Nimependa Haya Maneno

Nimependa Haya Maneno

Ambiele Kiviele

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
15,271
Reaction score
29,934
NIMEYAPENDA SANA HAYA MANENO

Mwanamke ni kama Jua unaweza
usione umuhimu wake, yaani kila
siku unaenda mjini jua lipo tu,
unaliangalia lakini huangalii umuhimu
wake kwako.

Wakati mwingine likiwa
kali unaanza kulalamika kuwa
linachoma na lina kera. Lakini
ukitafakari kidogo tu utajua kuwa bila
jua maisha yasingekuwepo.

Hembu
chukulia mfano mchana kungekuwa
giza tu kama usiku nini kingetokea?
Chakula tunachokula ni kwasababu
ya Jua, mvua ikinyesha sana
mafuriko yakitokea tunatamani jua,
kwenye baridi tunatamani pia jua,
Hatuliwazii kwasababu lipo tu na
linatimiza majukumu yake kimya
kimya bila kelele.

Hiyo ni sawa na
mwanamke, ukishaoa kuna mambo
ambayo mwanamke huyafanya na
baada ya muda unaanza kuyaona ya
kawaida kawaida, chakula kinakuwa
mezani kila siku hujui kinapikwaje na
vyombo vinaoshwaje, anabeba
mimba na watoto wanazaliwa hujui
maumivu aliyoyapata lakini
unatabasmu na kucheka ukijisifia
watoto wangu na hata mkigombana
unasema niachie wanangu wewe
nenda tu tafikili unajua maumivu
aloyapata kipindi anawaleta duniani
ao watoto.

Watoto wanaumwa mpaka
wanapona hujui hata wameponaje,
wanalia usiku hujui hata nani alikuwa
anawabembeleza, ukirudi unakuta
nguo safi chumba kisafi hutoi hata
shukurani kwakuwa ushasahau kua
kuna mtu anasafisha siwe safi muda
wote.

Na anafanya vitu vyote hivyo
kama Jua bila kelele lakini wewe
ukitoa elfu mbili ya sukari
utamnynayasia mpaka ndugu zake
kuwa unawalisha wewe!

Hembu siku
aondoke akuachie hao watoto
unaojisifia kila siku kuwa ni wakwako
na kumuambia hajaja na kitu, uanze
kuwapikia na kuwaandaa kwenda
shule, ufue nguo zao na zako.

Unaweza kuajiri mfanyakazi lakini
hawezi kufanya hata nusu ya kile
anachokufanyia mkeo, kwani yeye
atafanya kama kazi lakini mkeo
anafanya kwa mapenzi, hahitaji
umlipe chochote zaidi ya kutimiza
majukumu yako na kumheshimu
kama mke katika maisha yenu.

Vuta
picha umeamka mkeo hayupo, watoto
wanataka kuogeshwa kunywa chai na
kwenda shule, hapo unatakiwa
kuwahi kazini na mchana watoto
wale! Mheshimu sana mkeo kuna
mambo mengi ambayo anayafanya
ukiambiwa uyafanye ww
utachanganyikiwa na mkeo huyafanya
kwa upendo.

Mwanamke anachohitaji
kwa mume ni upendo na heshima tu.
Mhudumie, mpe upendo, muheshimu
na muonyeshe kuwa kwako ana
umuhimu mkubwa, mfanye mkeo
atabasamu kila mara na familia nzima
itatabasamu
 
Umenenena, sijui mama au Dada? Au mbaba maana humu watu hawatumii majinayao kamili.
 
Wanawake !!!!!! wanaimbiwa nyimbo wao,wanatafutiwa pesa wao,wanatungiwa mashairi wao!
 
