Nini dawa ya vidonda vya koo?

Nini dawa ya vidonda vya koo?

yorkshire

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2016
Posts
2,533
Reaction score
3,175
Ndugu yangu anasumbuliwa sana na vidonda kooni kwa muda mrefu kiasi hata kumeza hata maji tu inamletea maumivu, ametumia Pen V mpaka basi lakini hakuna kitu, Mwenye ufahamu wa dawa atiririke hapa.
 
Aende Hospitali akapate vipimo kwanza kabla yakutumia dawa yeyote ile.
 
Ili apate tiba ni muhimu akafunguka kwanza chanzo ni nini?

Maana naskia hata kama mtu akipenda kulamba chumvi sana huwa matokeo yake Ni vidonda.
 
Ndugu yangu anasumbuliwa sana na vidonda kooni kwa muda mrefu kiasi hata kumeza hata maji tu inamletea maumivu, ametumia pen v mpaka basi lakini hakuna kitu ,mwenye ufahamu wa dawa atiririke hapa.
Vidonda vya koo huwa pia ni dalili ya kansa ya koo ambayo kwa sasa inashika kasi sana ikiwaathiri zaidi vijana waliopo katika umri wa kati ya 20 hadi 30 maana hawa ndio mabingwa wa kupeleka midomo na ndimi zao huko uvunguni yaani oral sex a.k.a uvinza.

Na hawa wanawake wanaofanya na wenzao kupitia oral sex then huwa wanajipa sana infections midomoni kwa sababu kule uvunguni kuna bakteria wengi sana wa magonjwa mbali mbali, eg. UTI, gonorrhea, PID, etec ambao wao huwabebelea midomo bila kujijua na kuja kukutana na wewe mkapeana busu zito la mahaba ile hali anakuhamishia wewe hayo madudu bila kujijua then unapata maambukizi kooni na hatimae vidonda huanza na kuchochea kansa ya koo.

Haya magonjwa kusambaa inasababishwa sana na kukosa msimamo wa kuwa na mtu m'moja tu katika mahusiano.

Ukitaka takwimu zaidi nenda pale hospital ya ocean road utajionea kwa wingi wao.
 
Ndugu yangu anasumbuliwa sana na vidonda kooni kwa muda mrefu kiasi hata kumeza hata maji tu inamletea maumivu, ametumia pen v mpaka basi lakini hakuna kitu ,mwenye ufahamu wa dawa atiririke hapa.
Mwambie ndugu yako aache upumbavu, mtu anaumwa halafu anakaa nyumbani anategemea ushauri atapewa na watu baki badala ya kwenda hospital tena kubwa kupewa majibu ya vipimo?!

Aende hospital chap
 
Mwambie ndugu yako aache upumbavu, mtu anaumwa halafu anakaa nyumbani anategemea ushauri atapewa na watu baki badala ya kwenda hospital tena kubwa kupewa majibu ya vipimo....?!

Aende hospital chap
Ujumbe umemfikia nitampa majibu yake mujarabu kbs

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Karibu asilimia 90 ya vidonda vya koo husababishwa na viru. Virus havina dawa kwahiyo hiyo pen v haisaidii kitu.
Ukiona vidonda vya koo vimeambatana na mafua ujue moja kwa moja ni virus. Hapo ant biotic hazitafanya kitu.

Piga dawa za kutuliza. Cetirizine, za maji, za maumivu na jifukize.
 
Ndugu yangu anasumbuliwa sana na vidonda kooni kwa muda mrefu kiasi hata kumeza hata maji tu inamletea maumivu, ametumia Pen V mpaka basi lakini hakuna kitu, Mwenye ufahamu wa dawa atiririke hapa.
Nenda Rabininsia hospitali iliyoko NAMANGA kama unaelekea Bunju.
Ukifika pale watafute wataalam wa ENT (Masikio,Pua na Koo)
Watakusaidia...walinisaidia na mm.
Utapewa dawa za mwezi au miezi miwili kutegemeana na maendeleo yako
 
Ndugu yangu anasumbuliwa sana na vidonda kooni kwa muda mrefu kiasi hata kumeza hata maji tu inamletea maumivu, ametumia Pen V mpaka basi lakini hakuna kitu, Mwenye ufahamu wa dawa atiririke hapa.
Acyclovir tabs ilinisaidia sana, ila nilitibiwa TMJ enzi hizo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom