Neymar atajwa kuwa mwanasoka ghali duniani

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Neymar-750x375.jpg

Staa wa soka anayekipiga wa Barcelona, Neymar ametajwa kuwa mchezaji ni ghali zaidi duniani akiwapita mastaa wengine ambao wanatajwa kuwa wakubwa zaidi yake akiwepo mchezaji mwenzake wa Barcelona, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ambaye hivi karibuni ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia 2016.

Jambo hilo la Neymar kuwa mchezaji ghali duniani limejulikana kupitia utafiti ambao umefanywa na kampuni ya tafiti za soka ya CIES Football Observatory ambayo imesema kwasasa Neymar ana thamani ya Euro milioni 246.8.

Katika utafiti huo, Lionel Messi ameshika nafasi ya pili akiwa na thamani ya Euro milioni 170.5 na Paul Pogba akishika nafasi ya tatu kwa kuwa na thamani ya Euro milioni 155.3 huku Cristiano Ronaldo akiwa katika nafasi ya saba kwa kuwa na thamani ya Euro Milioni 126.

Aidha CIES walisema vigezo walivyotumia kuchagua wachezaji hao ni uwezo wa mchezaji uwanjani, msaada anaotoa kwa timu yake, magoli anayofunga na dakika anzocheza pia kuangalia umri na mkataba alionao katika klabu anayoichezea.

Chanzo: Mo Dewj Blog
 
pesa za sasa kwenye ulimwengu wa soka hazi reflect ubora wa mchezaji. sasa uwezo wa Neymar na Ughali wake wote atamfikia Sanchez?
 
pesa za sasa kwenye ulimwengu wa soka hazi reflect ubora wa mchezaji. sasa uwezo wa Neymar na Ughali wake wote atamfikia Sanchez?

Umri ndiyo unamfanya awe hivyo lakini uwanjani wa kawaida sana...angalia kacheza game ngapi bila goli.

Tathmini zingine za kijinga kabisa messi anaeibeba tim almost kwa 80% halafu thamani yake 170.5 alaf hiki kitoto kinaomtegemea mwalimu wake/messi na bado hakifanyi vizuri eti thamani yake 246.8,yani na wengine pia kawazidi eti mbali!!... wamechemsha aise..
 
Mkuu! siongopi .....

hebu fikiria kwenye ulimwengu wa ambao Messi na Ronaldo hawapo......huyu dogo atawashindaje wakina Suarez,Griezman, nk

Ha ha haaaa mukuu ndio hapo sasa..i agree with your assessment 100%, upo sahihi kabisa! huyu dogo alishakili kabisa pale barca haondoki akamwacha pacha wake messi,messi ndie kamfanya asiondoke pale..Uzuri wa messi bana sio mbinafsi anampa shule dogo sema tu kichwa chake labda kitakua kigumu kuelewa..we angalia hata asipopata goli,penalt ikapatikana ataachiwa na messi kupiga angalau na yeye apate kuliko kukosa kabisa. Messi anawalinda sana vijana pale basi tu...alaf eti thamani yake kubwa yani nimecheka mpaka basii..
 
Umri ndiyo unamfanya awe hivyo lakini uwanjani wa kawaida sana...angalia kacheza game ngapi bila goli.

Tathmini zingine za kijinga kabisa messi anaeibeba tim almost kwa 80% halafu thamani yake 170.5 alaf hiki kitoto kinaomtegemea mwalimu wake/messi na bado hakifanyi vizuri eti thamani yake 246.8,yani na wengine pia kawazidi eti mbali!!... wamechemsha aise..
Wewe kichwa yako imejaa messi tuu...Yaani akitajwa mwingine lazima upinge kwa nguvu..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom