Habar zenu waadau
Naomba niende directly, kuna mahali flan mkoa wa manyara hua nafanya kilimo, katika halakat zangu za kilimo nikaona niwe napeleka na biashara ya nguo
Nikanunua robota moja la suruali za kiume nikapeleka na biashara ikawa nzuri tu
Nikawa nazunguka na kwenye magulio ya vijiji vya jiran kiukweli biashara sio mbaya ukanda huu
Kuna lafiki yangu mmoja akanishauri kwamba nifungue saloon
Maana eneo hilo kuna uhitaji wa saloon na zilizopo hazikidhi viwango kias kwamba watu wenye hadhi husafili umbali mrefu kwenda kutafta saloon zenye hadhi hasa walimu watendaji wafanyakaz wa zahanati
Nikaufanyia kazi ushauri nikaludi home nikajipanga nikanunua sofa kali mziki mnene mashine na kila kitu
Nikapata flame nzuri kbsaa yenye hadhi nikaanza kutafuta kinyozi
Kuna jamaa akasema yupo kijana ambae yeye hua ananyoa kwa kutumia wembe anakubalika kijiji chote hivo nimtafute
Nikamtafuta na nikamwambia nataka awe ananilipa kwa week, ijapokua sikua nimepanga ni kiwango gan kwa sababu sikua nimejua mzunguko wa biashara
Tukakubaliana tukae week moja wote tuone ratio yake,
Lakini akaniambia kua bado anavuna mazao yake kwa hio akimaliza ataanza rasmi lakini atakua anakuja siku anauokua free nikamkubalia
Kiukweli baada ya kufungua saloon yangu nilifanya saloon nyingine wafunge na wengine kuhama kijiji
Watu wote waliiipenda saloon yangu kwa jinsi nilivoipangalia
Shida ikaanza kwa huyu kinyozi wangu amemaliza kuvuna lakini haishiwi visingizio kila leo atasema kaenda msibani kesho atasema ni zamu yake kuchunga kesho kutwa atasema mtoto kaumwa kampeleka hospital
Yaani kwa week anaweza kuja siku tatu au nne, ipo ivi hulka ya hiki kijiji vijana wakiwa na mahindi ndani kazi hawafanyi kabisaaa
Nimewekeza nusu ya mtaji wangu wa nguo hapo nikitegemea utaludi,
kichwa kinawaza mpk sijui nifanyeje
Na kupata kijana mwingine ni ishu sana kias kwamba kuna dogo hua namtafuta akae huyu kinyozi akiwa hayupo , lakini wateja wakija wanasema kama muhusika hayupo hawanyoi na kuondoka
Kuna muda anaweza akaja kazini akafunga ukimuuliza kaenda kuangalia mechi mara kaludi nyumbani kula
Wadau Hapa nipo dilema nini nifanye