ndoa ya binamu yangu iko hatarini msaada tafadhali

ndoa ya binamu yangu iko hatarini msaada tafadhali

sakapal

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
1,804
Reaction score
1,425
Habari zenu wanajamvi wote na hongereni kwa kuingia 2013, amani na upendo kwenu wote. Jamani leo naombeni mnisaidie nimjibuje huyu binamu yangu maana tangu juzi ananipigia simu hajui afanyaje story ilianza hivi miaka kadhaa iliyopita.................


Hii ilimkuta binamu yangu kabisa ni kweli wala si story, (kosa kubwa wanalofanya wanaume wanaonyimwa watoto na wanawake waliozaa nao ni kutokuwa wawazi tangu mimba ina)poshika hadi mtoto kuzaliwa. Unajua nn, huyo binamu yangu alikuwa na boyfriend wake alikuwa anafanya kazi wakati huo binamu yangu yuko chuo, kufika mwaka wa pili binamu mimba ikashika huku na huku yule kaka akasema zaa chuo ntamalizia kukulipia kwani binamu alikuwa anasomeshwa na wazazi wake na mtoto ntalea si ninafanya kazi? binamu machale yakacheza akambembeleza jamaa akaitoa. Ile anamaliza mwaka wa tatu tu kabla hata ya majibu kutoka mimba ikakubali tena this time binamu hakuhofu kitu akijua sasa na harusi itafungwa kumbe jamaa alikuwa part time- hakuwa wa kuoa, ile kumwambia mimba imenasa jamaa akawaka mimba lazima itolewe na akampa na hela wakati ule alipewa Tsh 30,000/- gharama ya kutolea mimba (imeshapita miaka mingi tuu na mtoto now ni mkubwa) binamu huku na huku kachanganyikiwa akagoma kutoa ile mimba ila pesa alichukua ndo akanifata kwa ushauri je atoe mimba? na hela kanionesha huku akijiuliza kwanini niitoe hii mimba kama chuo nshamaliza na mie huyu jamaa nampenda na kama alikuwa hanipendi au hana mpango wa kunioa mbona iliposhika mimba ya kwanza alitaka nizae na huku akiniahidi atamalizia kunisomesha chuo kama nyumbani wangechukia mie kushika mimba wakati niko chuo? huku analia machozi nikamuonea huruma. Kwa akili yangu ya wakati ule nilimpa ujasiri na kumfariji kuwa asikate tamaa na asiitoe mimba as two wrongs does not make one right yaani kosa la kushika mimba nje ya ndoa na afanye na kosa la pili la kuitoa, nikamwambia je ukiwa unaitoa mimba ikagoma kutoka na ukajikuta unazaa mtoto mlemavu, je ukitoa mimba kikatoka na kizazi ukaja olewa aidha na yeye au na mwingine then watafuta mtoto wee utavumilia uchungu wa kutokuzaa hali ulitoa mimba kisa mwanaume haitaki? je kama huyu aliyetumboni kwako ni blessing from God utazuia mpango wa mungu? (kutokana na imani yangu) nikamwambia wajua hata yesu kabla ya kuzaliwa alikumbana na vikwazo vingi lakini kwasababu ilikuwa kusudi la mungu alizaliwa japo kwa shida nikamwambia tulia zaa mtoto wako jamaa atajirudi tuu na mtalea mtoto wenu na ile elf 30 nikamsindikiza akanunua cheni ya gold ya hela hiyo hiyo. Tena nikamwambia itakuwa ukumbusho wako kila uvaapo cheni hiyo juu ya mtoto utakayezaa. Basi home ikawa soo jamaa akakata mawasiliano kabisa thenk God akajifungua salama mtoto wake mzima mwenye afya tele. Baadae binamu yangu alipata kazi akamlea mtoto wake mwenyewe na mwaka mmoja baadae alimtafuta baba wake ili mauulize kwa mara ingine kama atajirudi yuko tayari kumsamehe ili wmlee mtoto wao pamoja. Jamaa akasema hana uhakika kama atamuoa na hataki kumuahidi chochote. Binamu yangu huku na huku miaka miwili baadae akapata mchumba aliyempenda kwa dhati na kuolewa huku huyu mchumba mpya akimlea mtoto wa binamu yangu kama wake na jina alimbadilisha liwe la ubini wa mumewe.
Sasa kuanzia siku baada ya xmas binamu yangu akanipigia simu anashida, yule baba wa mtoto wake amejirudi eti anataka mtoto wake amlee ameona na yuko na mke mwingine na anataka amsomeshe na kumtengenezea kadi ya matibabu, wakati huku yeye (binamu) na mumewe wanamlea kwa hali nzuri wala hajajua hata kama yule si baba yake halali. Jamaa anamwambia namtaka mtoto wangu binamu kachanganyikiwa kwani hataki mtoto wake aende kulelewa na mwanamke mwingine na bado hajamwambia mumewe mie bado sijamwambia cha kufanya ila naomba wanajamvi mnisaidie nimshaurije? mtoto mwenyewe anaumri wa miaka 10. Ushauri tafadhali.
 
