Nauza Shuka za Kigoma

Nauza Shuka za Kigoma

albertt

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2013
Posts
339
Reaction score
78
shuka za kigoma futi (6×6) zikiwa na forinya(2).zipo rangi na maua mbalimbali nauza shilingi 45,000 kwa shuka 1 kama upo serious nichek 0716385824
 

Attachments

  • 1439457020547.jpg
    1439457020547.jpg
    59.8 KB · Views: 1,283
  • 1439457033861.jpg
    1439457033861.jpg
    47 KB · Views: 1,149
  • 1439457047316.jpg
    1439457047316.jpg
    54.2 KB · Views: 1,093
  • 1439457059964.jpg
    1439457059964.jpg
    48.7 KB · Views: 983
  • 1439457072982.jpg
    1439457072982.jpg
    54 KB · Views: 1,186
  • 1439457085353.jpg
    1439457085353.jpg
    51.5 KB · Views: 1,015
Naomba ufafanuz zaid mkuu, zina ukubwa gani, foronya kama zipo au hazipo na ni ngap, shuka ni pair au ni moja
 
Naomba ufafanuz zaid mkuu, zina ukubwa gani, foronya kama zipo au hazipo na ni ngap, shuka ni pair au ni moja

zina ukubwa wa futi 6×6 ni pair moja na ni foronya 2 unapata
 
Mleta Mada kwanza nakushauri fanya yafuatayo.
-Tafuta Camera Nzuri ili upate picha kubwa na Nzuri.Na ukitaka picha nzuri piga ikiwa kwenye kitanda
-Pia umejibu mtu kwamba bei hiyo ni kwa pair,wakati sio kweli,bei hiyo ni kwa shuka moja yenye foronya mbili.
-Halafu umepost copy moja tu aina ya Mwiba,ila umesahau kuweka na aina ya Mjazo.

Hizi shuka ni imara sana,na zinadum muda mrefu na ni attractive saaana.
Ninazo nyingi sana niliwahi kununua nilipokuwa natokea Congo kupitia Kigoma.Na zinafumwa kwa mkono

Hembu jazia hizi hapa chini
1.JPG 1.JPG 1.JPG 3.JPG 4.JPG
 

Attachments

  • 2.JPG
    2.JPG
    123.1 KB · Views: 1,029
Mleta Mada kwanza nakushauri fanya yafuatayo.
-Tafuta Camera Nzuri ili upate picha kubwa na Nzuri.Na ukitaka picha nzuri piga ikiwa kwenye kitanda
-Pia umejibu mtu kwamba bei hiyo ni kwa pair,wakati sio kweli,bei hiyo ni kwa shuka moja yenye foronya mbili.
-Halafu umepost copy moja tu aina ya Mwiba,ila umesahau kuweka na aina ya Mjazo.

Hizi shuka ni imara sana,na zinadum muda mrefu na ni attractive saaana.
Ninazo nyingi sana niliwahi kununua nilipokuwa natokea Congo kupitia Kigoma.Na zinafumwa kwa mkono

Hembu jazia hizi hapa chini
View attachment 275930View attachment 275930View attachment 275930View attachment 275936View attachment 275937

Sasa ajazie kama hana hizo zako na mtu akitaka itakuwaje???
 
Sasa ajazie kama hana hizo zako na mtu akitaka itakuwaje???

Atakuwanazo,mie hiyo Biashara niliifanya sana miaka ya 90,nilikuwa nachukua Kigoma naleta Zanzibar kwa njia ya Posta mfumo wa Cargo.
Wafanyabiasahara wanajuana,akikosa kwake huwa wanatafuta kwa mwenzie.Na kama hana kama hizo aniambie nimuelekeze wapi akaweke Order yake.Maana niliisha stafu kazi hiyo ila channels zote ninazo naweza kumsaidia kama ni mchanga wa Biashara hiyo.Ila mpaka kupost humu ni kwamba na yeye anafaham.
Sema tu hizo zake na Mjazo huo ni bei tofauti sana.Hizo zake ndio za bei rahisi ila hizo nimezomwambia ajazie bei yake shughuli pevu.

Biashara nzuri kama akijipanga,na akitafuta masoko mikoa mbalimbali
 
Atakuwanazo,mie hiyo Biashara niliifanya sana miaka ya 90,nilikuwa nachukua Kigoma naleta Zanzibar kwa njia ya Posta mfumo wa Cargo.
Wafanyabiasahara wanajuana,akikosa kwake huwa wanatafuta kwa mwenzie.Na kama hana kama hizo aniambie nimuelekeze wapi akaweke Order yake.Maana niliisha stafu kazi hiyo ila channels zote ninazo naweza kumsaidia kama ni mchanga wa Biashara hiyo.Ila mpaka kupost humu ni kwamba na yeye anafaham.
Sema tu hizo zake na Mjazo huo ni bei tofauti sana.Hizo zake ndio za bei rahisi ila hizo nimezomwambia ajazie bei yake shughuli pevu.

