Nini hatma ya hamad rashid katika siasa?

Nini hatma ya hamad rashid katika siasa?

Juma Salum

Member
Joined
Dec 19, 2011
Posts
7
Reaction score
1
Kwa kweli nimepokea kwa masikitiko sana kwa uamuzi wa CUF mliochukua kuhusu Hamad,sidhani kama ni uamuzi wa busara uliofanyika. HAMAD ni kiongozi shupavu na ndiyo hata sisi wananchi tulijua ipo siku atakuwa katika madaraka makubwa ya uongozi ndani ya CUF,sasa kwa hili nadhani viongozi wa CUF ni kama mmejichimbi kabuli ili mfukiwe na kufa kabisa,nguvu mliokuwa nayo kisiasa mnaiondoa na naiman maamuzi yenu mtayajutia,tatizo hasa silijui kwa undani lakini sidhani kama lazima liwapelekeeni katika maamuzi haya.
Kuna viongozi wachache sana wenye fikra na maono ya uongozi kama HAMAD,asimamapo bungeni na kuongea watu wote huwa tunafurahi kwani hugusa matakwa ya wananchi. CUF tambueni mna wabunge wachache bara,wengi wapo visiwani lakini bado hao hao mliokuwa nao mnawapunguza sasa hizi ni akili au kitu gani, hao CCM wenyewe hawapunguzi wabunge wao kuogopa kupungukiwa na wawakilishi bungeni lakini nyinyi wenye wachache mnawapunguza!. Nwaombeni CUF mfikilie kwa makini swala hili,tunaitaji ushindani katika siasa ili wananchi tupate viongozi wa kweli na si bora viongozi.
 
Back
Top Bottom