Nimegundua: Wanawake hufa mapenzini

MLALUKO JR

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2015
Posts
962
Reaction score
309
Habarini zenu wanaJF,

Poleni na pilika na mihangaiko ya maisha chini ya utawala wa baba Jesika.

Nilopotea JF for about 6 months.NiliwaMiss sana ndugu.


Straight to the point; mimi ni kijana barobaro, umri 20s. Kuna dada niliweka nia kumuoa kama mambo yakikaa sawa (sijawahi kuwa nae katika mahusiano ya kimapenzi).

Nilijiapiza nisijihusishe nae kimapenzi kabla ya ndoa kwa kuwa sikutaka kuwa nje ya mfumo wetu (kimaadili).

Ila ilitokea hali isiyokuwa ya kawaida, kwani binti alianza kutokujibu txt and samutaimzi tukiongea anaongea kwa 'mkato'.Nilijiuliza bila majibu.

Ila baadae alifanikiwa kuniambia kuwa "tatizo aliwahi kuwa na mwanaume mwingine,ila mwanaume huyo alimtenda (kumwacha) japo sijajua sababu."

So kila akikukumbuka "situesheni" analia na inampelekea kujiaminisha kuwa hakuna mwanaume muaminifu.

Kwa upande wangu imeniathiri na ninahisi taabu kama atakuwa ktk hali hiyo.

chasingi i have noted; ni kuwa wanawake wengi huwa wanazama ktk mapenzi kwa wapenzi wao wa mwanzo(sijajua tatzo).

Nishaurini nimsaidieje ili arudishe imani na wanaume(esp mimi).


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samtaymusi kumsahau alomwacha tena kwenye situesheni kamwachia uchungu moyoni ni shida sana kwa msichana kama asipokubali kama kaachwa na anatakiwa kumove on ... Anatakiwa atambue mapenzi ukiyalea kama mtoto mchanga yatakuumiza sana Kama yuko tayari kupiga hatua msaidie maana asipoangalia mbele ataumia mwenyewe na kuona wanaume ni sio watu wala hawana utu ...
 
Pole dada,ila mm nliweka nia kuoa kabisa kbla hata kujuana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vaa uhusika wake mfano ungekua yeye ungefanyaje ili kujisahaulisha? Kama bado hupati majibu nicheki FB kama unaona uvivu kazana kusoma
 

Mwanaume wa mwanzo anakuwa ana mapenzi ya dhati kwelikweli yaani anasimama na wew nyakati zote ndo maan tukitendwa nao tunaumia vibaya....tofauti na wa pili na watatu ...hawa hawaji kihivyo..kikawaida sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…