NEC nitajuaje jina langu lipo kwenye kituo gani baada kupanga kituo kimoja kuhudumia watu wasiozidi 500?

Mwifwa

JF-Expert Member
Apr 3, 2017
46,921
122,189
Vituo vingi vimeandikisha wapiga kura zaidi ya 500, NEC wanasema katika uchaguzi wa mwaka huu kituo kimoja kitahudumia watu wasiozidi 500.

Kwa mantiki hiyo vituo vitakuwa vimegawanywa na majina yatakuwa yamegawanywa na kupelekwa kwenye vituo vipya.

Kwa wale ambao majina yao yamehamishwa kwenye vituo vipya ili kukidhi matakwa ya kituo kimoja kuhudumia watu wasiozidi 500, NEC mnatujulisha vipi vituo vyetu vipya ili kuepuka usumbufu wa Octoba 28, 2020 pindi ambapo kila mmoja wetu atakapoandaa jambia lake maridhawa kwa kazi mahususi ya siku hiyo?

Kwenye kuhakiki taarifa zetu mumetupa namba *152*00# ambayo tunaitumia kupitia simu zetu kujua taarifa zetu.

Kwenye hizo taarifa naombeni muongeze kipengele cha kutujulisha kituo cha kupigia kura endapo jina litakuwa limehamishwa kituo kipya tofauti na kile ulichoandikishwa.
 
2020 naenda kuweka historia
1.Kupiga kura kwa mara ya kwanza kwa uchaguzi mkuu...
2.Kuwa sehemu ya uchaguzi huu wenye mvuto wa aina yake tangu mfumo wa vyama vingi.

Tafadharini wazoefu wa kupiga Kura mzidi kutupatia elimu walau hapa jamvini isitokee tukaharibu kura zetu au kushindwa kupiga kwa sababu fulani fulani...

Muhimu pia, NEC toeni huo utaratibu wa majina kuhamishwa vituo.
 
Kama ulijiqndikisha kituo A basi jina lako litakuwa kituo A pale pale na ndipo utakapo pigia kura!

Vituo viliongezwa kabla ya mchakato wa kuandikisha wapiga kura kwa hiyo uwezi kupelekwa kituo ambacho hukujiandikisha!

NEC hupeleka majina pale watu walipo jiandikisha na vituo viliongezwa kabla ya watu kujiandikisha hivyo uwezi kupelekwa kwenye kituo ambacho hujajiandikisha
 
NEC hupeleka majina pale watu walipo jiandikisha na vituo viliongezwa kabla ya watu kujiandikisha hivyo uwezi kupelekwa kwenye kituo ambacho hujajiandikisha

Nimejiandikisha mwaka 2015, na taarifa zangu zipo sahihi kwenye hicho kituo(nimehakiki sasa hivi kwenye simu).

Kituo kile kilikuwa na watu wengi sana ukizingatia kipo jijini Dar karibu na makazi ya wakubwa.

Sasa kama kituo hicho katika uchaguzi wa Octoba kitahudumia watu wasiozidi 500(kwa mujibu wa NEC), jee wengine watapigia kura wapi? Watajuaje kituo yalipohamishwa majina yao?
 
Hili shina la CCM halina lolote
Kama hawatatupatia njia bora ya kujua vituo walivyotuhamisha kwa ajili ya kupigia kura, itakuwa ni usumbufu mkubwa sana ifikapo tarehe 28 Oktoba.

Kituo kilichoandikisha watu zaidi ya 500 halafu kije kihudumie idadi isiyozidi 500 bila kutaarifu wengine vituo waliohaishiwa itakuwa ni shida sana kwa wapiga kura.

NEC watufafanulie kuhusu hili jambo ingali mapema kabla ya siku ya uchanguzi
 
Back
Top Bottom