Netanyahu: Iran sasa ni dhaifu


Kachanganyikiwa kama wewe



View: https://www.youtube.com/watch?v=s0KDOjsIHJg&t=16s
 
Baada ya kuangamiza viongozi wakuu wa Iran wa kidini na kijeshi na kuchakaza miundombinu mikuu ya kijeshi ya Iran, Trump aliwapa amri moja tu: anataka unconditional surrender! Kama aliyopata Venezuela. Hakukuwa na mazungumzo. Huyo ndio Trump.

Bahati mbaya Iran sio Venezuela. Alishangaa kuona drones na makombora ya bei rahisi yakishambulia bases na properties za maana za US huko nchi za Ghuba na kupenya iron dome ya Israel. Kisha wakadhibiti pito la Hormuz na kuweka “kibanda cha tozo” (toll booth) na kuanza kukusanya US2m kwa kila meli wanayoiruhusu kupita. Meli zlizolazimisha kupita zilipigwa makombora. Bei za oil zikapanda. Hofu ya kiuchumi ikatanda US na duniani. Hilo ndilo jibu alilopata toka Iran. Akashtuka sana. Hakutegemea.

Nani anaongoza mashambulizi huko Iran? Hamjui. Waongee na nani? Hajui. Wote waliokuwa wanaongea nao wamewaua! Walioonekana kuwa na hekima na simile wamewapuuza na kuwaua sasa wanahangaika na vichaa wasiojulikana.

Trump sio mtu wa kuongea na watu wanyonge na masikini. Hata ndani ya nchi yake na ndani ya serikali yake. Anaabudiwa. Viongozi wa Ulaya/NATO anawasemea mbovu kila wakati. Alimdhalilidha Zelenskyy vilivyo WH. Anaowaheshimu hapa duniani ni Putin, Xi, na Kim.

Pakistani wamejitolea kuleta muafaka. Iran walidai timu ya US iongozwe na VP JD Vance ndio watashiriki. Trump akakubali. Haijawahi tokea US kupangiwa mjumbe wake kwenye mazungumzo.

Anyway, yameshindikana. Hakuna haja ya maneno mengi. Sasa tunasubiri kuona jinsi US na Israel watakavyoichakaza Iran hadi kurejea zama za mawe (Stone Age) kama wengi mnavyotarajia.
 

Sisi Makobaz uongo ni suna Muddy pia alikuwa muongo na tapeli ndo tunapita humo humo. Kwa mjomba wetu
 
Kama iran dhaifu anaogopa nn kwenda ardhini,,, na yy ndio dhaifu zaid maana sio kipondo kile
 
Nani anaongoza mashambulizi huko Iran? Hamjui. Waongee na nani? Hajui. Wote waliokuwa wanaongea nao wamewaua! Walioonekana kuwa na hekima na simile wamewapuuza na kuwaua sasa wanahangaika na vichaa wasiojulikana.
😁😁😋😋Labda Ni majini ndiyo yanayopigana.
 
😁😁😋😋Labda Ni majini ndiyo yanayopigana.
Inawezekana kwa wanaoamini katika hayo madude.

Kazi ngumu sana kupigana na watu wasioogopa kifo wala wasio na tamaa ya Maisha ya dunia hii. Ni kama kupigana na "majini"😁

Kule Afghanistan Soviet Union walikimbia baada ya miaka tisa ya kuangamiza maelfu ya wapiganaji wa Mujahideen. US walikimbia baada ya miaka ishirini ya kupambana na Taliban pamoja na kuua maefu yao.

2003 US waliingia Iraqi kwa mbwembwe wakaichakaza kwa makombora (desert storm/shock and awe). Wakasambaratisha utawala wa Saddam Hussein. Wakampitisha kwenye Kangaroo court akanyongwa. Wakatangaza ushindi mwaka huohuo (Mission Accomplished). Kabla hawajakaa sawa wakajikuta wakikabiliana na kundi la ISIS lililowapeleka puta hadi 2011 walipoamua kubwaga manyanga na kuondoka Iraq haraka sana wakiacha civil war. Hata Wakristo wachache waliokuwa huru kuabudu wakati wa Saddam Hussein ndio ikawa mwisho wa jamiii hiyo.

Tuone Trump atafika wapi na hayo majitu. Wao wanasema: you have the watches, we have the time (wewe unamiliki saa, sisi tuna muda).

Kajiletea tabu ya bure kwa kumuendekeza Netanyahu. Hakujiuliza kwa nini Netanyahu na ubabe wake wote amehangaika kutafuta support ya US miaka 40 ili kuipiga Iran na kukakataliwa na maRais wote wa US kabla ya Trump.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…