Nini kifanyike?

dagaa

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2011
Posts
290
Reaction score
382
Habari wana jamvini

Mimi sijui kama ni tatizo au ni uwelewa wangu ni mdogo, mimi naishi na mume wangu, na mwanangu na dada wa kazi, wiki tatu zilizopita niliongea na mume nikamwamwambia nilikua naomba nimlete mtoto wa marehe dada yangu anamjua toka tu wachumba, yupo na bibi yake bukoba, ila anaishi bukoba mjini, muda wote huyo mtoto mimi na mama angu ndo uwa tunamlipia fees na sasa yupo la tano. Mume wangu alinijibu akasema ntakujibu nipe mda nifikilie.

Ikapita wiki mbili nikamkukumbusha akanijibu nitakwambia we tulia tu, leo asubuhi wakati tupo kwa gari nikamuuliza ivi d ulisema unafikilia bado? Akanijibu unajua ukishaanza kuishi na huyo mtoto lazima umtumie nauli aje, umfanyie uamisho na kuna chakula na maradhi, kiukweli hayo mambo ya uamisho na nauli ni juu ya bibi yake, akaona anipe bomu jingine akasema lazima umnunulie nguo, na matumizi mengi, sikupenda kumjibu kwa sabubu mimi nilikua nshaongea nae nimemueleza gharama zote ni za mama, na hata kama angeumwa sana, hata kidogo bibi yake ashindwi kutuma pesa ya matibabu kwa mjukuu wake, na kingine kwa upande wangu nilikua najua atakubali kwanza mwanetu yupo mwenyewe, labda angepata wa kucheza nae. Harafu ni kajiuliza sijui kama kuna mtu anatembea na huai kuna leo na kesho. Katika maongezi akasema kwanza atuna income yoyote tofauti na mshahara, nika mwambia d ndo kwanza tumeamia kwa kibanda chetu, maana mishahara yetu wote ilikua tunaiweka kwa ujenzi, sasa ndo tufikilie bihashara. Na si kwamba atuna plan tunayo.

Ila sa nyingine ukubwa dawa, ile siku ya kwanza namwambia mume wangu kuhusu lile swala na kunijibu anafikilia, mama yangu alinijibu labda hataki, muache ntaendelea kukaa nae, mimi nikawa namwambia mama tumsikilize labda atakubali, ila majibu yanaonyesha kabisa hataki kuishi na huyo mtoto.

Swali langu ni vibaya kuishi na ndugu, make hata mimi nimelelewa na kaka zangu, na yeye pia vivyo hivyo kalelewa na ndugu, au ni mtu hasiyependa mwingiliano wa watu? NAMI NAONA NISIMUULIZE TENA SWALA HILI, ILA NAYE NDUGU ZAKE WAKIJA NI WAFANYIE VITUKO? Ila wakati mwingine ni roho ya mtu kama huna roho mbaya au ya ukatili uwezi, kama mimi na hisi roho mbaya siwezi kabisa.
 
Hayo ndo madubwana ya ndoa kulaleki waweza dhani watu wenye roho mbaya wanakaa labda msitu wa pande kumbe ndo hao hao tunaokula nao,sex nao,cheka nao in short ni party ya jamii yetu kabisa directly.
Back to the topic hebu we muache usilazimishe maana huyo mtoto anaweza kuja kutibua ndoa yenu kwa sababu hakuna sababu ya msingi sana ya yeye kuhamia kwako coz inaonesha mama yako anajiweza kimapato na wewe kama utaguswa utakuwa unatuma fedha za mahitaji.
Haya ndo mambo kaka Mtambuzi huwa anayazungumzia kila siku MUNGU akupe maisha marefu kwa kuielimisha jamii na threads zako.
 
Last edited by a moderator:
Mlikubaliana naje.. Hapo awali katika maswali ya kuishi na ndugu/kusaidia ndugu???

Awe wa kwako au wa kwake??



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Sema nae kwa upole mumeo ila kwa kweli kuishi na ndugu wakati mwingine ni kazi lazima atawakwaza tu
 
This is highest level of selfishness I ever seen,,,,

Hivi mtoto mmoja anaharibu kitu, tena mtoto wa marehemu...

Hizi ndo hizi ngoja tuingie tukaone wenyewe...
 
huyo hataki ,wala usimlazimishe,mwache mtoto akae tu na bibi yake ,ila sio fair kwa kweli
 
This is highest level of selfishness I ever seen,,,,

Hivi mtoto mmoja anaharibu kitu, tena mtoto wa marehemu...

Hizi ndo hizi ngoja tuingie tukaone wenyewe...
jana mlitusema sana na yule mama alogoma kuuguza wakwe . wanawake jana tulionekana wabayaa..leo mnalo kumbe na nyie mnazo roho mbaya eeeh!
 
Mara nyingi Mwanaume anajaribu kupunguza gharama za mjini(dar) ili aweze kufanya vitu vingine, so usimchukulie vibaya
 
jana mlitusema sana na yule mama alogoma kuuguza wakwe . wanawake jana tulionekana wabayaa..leo mnalo kumbe na nyie mnazo roho mbaya eeeh!


Maisha yanavyozidi kubana, watu roho mbaya zinazidi hadi zinapitiliza..

