Niliyoyaona Utumishi

Niliyoyaona Utumishi

albab

JF-Expert Member
Joined
Jul 6, 2018
Posts
2,000
Reaction score
3,395
Habari wasakatonge,
Kwa kuanza ijulikane kwamba NAMI Ni mtafutaji Kama walivyo watafutaji wote na tusichoke Wala kukata tamaa siku yetu yaja.

Kama mtafutaji nimeomba kazi Utumishi Mara 4 ambapo nimara 1 tu sikuitwa kwenye usaili Ila pia kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu ama dharura nimehudhuria moja tu ya Jana.

NIKICHOKIONA JANA.
1. Napata mashaka Kama Utumishi hua wanapitia maombi yote mpka kuita watu, naongea hili nikiwa najiamini kabisaaa kwamba hawafanyi hivo ila eidha huita watu wote au kukata sehemu tu ya walioomba.

2. Utumishi hawajui Ni watu wa aina gani wanaenda kukutana nao kwenye usaili husika. Kukosa taarifa huku Kuna wapa changamoto kwenye kufanya baadhi ya maamuzi.
Mfano. Kama ulihitaji watu kutoka Walopita JKT je Ni wapi?? Walioko majumbani (Hawa wana vyeti) au walioko makambini (Hawa hawana vyeti na watapewa siku wanarudi nyumbani). je walioko makambini unataka wapi? Kundi senior (OP JK) Hawa wana miaka mnne, kundi la Kati miaka 2 (op JPM), Au kundi dogo kabisaaa (op mirerani) mwaka mmoja.
Utumishi hawapokei testimony kwa wameainisha hilo kwenye tangazo lao kundi kubwa la waliotooa JKT wameitwa na hawana vyeti hili limekaaje??

3. Huwezi kushindana na mitihani ya Utumishi Cha msingi ni kufanya na kufanya Tena Kuna siku utapata. Hawa jamaa wana uwanja Mpana Sana wa kutoa maswali hivyo ukishindwa subiri awamu ijayo.

3. Nimejaribu kuwaza aina ya usahishaji wa hi mitihani walimu watatuelekeza tujifunze pia waza una karatasi 6000 na unatakiwa ndani ya siku mbili uwe umesahihisha na majibu umeyafeed kwenye system na kuyarelease.

4. Baadhi ya Watumishi wa Utumishi dahhh si kwa lugha ile majibu Kama usinifundishe kazi, ntakuharibia maisha, Ni ya kawaida kwao. Nimeyasikia zaidi ya Mara mbili kwa watu wawili tofauti.
5. Vijana wanaonatafuta Ni wengi nimekutana na wadau wengi na nimejifunza mengi kutoka Utumishi Na mitihani yao.
Wasalam.
Albaaaaaaaabbbbbbbbb
 
Wale jamaa huwa hawasomi kabisa applications, yan mtu wameku shortlist wenyew lakin unaenda kwenye interview wanakuambia haukidhi vigezo na kwahiyo hautafanya usail kabisa.
Sasa unajiuliza kama sina sifa kwanini waliniita sasa
Jibi ni kwamba hawako makini na hawasomo application zote
 
Wale jamaa huwa hawasomi kabisa applications, yan mtu wameku shortlist wenyew lakin unaenda kwenye interview wanakuambia haukidhi vigezo na kwahiyo hautafanya usail kabisa.
Sasa unajiuliza kama sina sifa kwanini waliniita sasa
Jibi ni kwamba hawako makini na hawasomo application zote
Jambo lolote likifanywa na mswahili huwa halikosi walakini.uzembe ni mwingi sana kuliko uweledi.
 
Mm nimeapply dijawah kuitwa hata moja. Nmeona nisiapply tena.
 
Mm nimeapply dijawah kuitwa hata moja. Nmeona nisiapply tena.
Hakuna ishu huko maana hata ukiitwa unaweza kuja tena jukwaani lalamika mumeitwa watu 2000 ila post 1 tukushauri uende au usiende.
 
Mbona private hata wabongo wanajitahidi kidogo
Yes private wanajitahidi especially kwenye kampuni zinazomilikiwa na wazungu.
Ila kwenye kampuni za wabongo na wahindi nako ni kichefu chefu tu.
Unakuta mtu unaitwa interview saa 2 asubuh halaf unasubiria hadi saa 8 mchana interview bado haijaanza.
 
Back
Top Bottom