Anaekufa kwa dhiki ndio rafiki...

huyo baba naye mwanga tu, huyo dada asikubali mtoto wake alelewe na mama wa kambo, kama vipi ampeleke huyo baba kwenye vyombo vya sheria ili asiendelee kungangania mtoto..alipokuwa mdogo alimkataa leo ndio anamuona wa maana..pambaf kabisa
 
Mwambie amshirikishe mumewe wa sasa kupata ufumbuzi wa hili suala.
 
Msheeeeeeeeeeeeeeeeew!!!!!!!!!!!! special kwa hilo jinaume lilikotaa mtoto!!! Hakuna kumpa mtoto wala nini! Tena akienda ustawi unasema kuhusu kutoa pesa mimba itolewe! Asikubali wala nini!
 
Kwanini asiongee na mumewe ili wajue cha kufanya?

Mwansheria pia anahusika!
 
Habari zenu wanajamvi wote na hongereni kwa kuingia 2013, amani na upendo kwenu wote. Jamani leo naombeni mnisaidie nimjibuje huyu binamu yangu maana tangu juzi ananipigia simu hajui afanyaje story ilianza hivi miaka kadhaa iliyopita.................


Hii ilimkuta binamu yangu kabisa ni kweli wala si story, (kosa kubwa wanalofanya wanaume wanaonyimwa watoto na wanawake waliozaa nao ni kutokuwa wawazi tangu mimba ina)poshika hadi mtoto kuzaliwa. Unajua nn, huyo binamu yangu alikuwa na boyfriend wake alikuwa anafanya kazi wakati huo binamu yangu yuko chuo, kufika mwaka wa pili binamu mimba ikashika huku na huku yule kaka akasema zaa chuo ntamalizia kukulipia kwani binamu alikuwa anasomeshwa na wazazi wake na mtoto ntalea si ninafanya kazi? binamu machale yakacheza akambembeleza jamaa akaitoa. Ile anamaliza mwaka wa tatu tu kabla hata ya majibu kutoka mimba ikakubali tena this time binamu hakuhofu kitu akijua sasa na harusi itafungwa kumbe jamaa alikuwa part time- hakuwa wa kuoa, ile kumwambia mimba imenasa jamaa akawaka mimba lazima itolewe na akampa na hela wakati ule alipewa Tsh 30,000/- gharama ya kutolea mimba (imeshapita miaka mingi tuu na mtoto now ni mkubwa) binamu huku na huku kachanganyikiwa akagoma kutoa ile mimba ila pesa alichukua ndo akanifata kwa ushauri je atoe mimba? na hela kanionesha huku akijiuliza kwanini niitoe hii mimba kama chuo nshamaliza na mie huyu jamaa nampenda na kama alikuwa hanipendi au hana mpango wa kunioa mbona iliposhika mimba ya kwanza alitaka nizae na huku akiniahidi atamalizia kunisomesha chuo kama nyumbani wangechukia mie kushika mimba wakati niko chuo? huku analia machozi nikamuonea huruma. Kwa akili yangu ya wakati ule nilimpa ujasiri na kumfariji kuwa asikate tamaa na asiitoe mimba as two wrongs does not make one right yaani kosa la kushika mimba nje ya ndoa na afanye na kosa la pili la kuitoa, nikamwambia je ukiwa unaitoa mimba ikagoma kutoka na ukajikuta unazaa mtoto mlemavu, je ukitoa mimba kikatoka na kizazi ukaja olewa aidha na yeye au na mwingine then watafuta mtoto wee utavumilia uchungu wa kutokuzaa hali ulitoa mimba kisa mwanaume haitaki? je kama huyu aliyetumboni kwako ni blessing from God utazuia mpango wa mungu? (kutokana na imani yangu) nikamwambia wajua hata yesu kabla ya kuzaliwa alikumbana na vikwazo vingi lakini kwasababu ilikuwa kusudi la mungu alizaliwa japo kwa shida nikamwambia tulia zaa mtoto wako jamaa atajirudi tuu na mtalea mtoto wenu na ile elf 30 nikamsindikiza akanunua cheni ya gold ya hela hiyo hiyo. Tena nikamwambia itakuwa ukumbusho wako kila uvaapo cheni hiyo juu ya mtoto utakayezaa. Basi home ikawa soo jamaa akakata mawasiliano kabisa thenk God akajifungua salama mtoto wake mzima mwenye afya tele. Baadae binamu yangu alipata kazi akamlea mtoto wake mwenyewe na mwaka mmoja baadae alimtafuta baba wake ili mauulize kwa mara ingine kama atajirudi yuko tayari kumsamehe ili wmlee mtoto wao pamoja. Jamaa akasema hana uhakika kama atamuoa na hataki kumuahidi chochote. Binamu yangu huku na huku miaka miwili baadae akapata mchumba aliyempenda kwa dhati na kuolewa huku huyu mchumba mpya akimlea mtoto wa binamu yangu kama wake na jina alimbadilisha liwe la ubini wa mumewe.
Sasa kuanzia siku baada ya xmas binamu yangu akanipigia simu anashida, yule baba wa mtoto wake amejirudi eti anataka mtoto wake amlee ameona na yuko na mke mwingine na anataka amsomeshe na kumtengenezea kadi ya matibabu, wakati huku yeye (binamu) na mumewe wanamlea kwa hali nzuri wala hajajua hata kama yule si baba yake halali. Jamaa anamwambia namtaka mtoto wangu binamu kachanganyikiwa kwani hataki mtoto wake aende kulelewa na mwanamke mwingine na bado hajamwambia mumewe mie bado sijamwambia cha kufanya ila naomba wanajamvi mnisaidie nimshaurije? mtoto mwenyewe anaumri wa miaka 10. Ushauri tafadhali.

