Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,198
- 162,742
Uchaguzi mkuu wa mwaka huu, endapo utafanyika, hautaicha Tanzania ikiwa salama na mwaka huu ndio Tanzania itajulikana zaidi kimataifa(ita-make the headlines).
Kumbuka,nchi za kiafrika hutangazwa sana duniani na vyombo vya habari vya kimataifa si kwa mazuri,bali tu pale panapokuwa na machafuko au ghasia za kisiasa na magonjwa kama vile Ebola n.k.Tanzania mwaka huu sidhani kama tutalikwepa hili.
Mwaka huu kuna kila dalili na kila sababu ya wapinzani(UKAWA) kususia au kupinga matokeo ya uchaguzi huu na hivyo kusababisha sintofahamu kubwa katika nchi hii.Sababu hizo ni kama ifuatavyo;
Mosi,zoezi la kuandikisha wapiga kura linafanyika katika mazingira yasiyo rafiki kwa wapiga kura na hali hii huenda ikasababisha wananchi wengi wakashindwa kujiandikisha na baadae kuzua malalamiko na hivyo kuufanya uchaguzi ujao usiwe huru na wa haki.
Kwa mfano,jana kupitia ITV,nilishuhudia wananchi wakilalamikia zoezi la uandikishaji huko Iringa kwamba linachukua muda mrefu na kuwafanya wengine wafike kwenye vituo saa 8 za usiku ili kuwahi kuandikishwa na dada mmoja alifika mbali zaidi kwa kusema zoezi hilo linahatarisha ndoa zao kwani hutumia muda mwingi kukaa vituoni kuanzia saa 12 za asubuhi.
Mbali na wananchi, hata viongozi wa vyama vya siasa nao wameulalamikia mfumo huu mpya wa uandikisha wapiga kura unaojulikana kama BVR bila kusikilizwa licha ya ushauri mzuri wanaoutoa kwa viongozi wa nchi hii.
Pili, vijana wengi hawataipigia kura CCM na hivyo kuifanya CCM kushindwa vibaya na ni vijana hao hao ndio baadhi yao watakosa fursa ya kujiandikisha kutoka na mfumo huu wa BVR na wengi wao hawatakubali kupoteza haki hiyo.
Tatu,kashifa za Escrow,unyama wa polisi,maslahi duni ya wafanyakazi na hasira ya wafanyabiashara kwa serikali zitakipunguzi CCM kura nyingi na kuongeza uwezekano wa CCM kushindwa.
Nne,muungano wa UKAWA safari hii utawafanya wapinzani wawe wenye nguvu zaidi katika kudai haki yao na pia unaweza ukawafanya wakatae hata ku-compromise kwani teyari wana umoja na isitoshe mawazo na maoni yao mengi yamepuuzwa na watawala kiasi cha kutosha.
Kitakachotokea ni CCM kujaribu kuchakachua matokeo na kulazimisha ushindi na hapa UKAWA hawatakubali na ndio itakuwa mwanzo wa vurugu na machafuko nchi nzima.
Katika majimbo mengi,wabunge wa chama tawala watashindwa ila tume haitatoa matokeo kwa wakati na wananchi kwa kushirikiana na wabunge walioshinda hawatavumilia na machafuko yatatokea sehemu nyingi za nchi kwa wakati mmoja na polisi watashindwa kutuliza hizo ghasia na itakuwa ni fujo kila mahali(kwenye kila jimbo).
Matokeo ya uraisi yatakayotangazwa na tume,wapinzani hawatayakubali(kumbuka walitaka tume huru) na hivyo kuongeza hasira za wananchi na za viongozi wa upinzani.
Matokeo ya ujumla ya haya yote itakuwa ni fujo,ghasia na wapinzani kuhamasisha maandamo ya nchi nzima kupinga matokeo ya uchaguzi huo na kutaka uchaguzi urudiwe na safari hii usimamiwe na tume huru.
Viongozi wengi wa upinzani ikiwemo wagombea ubunge watakamatwa,watapigwa na kutiwa ndani kwa kitakachoitwa kuchochea vurugu na hapo ndipo vyombo vya habari vya kimataifa vitakapoimulika Tanzania na zaidi pale watu watakapopigwa, kujeruhiwa na hata kuuwawa katika ghasia hizo.
Wafuasi wengi wa upinzani na hasa vijana, hawatavumilia kuona Mbowe,Dr.Slaa,Mbatia na Lipumba wakipigwa virungu na polisi au kuona wabunge na madiwani waliowachagua wakikamatwa bila sababu za msingi.
Watawala,muda wa kufanya marekebisho na kuepusha balaa hili bado upo, ila kama mnataka kulazimisha ushindi,basi mjiandae kuhudhuria mahakama za kimataifa kama wenzenu wa Kenya.
