababu uliona wa kwanza ana mapungufu yasiyovumilika ndio maana ukamtafuta wa pili.
Ukioa huyo wa kwanza utajikuta unarudi tena njia panda.
NA kama imani yako inaruhusu waoe wote, kila mmoja uanze nae hapo ulipo. Sio utafute na mmoja uje kutumia na wawili, ni UNYONYAJI.
Mpigie wa kijijini muulize unapenda kuwa mkia au kichwa na pia muulize huyo wa mjini hivyo hivyo. Majibu yao, ni kwamba moja atakuwa kichwa mwingine mkia, chukua shilingi rusha juu acha ianguke, upande utakaoangukia ndiyo huyo huyo oa.