Ningejiuzulu!

Ningejiuzulu!

tubalayya

Member
Joined
Apr 16, 2010
Posts
69
Reaction score
105
Najua fika haitafanyika hivyo. Ila si vibaya kutoa ushauri kwa vile yaelekea wenye kazi hiyo aidha wanaogopa, wanaona ni kazi bure au hawamtakii mema rais wetu. Si kwamba hawajui.

Hata saa hii, saa kumi na mbili kasorobo, bado kuna wakati kwa rais Samia kuokoa kilichobaki katika heshima na utu wake. Lakini akiishinda ego.

Ego, ( nafsi, kiburi, kuonekana, kutoambilika), ndiyo ilimfanya Shetani akosane na MMungu hadi akamfukuza milele, ingawaje Yeye Allah ni Mwingi mno wa kusamehe na wa huruma.

Ego, ndiyo sifa mbaya zaidi katika nafsi ya binadamu, na ndiyo sababu ya msingi ya majanga na kila maovu. Mtu ataiba mabilioni, atachukua rushwa, atakusanya vito vya fahari......si kwa sababu anavihitajia vyote hivyo! Ego.

Ego yaweza kumrubuni rais kwamba akiondoka yeye hakuna mwingine atayeweza kuongoza nchi. Au kumpotosha kuwa haya yatapita tu, au yote yaliyotokea ni njama za nje au Dini fulani!
Maoni yangu ni kuwa kuachia madaraka hivi sasa kungemrejeshea baadhi ya heshima na hata pengine huruma. Actually, watu huwa wanamsamehe haraka mtu anayejiuzulu (Mwinyi, Sokoine...)

Kama ningekuwa miye >
1. Ningelihutubia Taifa na kukiri bila kuuma maneno, kwamba makosa yalifanyika, na mimi, kama Kiongozi Mkuu, nachukua majukumu yote.

2. Ningeomba msamaha wa dhati kwa wananchi, kuahidi wote waliohusika kuchukuliwa hatua, na wote walioathrika kupatilizwa yaliyowasibu. Ningeunda mara moja kikosi kazi cha kuwatafuta na kuwarudisha wote waliopotea, ikiwemo miili ya marehemu, kuwaachia wafungwa wa kisiasa, na kuweka mipango ya kulipa ridhaa.

3. Ningetangaza kujiuzulu rasmi katika muda nitakaouanisha kwa mujibu wa taratibu za Katiba zinazoelezea nini kifanyike katika hali hiyo.

4. Ningeitisha mkutano wa maridhiano ya Kitaifa.
Kwa kuendelea kuongoza katika hali hii si tu makosa zaidi yatafanyika siku hadi siku. Na hata asipofanya makosa, kwa wengi, kila atakalolifanya halitaonekana zuri, hata akiamua kumpa kila Mtanzania nusu kilo ya dhahabu! Rais Samia asiamini kabisa kuwa Watanzania wengi na Dunia wanaamini kuwa ameshinda uchaguzi.

Hata akiamua kubakia, njia pekee ni kurudia uchaguzi.
Kuendelea kuongoza, inevitably, hiyo itabakia kuwa sumaku ya machafuko na migogoro. Aidha, Tanzania itaathirika na kusuasua (hatuna wakati; mwaka 2035 tutakuwa milioni 100). Asilimia 30 ya bajeti ya Tanzania yategemea misaada na mikopo.

Kamwe hakutakuwa na misaada kwa miaka mitano. Hii kusema "tutajitegemea, tutakaza mkanda, who're you, ni heri kula majani..." siyo scientific! Wachina, Warusi au Wahindi watatusaidia, technically, lakini hawana liquidity (fedha rojorojo).

Deni la nje la Tanzania linakaribia kula asilimia 45 ya GDP (mapato yote) yetu. Tutalipaje! Baya zaidi, bila mabadiliko, kuna uwezekano wa vikwazo zaidi vya uchumi.