Vipi haya

"
a woman is like a swimming pool, don't bother who swam before you..who is swimming with you or who will swim after you. "
 
Vipi haya

"
a woman is like a swimming pool, don't bother who swam before you..who is swimming with you or who will swim after you. "
Ibadilishe kwa sisi wa St Kayumba tupate kuelewa plz
 
Wanawake ni sawa na kuku,kuna aina mbili za kuku ambao ni wakufuga ambao ni wa kienyeji kuliwa kwa mpangilio lakn hawa wa kisasa ni kwaajili ya nyama tu,hivyo kuna mke na wengne wa kutimiza haja ya mwanaume tu,hawafai kuolewa kabisa ukioa ni hasara tupu,lakin wale wafaao kuitwa mke hata ukioa maisha una furahia
 
Wanawake ni sawa na kuku,kuna aina mbili za kuku ambao ni wakufuga ambao ni wa kienyeji kuliwa kwa mpangilio lakn hawa wa kisasa ni kwaajili ya nyama tu,hivyo kuna mke na wengne wa kutimiza haja ya mwanaume tu,hawafai kuolewa kabisa ukioa ni hasara tupu,lakin wale wafaao kuitwa mke hata ukioa maisha una furahia
 
Wanawake ni sawa na kuku,kuna aina mbili za kuku ambao ni wakufuga ambao ni wa kienyeji kuliwa kwa mpangilio lakn hawa wa kisasa ni kwaajili ya nyama tu,hivyo kuna mke na wengne wa kutimiza haja ya mwanaume tu,hawafai kuolewa kabisa ukioa ni hasara tupu,lakin wale wafaao kuitwa mke hata ukioa maisha una furahia
Dahh.. nimecheka sana Mkuu,.......
 
Wanawake ni sawa na kuku,kuna aina mbili za kuku ambao ni wakufuga ambao ni wa kienyeji kuliwa kwa mpangilio lakn hawa wa kisasa ni kwaajili ya nyama tu,hivyo kuna mke na wengne wa kutimiza haja ya mwanaume tu,hawafai kuolewa kabisa ukioa ni hasara tupu,lakin wale wafaao kuitwa mke hata ukioa maisha una furahia
Kwahiyo nyie ni sawa na jogoo???
 
Acha kuwaza upumbavu wewe, soma Maandiko Matakatifu utaelewa mwanamke ni nani. Haya yote mbona yamo Maandikoni! Uvivu wenu unawafanya muwe watumwa kila siku na mkishaandika hivi vidude vyenu basi mnajiona wavumbuzii!

Imeandikwa, "Mwanamke atazaa kwa uchungu."

"Mwana mwenye hekima humfurahisha babae, bali mwana mpumbavu ni mzigo wa *****. Hapo wadhan nan anaetakiwa kufunza mtoto adabu?
 
Acha kuwaza upumbavu wewe, soma Maandiko Matakatifu utaelewa mwanamke ni nani. Haya yote mbona yamo Maandikoni! Uvivu wenu unawafanya muwe watumwa kila siku na mkishaandika hivi vidude vyenu basi mnajiona wavumbuzii!

Imeandikwa, "Mwanamke atazaa kwa uchungu."

"Mwana mwenye hekima humfurahisha babae, bali mwana mpumbavu ni mzigo wa *****. Hapo wadhan nan anaetakiwa kufunza mtoto adabu?
Sikatai maoni yako lakini hao unao waongelea wew ni wanawake wanao jitambua na kujua wajibu wao wa family kuna wanawake wengne hawajui nini maana ya ndoa mfano,umeoa mwanamke lakn chakula anakupikia house girl,kitanda anatandka house girl,nguo za mme wake anafua house girl,yeye hana kazi ya kumuweka bize mpaka majukum yampasayo kufanya ampe house girl,kazi yake ni kuingia fb,whsp ni addmin wa magroup,halafu kucha amefuga kama jini yeye mwenyewe hajui kujisafisha ukisema umueleweshe anakwambia,babuu eeh ndoa ya masharti hivi mim siwezi bora nirudi zangu hom usije nizeesha buree mtoto wa mwenzio,kwa mfano huo huyo mwanamke utamuweka kundi gan?kwa wew unae tete wanawake wasio jitambua
 
Back
Top Bottom