Netanyahu aachia mamlaka ofisi za wizara

Netanyahu aachia mamlaka ofisi za wizara

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,286
Reaction score
10,831
1578031483313.png
Waziri Mkuu wa Israel Benjami Netanyahu ataachia mamlaka ya wizara kadhaa ambazo awali zilikuwa chini yake, huku akiwa anakabiliwa na mashtaka ya ufisadi.

Ofisi yake imethibitisha leo kwamba Netanyahu atabaki kuwa waziri mkuu, lakini wizara za afya, maswala ya kijamii, kilimo na inayowashughulikia wanaoishi nje ya nchi hazitakuwa tena chini ya mamlaka yake.

Jakov Litzman, naibu waziri wa afya wa zamani, ameteuliwa kuwa waziri mpya wa afya. Watakaochukua nyadhifa za wizara hizo na ofisi nyinginezo watatangazwa wiki ijayo.

Mwendesha mashtaka mkuu alitangaza mwishoni mwa mwaka jana kwamba Netanyahu atashtakiwa kwa makosa ya kuhusika na hongo, udanganyifu na uvunjaji wa uaminifu.


Chanzo: DW Swahili
 
Back
Top Bottom