Kwa maslahi ya Tanzania...
Huu ndio ushauri wangekupa washauri wako. Lakini...nani '(atamfunga paka kengele)'###
Naaa......'hoja haipigwi gongo'.
 
Na Kwa Sasa anaumwa sana hadi anapumua Kwa mashine
 
Ajiudhuru ashitakiwe kirahisi?
Hiyo sahau.
Alikosea angejiudhuru kabla ya kutoa amri ya shoot to kill mtu yeyote anayetoka nje wakati wa curfew baada ya uchaguzi.
Angekataa kutangazwa mshindi kinguvu kwa matokeo yenye utata. Angesamehewa na kushangiliwa kwamba kafanya jambo la kizalendo kwa taifa kukataa kumwaga damu.
Kwa sasa hata mimi ningekuwa mshauri wake ningemshauri ang'ang'anie hadi kifo.
Akimaliza mitano bado atashitakiwa huko kimataifa au warithi watabadili katiba na kumuondolea kinga ashitakiwe ndani.
Nafasi finyu ya kukwepa adhabu ipo, akiweza ajiondolee kinga ashitakiwe mahakama za ndani ila atumie vyombo vyake kuhakikisha ushahidi dhidi yake unakosekana. Hapo atatoboa. Ila kwenye harakati za kupoteza ushahidi asiuwe watu sababu chuki dhidi yake zitazidi atapinduliwa haraka.

Note: Siungi mkono mauwaji na ukandamizaji haki. Hapo nimejaribu kuwa neutral na kuvaa nafasi yake kwenye janga hili linalomkabili.
 
Ukisikiliza simulizi za waliokamatwa au waliopoteza ndugu na rafiki kwenye janga hili. Watu wameteswa na kuonewa sana na vyombo vya dola, Kimakosa au kwa makusudi.
Utaona kuna hasira na chuki kali sana dhidi yake na CCM.
Safari hii hili halitapita bila kuondoka na watu wazito. Inaweza kuja kulipuka vurugu kubwa sana na vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Uhasi waja kusipochukuliwa hatua sahihi.
 
Ajiudhuru ashitakiwe kirahisi?
Hiyo sahau.
Alikosea angejiudhuru kabla ya kutoa amri ya shoot to kill mtu yeyote anayetoka nje wakati wa curfew baada ya uchaguzi.
Angekataa kutangazwa mshindi kinguvu kwa matokeo yenye utata. Angesamehewa na kushangiliwa kwamba kafanya jambo la kizalendo kwa taifa kukataa kumwaga damu.
Kwa sasa hata mimi ningekuwa mshauri wake ningemshauri ang'ang'anie hadi kifo.
Akimaliza mitano bado atashitakiwa huko kimataifa au warithi watabadili katiba na kumuondolea kinga ashitakiwe ndani.
Nafasi finyu ya kukwepa adhabu ipo, akiweza ajiondolee kinga ashitakiwe mahakama za ndani ila atumie vyombo vyake kuhakikisha ushahidi dhidi yake unakosekana. Hapo atatoboa. Ila kwenye harakati za kupoteza ushahidi asiuwe watu sababu chuki dhidi yake zitazidi atapinduliwa haraka.

Note: Siungi mkono mauwaji na ukandamizaji haki. Hapo nimejaribu kuwa neutral na kuvaa nafasi yake kwenye janga hili linalomkabili.
alaa! kumbe watu kama nyie wako wengi? Ambao maslahi mapana ya nchi hayana umuhimu zaidi ya malahi finyu binafsi! Basi kumbe tunatastahiki viongozi kama hawa ikiwa akili zetu zimeumbwa hivi. Kuna Mwanafalsafa mmoja wa Kifaransa aliwahi kusema: 'L'esclavage est ce que veut l'esclave' yaani 'Utumwa ndiyo kitu hasa anachokipenda mtumwa'. Unathibitisha hilo. Tusiwalaumu madikteta, wauza watu wala wakoloni kwani hayo ndiyo hasa tuyatakayo!
Ni kujiuzulu, hakuna Kiswahili cha kujiudhuru!
 