Umemsoma baba wa mtoto... Kiranja Mkuu?
https://www.jamiiforums.com/mahusia...mwenza-anangangania-mwanangu.html#post5362874
 
very simple.....ingekuwa mie ningemtoa spidi 180 kama sio 240.......... Hakuwa na uchungu mwanzo apate uchungu sasa?

Kama binamu yako anataka kutupa mtoto athubutu.......

Amwambie mtoto anae baba haitaji baba wa ziada.........


Asubirie mtoto akikua atamtafuta
 
Sasa uhatari wa ndoa yake hapo uko wapi????

wakati binamu yangu anachumbiwa na huyu mumewe, mume wake akamwambia tafadhali sitapenda wala sitafurahia wala sitarajii kusikia mkiwasiliana na baba wa mtoto an nisije nikasikia siku unaniambia baba wa mtoto anamtaka mtoto nawe ukasema umpe. Huyu baba wa mtoto ndie amekuwa akimtumia binamu yangu mail japo binamu anasema hamjibu na anaogopa mumewe akijua jamaa anafatilia mtoto anaweza kuwaka na kuleta migogoro kwenye dnoa yao as huyu baba wa mtoto anatuma email na kuonesha anakuja kwa nguvu kudai mtoto wake. Nimeongea nae mchana huu na kumshauri binamu yangu aongee na mumewe kuhusu hili week end hii kabla jamaa hajajileta home kwao na kumgeuzia kibao.
 
very simple.....ingekuwa mie ningemtoa spidi 180 kama sio 240.......... Hakuwa na uchungu mwanzo apate uchungu sasa?

Kama binamu yako anataka kutupa mtoto athubutu.......

Amwambie mtoto anae baba haitaji baba wa ziada.........


Asubirie mtoto akikua atamtafuta

asante sana naufikisha huu ujumbe kama ulivo bila kuuongeza wala kuupunguza, ubarikiwe
 
Alipo zaa nje ya ndoa hakujua kutakuwa na madhara.
 
Mshauri huyo ndugu yako asikubali upuuzi huo,amwambie wala mtoto si wako kwani mimba yako
niliitoa kwa 30,000 uliyonipa,nilikuwa nakuongopea tuu ili unioe,tena mwambie hakuna haja ya kumficha
mumewe atafute muda mwafaka amweleze taratibu na kumuomba amsaidie kumshikisha adabu jamaa
kwa kutaka kuiba mtoto asiye wake,ninyi pia ndugu msaidieni ndugu yenu kumvuruga huyo jamaa mpaka
asiwe na hamu tena ya kudai mtoto.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom