Mkuu kwa leo Mbezi Mwisho hadi Posta ukiwa na private car unatumia dakika 30 hadi 40 wakati siku nyingine huwa ni dakika 90 hivi.
Ni kweli sababu ni hiyo ya kutokuwepo kwa malori yanayoingia jijini, kwa kawaida kuanzia alfajiri ya saa 11 msururu wa malori huwa unaanza kujilimbikiza pale Kimara Mwisho na kadiri muda unavyojongea foleni nayo hukua taratibu na baadaye huamia Ubungo.