Ni upuuzi mkubwa kufikiria Nape na watu fulani kuhama CCM

Kaka sijui umefikiria kupitia nn wanaohama ACT kwenda ccm au Chadema kwenda CCM njaa mbaya sana na huko ni kubadilisha nini?? Yan mifano ni wanawake tu
 
Sina cha kuongeza wala kupunguza katika uzi wako huu, kuwa mpinzani wa kweli inabidi uwe umekubari kuwa tayari kwa lolote hasa kifo na umaskini, hata hapo CHADEMA wapinzani wakweli ni wachache sana wengi wapo nyuma ya migongo ya kina lisu.

Mimi ni CHADEMA hasa kwakuwa nawachukia sana CCM lakini namshauri tu Nape na Bashe wafunge tu midomo, sisi tunao jitambua tunajua fika hawawezi kutoka CCM wenyewe bila kufukuzwa na kwakuwa siku wakifukuzwa watakufa njaa mapambano ya kweli wawaachie CHADEMA maana wengi hakuwahi kuota kama watakujakuwa wabunge, ubunge kwao ni zari tu hivyo maranyingi wapo tayari kuishi kama mbwa mitaani lakini si kupiga magoti kwa CCM.
 
Nape angekuwa ameshajijenga kimaisha angeweza kuondoka ccm. Lakini kwakuwa ni masikini na hana ujanja nje ya siasa hawezi kuhama. Ila ataendelea kubaki ccm hata kama kwa sasa imemtumbukia nyongo. Sio mbaya acha tu ccm imrushe roho maana hata yeye ni wale wanaounga mkono upuuzi wowote unaoletwa na ccm kama kufunga bunge live.
 

Ninachokiona kwako hujui michezo ya siasa za bongo mkuu na si bongo ata nchi zingine pia
Nape asiame yeye ni nani kwenye CCM
Usiangaike na maneno wanayotumia Leo kuwa sihami na sitohama hizi ni siasa tu
Walikuwepo akina kingunge walidumu tangu TAA na TANU hakuna MTU ambaye alihamini atakikimbia chama na alipokuwa akiulizwa alikuwa anakataa siwezi hama na sijawahi fikiria

Lowasa Naye vivyo hivyo alisema sitohama CCM anayefikiria Mimi ntahama basi atahama yeye lakini mwisho wa siku akaondoka zake.
Na wengine wengi walikuwa hivyo

Ebu jaribu kusoma siasa za bongo
Acha kuzungumzia nafsi za watu mkuu
Huyo unayemsema NAPE kuna kitu anawaza kichwani mwake

Anachokifanya NAPE kwa sasa anajenga mtaji wa uko mbeleni yaani mashabiki
Kama unamfuatilia ameanza kuwa mpinzani ndani ya chama ili kuteka watu wawe na imani Naye kuwa ni jasiri

Ili mwishowe akitoka hapo awe na mtaji mzuri
Ukija kwa Nyalandu naye mwishoni uku alianza kuwa mpinzani ndani ya chama ili kuteka watu akawa anafanya vitu ambayo chama chake akitaki kwa mfano kumtembelea lissu Hospitalini uko Nairobi

Wakati chama kilizuia wabunge wa CCM wasiende kumuona
Na mengine mengi akawa anayafanya ili kuteka watu
Mtaji wa mwanasiasa ni watu kwa maana mashabiki ambao ni wapiga kura pia
Mfuatilie vizuri NAPE kuna kitu anakitafuta na kujiandalia,anangalia upepo jinsi unavyoenda kuelekea uchaguzi 2020

Unajua jinsi anavyoenenda NAPE kupingana na serikali ya chama chake kwa sasa ni dhairi CCM hawatampa ridhaa ya kugombea ubunge kupitia hicho chama 2020 kwa jinsi ninavyoifahamu roho ya mwenyekiti wa chama hicho ilivyo,sasa Nape hilo analijua na anajipanga kufanya kitu hapo mbeleni wewe subiri utaona na kusikia tu mkuu
Fuatilia sana siasa za bongo zinavyokwenda

Afu usiwe na mawazo hasi eti kuwa MTU Fulani hawezi kuendesha maisha au kuishi bila kuwa CCM,ukiwa na mawazo hayo ni ulemavu wa akili mkuu na uoga pia
Mzee kingunge ata kwenye kula kiapo alikuwa anatumia katiba ya chama cha mapinduzi badala ya biblia mpaka watu wakawa wanasema mzee hana dini,wakidai anaabudu CCM lakini Leo hayupo CCM,ulikuwa umwambii kitu kuhusu CCM yule mzee

Achana na mambo ya siasa huyajui utaumiza akili tu
Fanya mambo yanayokuingizia kipato tu

Siasa waachie wenyewe.
Unajua siasa ni kama upepo tu Leo unavuma kwenda uku kesho unaelekea kule.
 
Nape anastahili kuhama ssm, ila sasa anahamia wapi kwa mbowe au kwa lipumba au zitto ama mbatia bora abaki huko..!
 
