Ni raia gani akiumwa anakimbizwa nje? Kwanini mapacha wetu hatukuwapeleka India kwa matibabu?

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,013
8,369
Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema, binafsi ninatambua kuwa sisi binadamu wote ni sawa na mazao tuliopandwa duniani na muda wowote ukiamua kutuvuna unatuvuna tyuuu majira yoyote.Nina tambua wanadamu kabla ya kifo chetu huwa tunaangaika sana kupingana na wewe Mola wetu usituvune.

Mungu wetu juma lililopita umewavuna mapacha walioungana hakika mimi niamini wewe umeamua kutenda lile wanadamu hatuwezi kulipinga wala hatuna nguvu hiyo! Sambamba, hayo yote nilitaka kujua Serikali yetu imepigania uhai wa watoto wetu vya kutosha?

Waliumwa mara ya kwanza wakalazwa huko kwao Iringa baadae wakaletwa Muhimbili wakapata nafuu, wakarudi huko kwao Iringa wanakaumwa tena na kurudishwa hapo hapo Iringa! Mpaka mauti yalipowakuta.

Sasa swali moja tu Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipigania roho za watoto wetu vya kutosha?

Je kama walikuwa na tatizo la moyo kwanini hatukuwapeleka India ili wakatibiwe tatizo lipone kabisa?

Sawa wamekufa ila lazima tujiulize mchango wa Serikali kwa watoto hawa mpaka wanaaga Dunia katika hali za maumbile waliyokuwa nayo.

Pumzikeni kwa amani Consolata na Maria!
 
hata mimi imenisikitisha bahati nzuri nawajua ndugu zao kwa karibu kuna kipindi walitangaza kuwa wanapelekwa Afrika kusini lakini nilipowaulizia wakasema hakuna kitu hicho na hata waliporudishwa Iringa siyo kwamba hali yao ilikuwa imeimarika labda wangekuwa wasanii wangepewa uzito mkubwa Mungu awarehemu huko waliko
 
am sorry to ask, walikufa wote kwa pamoja au mmoja mmoja? na je walikuwa wanatumia moyo mmoja au kila mtu na wake? tatizo lao hasa lilikuwa nini maana sikuwa mfatiliaji sana wa mambo yao, RIP
 
Unatoka hospital na kurudishwa nyumani kwa ambulance then unaambiwa afya yako imeimalika jamanii tumuogope Mungu... Tuliwapenda sana dada zetu na wanafunzi wenzetu mbele yenu nyuma yetu
 
Unatoka hospital na kurudishwa nyumani kwa ambulance then unaambiwa afya yako imeimalika jamanii tumuogope Mungu... Tuliwapenda sana dada zetu na wanafunzi wenzetu mbele yenu nyuma yetu

Nimejikuta nacheka kwa Saudi
 
Waliishia kutembelewa MMCH na viongozi kuanzia ngazi ya juuuuu huku bashite akiwa busy kumpeleka India yule mwarabu mpemba sijui mhindi na mkubwa kumsaidia wastara kwenda kujirusha India Sweden sijui Denmark na pesa ya walipa kodi.
 
Nazan kilichotokea wala sio cha kuilaum serikali.
Waliwajibika kwa kiwango gani? Hilo ndilo swali kaka. Kufa si issue hata wengine wanafia nje ila huwezi kumwacha mtu wako afe kwasababu kufa kupo. Swali ni je mbona hawakupelekwa india au marekani au hata cuba au wewe ulikuwa hujui wale wadogo zetu walikuwa wanahitaji special treatment and care?
 
Waliwajibika kwa kiwango gani? Hilo ndilo swali kaka. Kufa si issue hata wengine wanafia nje ila huwezi kumwacha mtu wako afe kwasababu kufa kupo. Swali ni je mbona hawakupelekwa india au marekani au hata cuba au wewe ulikuwa hujui wale wadogo zetu walikuwa wanahitaji special treatment and care?
mkuu ni special treatment gani waliokuwa wakiihitaji na ikakosekana?
 
Mawazo yangu: Sasa hivi hospitali zetu zinakomalia kutokusalimu amri kuwa wameshindwa kutokana vitisho. Wanaogopa kupoteza kazi. Hasa ukizingatia mgonjwa mwenyewe anatoka kundi la "malofa" hupelekwi nje hata iweje.
 
Waliwajibika kwa kiwango gani? Hilo ndilo swali kaka. Kufa si issue hata wengine wanafia nje ila huwezi kumwacha mtu wako afe kwasababu kufa kupo. Swali ni je mbona hawakupelekwa india au marekani au hata cuba au wewe ulikuwa hujui wale wadogo zetu walikuwa wanahitaji special treatment and care?
rais alienda hadi kuwatembelea pale muhimbili kuwapa moyo kama suala lao lingehitaji kwenda kutibiwa nje ya nchi nadhan pale ndo ilikuwa chansi..kumbuka ripoti ya madaktari ndo huwa inafanya mgonjwa ahamishwe kutoka hospital moja kwenda nyingne. Who knows kama ugonjwa wao haukushindikana kutibiwa hapa nchini. Na ndo mana wakaruhusiwa baada ya hali kutengemaa..kilichotokea ni matokeo tu ingekuwa was kupelekwa nje mbona serikali hii kwa sifa wangekuwa wameshapelekwa mda tu...amepelekwa mzee majuto mwenye tezi dume, Hawa wa moyo isingeshindikana.
 
Waacheni wale watoto wapumzike jamani...binadamu tunampenda sana Mungu lakini hatupendi kukutana nae..wale watoto wameteseka saana waache wakakutane na Mungu awavishe taji kwa uvumilivu, Upendo, na kumuheshimu mungu kwa uumbaji wake regardless walichokuwa wanapitia.

The same as you appreciate life..you should appreciate death too.

Kwani huko nje wanatoa viungo vya moyo na roho? Mbona wanaoenda nje wanarudishwa kwenye sehemu ya mizigo ya ndege?
 
Wangepelekwa nje wasingekufa???
Viumbe wazito sana ninyi...
Ndugu majirani wafa mitaani huko tena wengine mkiwashuhudia na mnawapotezea ila hawa lawama kwa serikali
 
Mbona walikuwa wanalelewa na Consolata missionaries huko Iringa? Ni mipango ya Muumba tu kwani hawakushindwa kuwapeleka nje kwa matibabu. May the Almighty God rest their souls in internal peace Amen
 
Back
Top Bottom