alaa! kumbe watu kama nyie wako wengi? Ambao maslahi mapana ya nchi hayana umuhimu zaidi ya malahi finyu binafsi! Basi kumbe tunatastahiki viongozi kama hawa ikiwa akili zetu zimeumbwa hivi. Kuna Mwanafalsafa mmoja wa Kifaransa aliwahi kusema: 'L'esclavage est ce que veut l'esclave' yaani 'Utumwa ndiyo kitu hasa anachokipenda mtumwa'. Unathibitisha hilo. Tusiwalaumu madikteta, wauza watu wala wakoloni kwani hayo ndiyo hasa tuyatakayo!
Ni kujiuzulu, hakuna Kiswahili cha kujiudhuru!
Nadhani umesoma na hukunielewa kwenye haya yangu ya mwisho ya hitimisho. Au haukusoma?
Hapo ndipo kuna msimamo wangu binafsi. Maelezo yaliyo tangulia I was only stating the obvious. Nikijaribu kuonesha sababu kwanini hajajiudhuru.
Pia hujanifuatilia humu JF nasimamia upande upi wa siasa za Tanzania na hasa mauwaji ya 29/10/2025.
It seems we have a very big problem when it comes to comprehension (reading and understanding) skills among Tanzanians. I don't know wether it's an individual problem or our education system.
 
Nadhani umesoma na hukunielewa kwenye haya yangu ya mwisho ya hitimisho. Au haukusoma?
Hapo ndipo kuna msimamo wangu binafsi. Maelezo yaliyo tangulia I was only stating the obvious. Nikijaribu kuonesha sababu kwanini hajajiudhuru.
Pia hujanifuatilia humu JF nasimamia upande upi wa siasa za Tanzania na hasa mauwaji ya 29/10/2025.
It seems we have a very big problem when it comes to comprehension (reading and understanding) skills among Tanzanians. I don't know wether it's an individual problem or our education system.
Who told you I was educated in Tanzania? Those who write 'kujiudhuru' instead of 'kujiuzulu' certainly were!
 
Ngoja nimsaidie hapa kwa msaada wa akili mnemba


Wananchi wenzangu wa Tanzania,

Leo, tarehe 8 Januari 2026, nimeamua kuwasiliana nanyi moja kwa moja kupitia hotuba hii maalum. Nimekuwa Rais wenu tangu mwaka 2021, na nimejitahidi kwa moyo wote kuwahudumia na kuongoza nchi yetu kuelekea maendeleo, amani na umoja.

Lakini, matukio ya Oktoba 29, 2025, wakati wa uchaguzi mkuu na maandamano yaliyofuata, yamekuwa na athari kubwa sana kwa nchi yetu. Mauaji ya raia wetu wengi, majeruhi, na mateso yaliyotokea wakati huo yameniumiza moyo wangu sana. Ingawa niliteua tume ya uchunguzi na nilitoa maagizo ili kushughulikia suala hilo, nimeona kwamba watu wengi bado wana maumivu makubwa, na imani kwa uongozi wangu imepungua sana.

Kama Rais, nina wajibu wa kuhakikisha amani, haki na umoja wa taifa letu. Lakini kutokana na msingi wa matukio hayo makubwa ambayo yalitokea chini ya uongozi wangu, nimeamua kwamba njia bora ya kurejesha imani na kutoa nafasi ya upya ni kujiuzulu wadhifa wangu wa Urais.

Kwa hiyo, kuanzia sasa hivi, ninajiuzulu rasmi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nitafuata taratibu za Katiba yetu ili makamu wa Rais achukue wadhifa huo kwa muda, na kuwapa nafasi Wabunge na taasisi zetu kushughulikia mabadiliko yanayohitajika.

Ninawaomba msamaha wananchi wote, hasa familia za waliofariki dunia, waliojeruhiwa na walioteseka kutokana na matukio hayo. Moyo wangu uko nanyi. Ninataka nchi yetu iendelee kuwa na amani, na ninaamini kwamba hatua hii itasaidia kurejesha umoja wetu.