My mother used to tell me "we are born with two hands, one to help yourself and a second one to help others,,,

Tujitahidi sana kuukimbia umaskini, ni mbaya sana unasababisha tuwe na roho za ajabu..
 
Asante dada white kwa ushauri, ila hata mimi nimefikilia sana nimeona simuulizi tena, ila pesa tangia hapo uwa natuma. :nono:
 
Mara nyingi Mwanaume anajaribu kupunguza gharama za mjini(dar) ili aweze kufanya vitu vingine, so usimchukulie vibaya
sijamchukulia vibaya sema, si dhani kama kuna gharama zinaongezeka, make kila kitu ni bibi yake labda maradhi na chakula, labda ungeniambia ni roho ya mtu.. hata ivyo sijamchukia yule ni mume wangu
 
huyo hataki ,wala usimlazimishe,mwache mtoto akae tu na bibi yake ,ila sio fair kwa kweli
Ni kweli make mtu kama hataki uwezi kumlazimisha, harafu wakati mwingine uwezi jua Mungu anakuepushia na nini.
 
This is highest level of selfishness I ever seen,,,,

Hivi mtoto mmoja anaharibu kitu, tena mtoto wa marehemu...

Hizi ndo hizi ngoja tuingie tukaone wenyewe...
Kweli MKATA KIU unajua maisha ndo yalivyo, yamejaa changamoto, na kila changamoto ina sababu yake
 
sijamchukulia vibaya sema, si dhani kama kuna gharama zinaongezeka, make kila kitu ni bibi yake labda maradhi na chakula, labda ungeniambia ni roho ya mtu.. hata ivyo sijamchukia yule ni mume wangu

Najua ni Mume wako, lakini usikae kimya mueleze ukweli amekosea,, nina imani wakristo na ndoa mlifunga kanisani,, sasa kanisa gani linaruhusu roho hiyo,,, hamuoni hata aibu jumapili mnapoenda kanisani mnaabudu nini sasa kama yupo hivyo..

Mtu akikosea mweleze ukweli ili abadilike... Huwezi jua kuna leo na kesho mnaweza mkapata ajali we na mumeo na mtoto wenu akalelewa na Ndugu,,, huyo dada akupenda kufa ili amwache mtoto wake...

Gharama za kulea mtoto wa std 5 sio kubwa ya kutisha,, wanaume tuna matumizi ya kijinga kibao mfano bar, sasa ukipunguza hayo kumsaidia mtoto sio mbaya
 

Acha nikuambie kitu dada dagaa.
Si vibaya kuishi na ndugu, wala si vibaya kusaidia ndugu anapokuwa anahitaji msaada wako. LAKINI.. Siku zote jitahidi sana kumsaidia mtu huko aliko badala ya kumhamishia nyumbani kwako! Hasa pale ambapo mtu huyo atakuja kukaa kwa muda mrefu (mf. kusoma). Mimi nnakiona anachojaribu kukwepa mumeo tena kwa nia njema kabisa. Leo utamchukua huyo mtoto, atakuja kukaa hapo kwenu. Kesho nayeye mdogo wa kakaake na shemeji yake atapata matatizo, atamleta hapo kwenu, na wewe huwezi kukataa maana si ulishamleta mdogo wako? Keshokutwa sijui nani huko kijijini atakuja kutafuta kazi mjini, atafikia kwenu. Before u know it, nyumba itakuwa imejaa watu kila mmoja na tatizo lake na wote hawana wanachokifanya zaidi ya kusubiri ugali wa kengele mchana, huku wakilala sebuleni, store, na wengine ukienda kuwaombea kwa majirani! Nakuambia hata hizo plan zenu za kufungua biashara hutajua zilikopotelea kwa jinsi garama za maisha zilivyo juu. Kwa sasa huwezi kuliona hilo, lakini mark my words, the moment unamkaribisha mtu mmoja, umefungua milango! Mbaya zaidi, nyumba ikishajaa watu namna hiyo, hata ule uhuru wenu wa kufanya mambo unapungua. Mumeo atakuwa hana hata hamu ya kurudi nyumbani mapema.. utarudi hapa kuomba ushauri.
Im talking from experience dada angu.
 
Ni kweli DADA WHITE hata mimi nimefikilia hivyo, nitamwacha kwa mama yangu na matumizi nitakuwa natuma, na toka zamani nilikua natuma,
 
ok mkubwa asante kwa ushauri
 
Huyo hataki,mwache mtt akae kwa bibi
ukilazimisha ndio inafikia ile ya mtt kafanyiwa ukatili,lkn angejua ni baraka kukaa na huyo mtt angekubali,so sad!
 
Pole shosti,usimlazimishe kama ukishaona majibu yenyewe ni hayo,mimi nimlea mjukuu wa shangazi yangu wazazi wake wote wamefariki lakini sikutaka ugomvi kukaa nae nimempeleka bording school anakuja wakati wa likizo yote sikutaka maneno na mume nimekubali kulipa hela nyingi lakini iwepo amani,sasa bora uachane na kumuliza hizo story,kwanza mtoto wa kike kama bibi yake yupo basi bora,mwenyezi mungu ameijua nia yako nini kwa huyo mtoto...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…