Habari za majukumu ndugu zangu. Ni matumaini yangu mko bukheri kabisa.
Kama kichwa kinavojieleza nimekua nikisumbuliwa na hili tatizo nadhani ni tangu nilipojitambua.
Kuna kipindi nikitaka kukimbia au kufanya kazi itayosababisha matumizi ya nguvu na hatimaye kutokwa jasho mwili wangu huanza kuwasha. Muwasho wa kutosha tu.
Lakini vile vile nikioga na kujisugua hali huwa si nzuri kwani mwili wangu huwasha kwa muda. Hii ni mbaya kwani nikijisugua zaidi na mwili huwasha zaidi.
Ningeomba msaada kwa mtu yeyote mwenye uzoefu na hata ufumbuzi wa tatizo hili.
Kama kichwa kinavojieleza nimekua nikisumbuliwa na hili tatizo nadhani ni tangu nilipojitambua.
Kuna kipindi nikitaka kukimbia au kufanya kazi itayosababisha matumizi ya nguvu na hatimaye kutokwa jasho mwili wangu huanza kuwasha. Muwasho wa kutosha tu.
Lakini vile vile nikioga na kujisugua hali huwa si nzuri kwani mwili wangu huwasha kwa muda. Hii ni mbaya kwani nikijisugua zaidi na mwili huwasha zaidi.
Ningeomba msaada kwa mtu yeyote mwenye uzoefu na hata ufumbuzi wa tatizo hili.