Tanzania ni nchi yetu sote. Tuendelee kuilinda na kuijenga kwa pamoja.

Mungu ibariki Tanzania.
Mungu awabariki ninyi nyote.

Asanteni sana.
 
Who told you I was educated in Tanzania? Those who write 'kujiudhuru' instead of 'kujiuzulu' certainly were!
As an expert in language, you should have been smart enough to understand my last paragraph.
Comprehension!!!!!!!
Kama hili tatizo la kusoma na kuelewa siyo lako binafsi mfumo wa elimu uliyopitia.
Rudi kadai pesa yako nchi ulikopata elimu yako.
Kipengele cha ufahamu (kusoma na kuelewa maana ya ulichosoma) unaanza kufundishwa mwanzo kabisa wa safari ya kutafuta elimu hasa kwenye somo la lugha yeyote duniani.
BTW, I'm not an expert in linguistics.
 
As an expert in language, you should have been smart enough to understand my last paragraph.
Comprehension!!!!!!!
Kama hili tatizo la kusoma na kuelewa siyo lako binafsi mfumo wa elimu uliyopitia.
Rudi kadai pesa yako nchi ulikopata elimu yako.
Kipengele cha ufahamu (kusoma na kuelewa maana ya ulichosoma) unaanza kufundishwa mwanzo kabisa wa safari ya kutafuta elimu hasa kwenye somo la lugha yeyote duniani.
BTW, I'm not an expert in linguistics.
let's end it there. We have more serious issues to ponder and resolve, rather than the luxury of indulging in this malignant narcissism.
 
Ngoja nimsaidie hapa kwa msaada wa akili mnemba


Wananchi wenzangu wa Tanzania,

Leo, tarehe 8 Januari 2026, nimeamua kuwasiliana nanyi moja kwa moja kupitia hotuba hii maalum. Nimekuwa Rais wenu tangu mwaka 2021, na nimejitahidi kwa moyo wote kuwahudumia na kuongoza nchi yetu kuelekea maendeleo, amani na umoja.

Lakini, matukio ya Oktoba 29, 2025, wakati wa uchaguzi mkuu na maandamano yaliyofuata, yamekuwa na athari kubwa sana kwa nchi yetu. Mauaji ya raia wetu wengi, majeruhi, na mateso yaliyotokea wakati huo yameniumiza moyo wangu sana. Ingawa niliteua tume ya uchunguzi na nilitoa maagizo ili kushughulikia suala hilo, nimeona kwamba watu wengi bado wana maumivu makubwa, na imani kwa uongozi wangu imepungua sana.

Kama Rais, nina wajibu wa kuhakikisha amani, haki na umoja wa taifa letu. Lakini kutokana na msingi wa matukio hayo makubwa ambayo yalitokea chini ya uongozi wangu, nimeamua kwamba njia bora ya kurejesha imani na kutoa nafasi ya upya ni kujiuzulu wadhifa wangu wa Urais.

Kwa hiyo, kuanzia sasa hivi, ninajiuzulu rasmi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nitafuata taratibu za Katiba yetu ili makamu wa Rais achukue wadhifa huo kwa muda, na kuwapa nafasi Wabunge na taasisi zetu kushughulikia mabadiliko yanayohitajika.

Ninawaomba msamaha wananchi wote, hasa familia za waliofariki dunia, waliojeruhiwa na walioteseka kutokana na matukio hayo. Moyo wangu uko nanyi. Ninataka nchi yetu iendelee kuwa na amani, na ninaamini kwamba hatua hii itasaidia kurejesha umoja wetu.

Tanzania ni nchi yetu sote. Tuendelee kuilinda na kuijenga kwa pamoja.

Mungu ibariki Tanzania.
Mungu awabariki ninyi nyote.

Asanteni sana.
Utaonekana msanii(humaanishi) kwa sababu ya ile hotuba ya "WHO ARE YOU"
 
Back
Top Bottom