Ndoani

Ndoani

Madigo

Member
Joined
Mar 7, 2013
Posts
24
Reaction score
11
[h=5]MKE KAMZIDI MSHAHARA MUME...hivi mnadeal nayo vipi hii....ile desturi ya kuwa Mwanamme ndo provider wa familia inakuwaje hapa.....!! na Je mahitaji yako yanakuwaje as Mwanamke, utahudumiwa au ndo inakuwa juu yako...
La mwisho, Mnagawana vipi majukumu.....please lets discuss hasa wenye uzoefu..!![/h]
 
Mwanamume atabaki kuwa mwanamume, hii haijalishi kuwa ana kipato kidogo ama kikubwa, anazidiwa na mwanamke ama la ila inategemea unaendeshaje familiya yako. Kama huyo ni mkeo mnatakiwa kuwa kitu kimoja mishahara yenu muiweke pamoja mpange mikakati kwa pamoja na kwa umoja japo hii inategemea tangu mwanzo mlianzaje mahusiano yenu ya kimapenzi na kifedha. A man is not a provider but a guider hivyo hata kama mkeo anakuzidi kipata anaweza kukuheshimu lna kuuleta mshahara wake wote mkaupanga kama hii fedha ni kwa ajili ya kusomeshea watoto, hii matumizi nyumbani, hii yako mama, hii yangu baba, hii ya dharula, hii akiba na hii ku-support ndugu na jamaa. Mambo yanakwenda vizuri ila kama ndoa imetawaliwa na ubinafsi, usaliti na kiburi basi mnatakiwa kubadili mtazamo na kuanza kushirikiana. Upandacho ndicho uvunacho hivyo nashauri ni bora mtu achukuwa mda kumpata mke anayemfaa kuliko kuangalia juu juu tu na kuopoa mke, maisha hayana kanuni hubadilika wakati wowote hivyo ni vyema kuchukua tahadhari kabla ya hatari.
 
Ingawa sna ndoa ila nadhani kati ya vitu vya msingi mwaanamme anavyotakiwa kua navyo ndani ya nyumba ni msimamo.
ukiwa na akili na msimamo hata kama kipato chako ni kidogo kuliko cha mwenzako bado nyumba itanyookatu.
hata hivyo hapa akili na msimamo ninaozungumzia ni lazima uwe chanya..........sio unakua namsimamo wa kibinafsi au usiokua na manufaa kwa famila af utegemee mkeo akuelewe wakati anahela kuliko wewe! Utaachwa.
lakini pia cha msingi ni mapenzi ya dhati kwa familia yenu.
kama kwa kipato kidogo kuliko cha mama ulichonacho unaonesha udhati kwa familia yako kwa hakika mama mwenye akili hatoacha kukupa sapot
Mwishoo, ingawa riziki haivutwi kwa kamba ila kwa kweli unapoona halikama hii inabidi
kuongeza mishemishe, kama unaomshahara uangalie namna ya kufanya na deal zingine iliuwe juu ya mama. hii hua inaongeza heshima ndani ya familia.
 
kwani ndoa siku hizi ni lazima mwanaume ndo uwe na mshahara mkubwa kuliko mwanamke?

Ngoja nipate shule na mm hapa
 
Back
Top Bottom