Hufahama siasa ikiwa unazungumzia wanasiasa wanachosema.mimi nakwambia kitu kwa kuangalia behind their words. Kuangalia wanachofanya.lowassa nlijua tu kuwa atahama sababu ya kilichokuwa nyuma yake zaidi ya ulichokuwa unasikia. Ungekuwa umesoma psychology huwez mfananisha lowassa na nape.ni watu wenye personality tofauti kabisa.

Nje ya siasa lowassa ni mfanya biashara, ni mwanahisa wa makampun kadhaa.ana mambo mengi haishi kwa siasa. Ni smart na hata kuhamia cdm alifanya check and balance akaangalia positive side na negative side yake akajipima akajua ata survive. Usidhan aliamka tu akasema anahamia cdm.

Nape alishapima na kama hajapima bas namshauri asihamie cdm. He wont survive...nje ya siasa nape ni hopeless.na nape hajawah kuwa smart trust me. Atakuwa smart sasa ikiwa hata hama ccm. Akihama ndo ata prove kuwa he isnt smart. Hakuna jimbo ambalo nape anaweza kugombea kama mwana chadema akashinda hapa tanzania hata udiwani.hamna.

So haya mambo tuachie sisi wanasiasa tunafaham nape mule ccm ni kama samaki anavyohitaj maji. Nape anahotaj sana ccm kuliko ccm inavyomhitaj nape.

So kwa sisi wanasiasa wakongwe wenye akili huwa hatuangalii maneno ya wanasiasa.tunaangia matendo au uhalisia wao. Nape akiingia cdm ni hatar sana kwake.

 
jiwe la maji wengi hawaelew haya... Wanafikiri ni rahisi tu.si rahisi kiasi hicho. Kuwa mpinzan ni kukubal umaskin na hata kifo.labda uwe mpinzani mpiga deal tu kama watu flan. Si rahisi kama makamanda wanavyofikiri kwa nchi zetu za kiafrika hasa tanzania

 
Kwahiyo Nape sio mwanaume? By the way source nini mkuu?
 
Nikweli kabisa, alafu makamanda wenzangu wanakuwa kama vile hawajui hari harisi ilivyo.

Mpinzani hapa kushinda ubunge au udiwani inategemea na mahitaji ya CCM ya jimbo au kata husika na si tu wingi wa wapiga kura wa CHADEMA.

Hebu fikiria uchaguzi unafanyika alafu majumuisho ya kura zote kule vituoni yanakuwa yanaonyesha furani ndio mshindi lakini wakifika kule halmashauri yule mshindwa analazimisha kura zihesabiwe upya kutoka kwenye masanduku ya kura, hapo wanakuwa wameshaongeza kura zilizopungua na kuzidisha kidogo. Mgombea unaedhurumiwa ukikubali umeliwa ukisusa wenzie wanaendelea na zoezi alafu wanajitangaza washindi.
Muda huo ni sasa nane za usiku alafu makamanda wote wanakuwa wamezuiliwa kusogea karibu na eneo la tukio na wanakuwa wafukuziwa majumbani na magenge ya watu yanakuwa yamepigwa marufuku.

Njia zote zikishindikana mtangaza matokeo anaambiwa amtangaze aliyeshindwa ndio kashinda alafu aliyedhulumiwa anaambiwa ikiwa hajaridhika aende mahakamani.

Aise Nape aangalie asije laza watoto njaa.
 
bavicha wanambinu mbaya sana ya kutisha wana ccm kwa kuwapa kashafa feki ili wahamie kwao halafu wakishahamia wanasema ni wasafi hawana mawaa
 
Wewe mzee umekura maharage ya wapi? sikia

Anaweza hama kwa faida ya ccm, na akalipwa na ccm huyohuyo.tena akafanya vizuri kwa mtaji wa ccm. ogopa sana wanasiasa wanao jifanya hawaelewani na uongozi wa chama tawala usiwafuate. mi vyama mingine inapokea pokea tu.

wanachama watakao kuwa hawajitambui kama Gudume ndo watatangulizwa mbele ya maandamano kama sadaka ya kuzindika chama wewe unajua but unatujaribu!

wengine mko humu ku-test zari za wabongo.
 

Bado msimamo wetu ni uleule.
 
Not sentenced to death....but it is life imprisonment Sir.
 
Mnanikumbusha siasa za Tanzania rejea aliye tangaza kustaafu siasa akiwa mwenyekiti wa chama fulani baadae akaibuka kuutataka tena uwenyekiti wa chama hicho hicho hadi kulala kwenye ofisi ya chama kumbe siasa inalipa sana
 
Nape wakati anaanzisha ccj ,wewe ulikuwa wapi ? Bila Kikwete ,Nape asingerudi ccm. Unachozungumzia wewe ni yoga wa kisiasa kutochikua maamuzi magumu ,hiyo unategemea MTU na mtu , Jiwe mwenyewe anataka kuanzisha chama chake .Atoke chama cha wapumbavu .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…