Nimepata mapacha ila ni pre-mature

Nimepata mapacha ila ni pre-mature

Ramea

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
2,146
Reaction score
4,090
Kuna siku nilikuja na Uzi wa kwanini dokta wa Ultrasound hakutaka kuniambia jinsia za wanangu. Wengi mlitoa comments zenu, nikaridhika nazo.

Kiukweli tarehe ya matazamio ya kujifungua tuliambiwa ni 21 November ila wife kajifungua tangu October 7th. Alipata complications na baada ya kucheck kwa Ultrasound tena na tena, majibu yalionesha mtoto mmoja aligeuka vizuri na mmoja alilala vibaya (kiubavu).

Madokta zaid ya watatu walisema lazima afanyiwe operation ingawa alianza kuonyesha dalili za uchungu wiki ya 33, wakanishauri tusubiri walau hadi iishe wiki ya 34. Ila uchungu ukazidi akajifungua mtoto wa kwanza (yule aliyekaa vizuri) kwa kawaida.

Mungu si Athman maandalizi ya operation ya kumtoa mtoto aliyebakia yalipokamilika akajifungua mtoto wa pili kwa njia ya kawaida. Tulikaa hospitali wiki moja tukaruhusiwa, ila huyu aliyebanwa na mwenzie alikula sindano 16 because alizaliwa dhaifu.

Kwa sasa hivi tunaenda hospitali kwa wiki mara moja kwa ajili ya kupima uzito. Mmoja ashafikisha 2 kg, na mwingine bado ana 1.7 kg. Ingawa wameongezeka hawakuzaliwa na kilo hizo.

Vipi kwa uzoefu na utaalam wenu, nipeni experience kwani hadi sasa hawajapata chanjo hadi watimize 2.5 kg.

Pre mature babies kama hawa hukua vizuri kama wengine ambao walitimiza umri tumboni?

Nifanye nini cha ziada?
 
Mama ale milo kamili yenye kuleta maziwa mazito kama vile supu ya nyama , samaki, vya moto, watoto walishwe kwa wakati bila uvivu watakuwa haraka hao kwa uwezo wa Mungu mtashangaa watakuwa mabonge,

Kikubwa zingatieni miiko mloelezwa na Wakunga na Madaktari
 
Uwe karibu na mkewo msaidiane kulea,

Ukitoka uwe kwenye sababu maalumu mfano kazini lakini ukimaliza kazi tu rudi nyumbani mapema mtiane moyo na kusaidiana!
Sawa, hilo nalizingatia. Usiku wife huwa anachoka na kulala fofofo, wakihitaji kunyonya nasimamia show hata yy bila kujua. Nambanisha chuchu mdomon mama yao akiwa usingizini. Nafanya hivyo had kunakucha.

Kiufupi tangu tumewapata hatulali kwa kutosha, Iwe mchana au usiku, mda wote tunakuwa na usingiz mzito.
 
Naamini muhimu ni mlo tu mzee na kutowatembeza sana mpaka watakapo kuwa stable

Hongera sana mkuu.
Mungu akukuzie.
 
Naamini muhimu ni mlo tu mzee na kutowatembeza sana mpk watakapo kuwa stable

Hongera sana mkuu..
Mungu akukuzie.
Asante sana kwa ushauri.
 
Watakuwa vizuri! Ila hakikisha mama ana pata mlo kamili! Ili atoe maziwa ya kutosha! Una bahati mimi ndugu yangu alikaa mwezi muhimbili!
 
Watakuwa vizuri! Ila hakikisha mama ana pata mlo kamili! Ili atoe maziwa ya kutosha! Una bahati mimi ndugu yangu ali kaa mwezi muhimbili!
Wanangu waliwekwa wiki moja tu chumba maalumu cha pre mature (baby warmer) Tunamshukuru Mungu wanaendelea vizuri kwa kweli.
 
Wataongezeka ila umakini unahitajika sana sana zaidi ya sana. Hakikisha unawavalisha nguo nzito maana baridi kidogo tu linawaletea madhara. Mama ajitaidi kula vyakula bora vinavyozalisha maziwa mengi. Mm nilijifungua pia pre mature wik 33 ingawa dotto alifariki ila kulwa yupo vizuri kilo saba saivi na anamiezi minne. Alizaliwa na 1.9 dotto 1.7
 
Back
Top Bottom