Amani na utulivu wa nchii baada ya uchaguzi wa Oktoba iko mikononi mwa viongozi wa UKAWA na kamwe si polisi wala watawala.
Kumbuka,nchi za kiafrika hutangazwa sana duniani na vyombo vya habari vya kimataifa si kwa mazuri,bali tu pale panapokuwa na machafuko au ghasia za kisiasa na magonjwa kama vile Ebola n.k.Tanzania mwaka huu sidhani kama tutalikwepa hili.
Mwaka huu kuna kila dalili na kila sababu ya wapinzani(UKAWA) kususia au kupinga matokeo ya uchaguzi huu na hivyo kusababisha sintofahamu kubwa katika nchi hii.Sababu hizo ni kama ifuatavyo;
Mosi,zoezi la kuandikisha wapiga kura linafanyika katika mazingira yasiyo rafiki kwa wapiga kura na hali hii huenda ikasababisha wananchi wengi wakashindwa kujiandikisha na baadae kuzua malalamiko na hivyo kuufanya uchaguzi ujao usiwe huru na wa haki.
Kwa mfano,jana kupitia ITV,nilishuhudia wananchi wakilalamikia zoezi la uandikishaji huko Iringa kwamba linachukua muda mrefu na kuwafanya wengine wafike kwenye vituo saa 8 za usiku ili kuwahi kuandikishwa na dada mmoja alifika mbali zaidi kwa kusema zoezi hilo linahatarisha ndoa zao kwani hutumia muda mwingi kukaa vituoni kuanzia saa 12 za asubuhi.
Mbali na wananchi, hata viongozi wa vyama vya siasa nao wameulalamikia mfumo huu mpya wa uandikisha wapiga kura unaojulikana kama BVR bila kusikilizwa licha ya ushauri mzuri wanaoutoa kwa viongozi wa nchi hii.
Pili, vijana wengi hawataipigia kura CCM na hivyo kuifanya CCM kushindwa vibaya na ni vijana hao hao ndio baadhi yao watakosa fursa ya kujiandikisha kutoka na mfumo huu wa BVR na wengi wao hawatakubali kupoteza haki hiyo.
Tatu,kashifa za Escrow,unyama wa polisi,maslahi duni ya wafanyakazi na hasira ya wafanyabiashara kwa serikali zitakipunguzi CCM kura nyingi na kuongeza uwezekano wa CCM kushindwa.
Nne,muungano wa UKAWA safari hii utawafanya wapinzani wawe wenye nguvu zaidi katika kudai haki yao na pia unaweza ukawafanya wakatae hata ku-compromise kwani teyari wana umoja na isitoshe mawazo na maoni yao mengi yamepuuzwa na watawala kiasi cha kutosha.
Kitakachotokea ni CCM kujaribu kuchakachua matokeo na kulazimisha ushindi na hapa UKAWA hawatakubali na ndio itakuwa mwanzo wa vurugu na machafuko nchi nzima.
Katika majimbo mengi,wabunge wa chama tawala watashindwa ila tume haitatoa matokeo kwa wakati na wananchi kwa kushirikiana na wabunge walioshinda hawatavumilia na machafuko yatatokea sehemu nyingi za nchi kwa wakati mmoja na polisi watashindwa kutuliza hizo ghasia na itakuwa ni fujo kila mahali(kwenye kila jimbo).
Matokeo ya uraisi yatakayotangazwa na tume,wapinzani hawatayakubali(kumbuka walitaka tume huru) na hivyo kuongeza hasira za wananchi na za viongozi wa upinzani.
Matokeo ya ujumla ya haya yote itakuwa ni fujo,ghasia na wapinzani kuhamasisha maandamo ya nchi nzima kupinga matokeo ya uchaguzi huo na kutaka uchaguzi urudiwe na safari hii usimamiwe na tume huru.
Viongozi wengi wa upinzani ikiwemo wagombea ubunge watakamatwa,watapigwa na kutiwa ndani kwa kitakachoitwa kuchochea vurugu na hapo ndipo vyombo vya habari vya kimataifa vitakapoimulika Tanzania na zaidi pale watu watakapopigwa, kujeruhiwa na hata kuuwawa katika ghasia hizo.
Wafuasi wengi wa upinzani na hasa vijana, hawatavumilia kuona Mbowe,Dr.Slaa,Mbatia na Lipumba wakipigwa virungu na polisi au kuona wabunge na madiwani waliowachagua wakikamatwa bila sababu za msingi.
Watawala,muda wa kufanya marekebisho na kuepusha balaa hili bado upo, ila kama mnataka kulazimisha ushindi,basi mjiandae kuhudhuria mahakama za kimataifa kama wenzenu wa Kenya.
Amani na utulivu wa nchii baada ya uchaguzi wa Oktoba iko mikononi mwa viongozi wa UKAWA na kamwe si polisi wala watawala.