Nikalie wapi TRA

Nikalie wapi TRA

Mfikilwa

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2008
Posts
412
Reaction score
123
naandika hapa nikiwa na hakika kuna mtu yoyote wa tra ambaye anaweza nisaidia, nina lori nataka kulitowa bandarini, kwanza nimelog na vielelezo vyote, ni wapi nimenunua na risiti za malipo ya benki za kuonyesha ni kihasi gani nimetuma, lakini tra wao waka uplift bei wanayotaka wao, nikasema sawa nikubali nilipe kubishana mpaka mpaka wakikujibu itachukua muda, matokeo yake wamenijibu kimakosa, kwenye import duty wameweka asilimia 25 badala ya 10 kwa malori, sasa makosa ni yao leo ni siku ya tatu hawajarekebisha, kila agent wangu akienda wanamwambia tunalifanyia kazi tutawajibu, sasa jamani ni siku ya tatu gari yangu ina cbm 105 na cbm 1 wanacharge dola 1, means kwa siku ni dola 105 toka walivyojibu wakakosea mpaka nitakapokuja kulitoa huo mzigo wa storage anaubeba nani?

Kisha niiomba serikali yangu, hili swala la kuruhusu maagent tu watutolee mizigo waliangalie upya, tunaumia sana wenye mizigo, maagent ndiyo wanaoruhusiwa kuingia sehemu zote zinazohusika na mzigo wangu, asilimia kubwa ya maagent ni waooooooongo mno, kwanini serikali isiruhusu mtu ukalogin mwenyewe mzigo, si unakuwa na TIN namba.

nchi za wenzetu kusafirisha mzigo ama kutoa mzigo bandarini ni kitendo cha siku moja tu, unaenda na document zinazoonyesha mzigo ni wako na vitambulisho vyako vya utambuzi, unatajiwa malipo, unalipa, kazi imekwisha, kwetu kwanza ulogin document, zinapita siku mpaka wakujibu, na kuuplift ni lazima, uanze kugombana nao kwanza, siku nazo zinapita, wanakujibu tena, ukubari, uende bank ukalipe, system yao ionyeshe kama malipo yameingia siku moja nayo imeenda, document zishuke bondeni nako uanze kubembeleza kupewa release, ukipata ulogin tena hili upate hesabu za bandari, jamani mtafute njia za kufanya kazi kwa ufanisi hivi ilivyo sivyo kabisa. wahusika ni vizuri wakaangalia upya utaratibu wa utoaji mizigo bandarini
 
Mfikilwa,

Haya ndo maajabu ya utendajikazi kwenye taasisi zetu nyingi hapa Tanzania, mambo mengi yanafanyika "in doublestandards" inategemea wewe ni nani na au pengine wajuana na nani, infact wanyonge wanaumizwa!!!

Juzi, kwenye kipindi Cha asubuhi cha "Amka na BBC" nilisikitika kuwasikia WANYARWANDA na WARUNDI wakiilalamika Bandari ya Dar-es Salaam, kwa Ubabaishaji wake hasa kwenye uondoaji wa magari pale Bandarini. Hivi kweli Mamlaka husika za juu hazilioni hili? na kama hawayaoni haya je, hata kusikia hawasikii?

Hivi tutangoja kila jambo aje Dr. Harrison Mwakyembe, akemee kwanza ndipo watendaji waamke?

Ndugu yangu Mfikilwa siku nyingine pitishia gari BANDARI ya MOMBASA. Potelea mbali Liwalo na Liwe!!!
 
Pale long room kuna kitu kinaitwa customer service manger zuka na doc zako, usimsikilize clearing agent atakjwa na vimeo vyake anashindwa kuingia kwa meneja

Na tra hawakosea wanaokosea ni hao ma clearing agent uchwara. I hate those guys more than TRA
 
mkuu document gani ambayo natakiwa niingie nayo kwa meneja? yule askari wa mlangoni jana alinizuia kuingia, nilipata hasira ya ajabu, nikaenda kulala, wanauzi sana, sasa mkuu una namba ya huyo manager nimpigie kwanza, kwakweli tunaumia sana, utaratibu wa kucharge ushuru nao wangebadilisha, ingekuwa kabla awajacharge ushuru wanaend akuuona mzigo physical, maana juu wanacharge, ukishuka chini kwenye release ambaye ndiye mkaguzi anauwezo wa kuuplift ushuru uliolipa na getini nako kuna mtu ana uwezo wa kuukataa ushuru uliolipa, watu 3 wanafanya shughuli moja, kwanini unapoligin document kabdla awajatoza ushuri wakague mzigo na kila kitu, unapoenda chini unaenda kulipia gharama za bandari tu na kutoa mzigo wako, serikali ijipange upya BANDARINI

Pale long room kuna kitu kinaitwa customer service manger zuka na doc zako, usimsikilize clearing agent atakjwa na vimeo vyake anashindwa kuingia kwa meneja

Na tra hawakosea wanaokosea ni hao ma clearing agent uchwara. I hate those guys more than TRA
 
for any enquiry or complain please dial TRA Call center no. 0800110016 for vodacom and TTCL


OR

0786800000 FOR AIRTEL.

SIMU HIZI NI BUREE.
 
asante mkuu

for any enquiry or complain please dial TRA Call center no. 0800110016 for vodacom and TTCL


OR

0786800000 FOR AIRTEL.

SIMU HIZI NI BUREE.
 
Baba hiyo uplift ndio style yao na nasikia huwa ile document ya pili huwa wanaitoa ya kwanza kwenye system na ile yenye value ndogo ndio wanayoitoa ya mwisho. Kisha ile doc wanayokubwa ni iliyokuwa uplifted wakt kwenye system wanajidai wamedown grade. Hii ile tofauti wanakula wao inauma sana aisee.
 
nimechoka jamani nahitaji msaada kweli kweli, nahitaji msaada, hapa sijaribu kukwepa kodi, nataka nilipe kodi iliyosahihi, kwanza bank tt yangu wameikataa, wametia bei wanayotaka wao, nimekubali, sasa Scania si linajulikana kwamba ni lori? na malori import duty yake ni 10% na VAT 18% ndiyo ninayotakiwa kulipa mimi, sasa mmeniwekea import duty 25% hii si sahihi na wenyewe wanajuwa kwamba si sahihi, eti uzito ulioandikwa kwenye b/l ni mdogo, hivi ushuru huwa unachajiwa kutokana na uzito? i am serious naombeni msaada, hii sitaikubali kabisa, hata mimi mwenyewe natafuta riziki pia sasa wanicharge kisahii, hizo namba nimejaribu wapi hakuna anayepokea, naombeni namba za Mwakyembe hii si haki kabisa.
 
Fanya kazi na kampuni za logistics za kueleweka wakufanyie clearance kama kuhne + nagel, sdv transami, dhl, panalpina etc achana na kampuni njaa hizo,, cheap is expensive kaka
 
Back
Top Bottom