Biashara nzuri kama akijipanga,na akitafuta masoko mikoa mbalimbali

Nimekuelewa vema.
 
Mleta Mada kwanza nakushauri fanya yafuatayo.
-Tafuta Camera Nzuri ili upate picha kubwa na Nzuri.Na ukitaka picha nzuri piga ikiwa kwenye kitanda
-Pia umejibu mtu kwamba bei hiyo ni kwa pair,wakati sio kweli,bei hiyo ni kwa shuka moja yenye foronya mbili.
-Halafu umepost copy moja tu aina ya Mwiba,ila umesahau kuweka na aina ya Mjazo.

Hizi shuka ni imara sana,na zinadum muda mrefu na ni attractive saaana.
Ninazo nyingi sana niliwahi kununua nilipokuwa natokea Congo kupitia Kigoma.Na zinafumwa kwa mkono

Hembu jazia hizi hapa chini
View attachment 275930View attachment 275930View attachment 275930View attachment 275936View attachment 275937

Hahaha we nomaa sana hata me nnazo kweli kabisa unachosema
 
Hahaha we nomaa sana hata me nnazo kweli kabisa unachosema

Nakumbuka wakati nasoma,nilinunuliwa naanza form one hadi form 4 ngoma haijachanika,aisee
Maana wakati huo shuka plain zilikuwa zinatokea Burundi,na ndio ngum na nzuri kwa kufuma.Hizi za Dar watu wanazingulia tu.Sema tu warundi na wakongomani siku hizi wamejanjaruka,wanazileta wao wenyewe Tanzania hizi plain shuka.Ili wafumaji wasipate tabu
Ukienda Kigoma karibia kila nyumba kuna mfumaji wa Shuka hizi,ni sawa na Ukija huku Zanzibar Ukienda Kijiji cha Makunduchi karibia kila nyumba kuna watu wanne wanajua kufuma Kofia za mtobo ambazo bei yake ni kubwa ile Mbaya kuanzia Elf 25,000 hadi Elf 50 kutegemea na mfumo,Mie tangu niliponunua ilikuwa siku ya Kuoa,hahahaha
 
Hahahaha me moja nilipewaga kipindi nipo fom six mpaka leo ndo naimalizia fikilia nilienda chuo nkatumia nmemaliza nkatumia nkaingia kazini toka 2013 mpaka leo Yaan nazikubali sana
 
Hahahaha me moja nilipewaga kipindi nipo fom six mpaka leo ndo naimalizia fikilia nilienda chuo nkatumia nmemaliza nkatumia nkaingia kazini toka 2013 mpaka leo Yaan nazikubali sana

Hahaha,mie nilipooa basiz ile zanguz oote nikazigawa kwa wadogo zangu,maana wife alikuwa na zake kibao kaja nazo.
Hizo Hapo juu ni za mwaka niliooa 2004,picha hiyo nimezipiga juzi usiku kumjazia mdau,kama mpya.
Ila kama huziju utauzia zenye material siyo,kuna wengine wanafuma kwa kutumia Vitambaa vya mashuka vya Bongo,kama hujui utazukumizwa tu,ila kama umewahi kutumia basi ukiiguza tu unajua kwamba Kitambaa chake ni cha Burundi au Congo original,na kwa mie niliofanya hiyo biashara ndio kabisaa.
Ni sawa na Kitenge cha Wax,Soso au Dubai,uukinipa tu nakuambia ni feki au ni chenyewe.Dar watu wanapigwa saaana hasa kwenye Wax orginal.Ila ndio jiji.

Nataka nikitulia mwakani niangalie baadhi ya Nchi nje ya Tanzania kama zinaweza kupenya kwenye Soko.
Unajua watanzania tunasubiria hadi mgeni aje ndio tuanzishe na sie.
Watalii wengi wanapenda vitu vya kutengeneza kwa mkono na sio Mashine,sasa hizi shuka aisee ukiziangalia unaweza kufikiria mashine,mie miama ya 2000 nilipokuwa nazileta Zanzibar watu wengi walibisha kwamba sio mkono ni mashine.Nilipiga hela ile mbaya,ila niliacha baada ya kuoa hii biashara,maana kwa Wanawake ni balaaa,utavunja ndoa siku sio nyingi.
Wife alipokuja akaanza kiasi then watu wakawa wagum saana kulipa,tuka quite

Ila akitokea mjanja akaanzisha hii biashara kisasa zaidi itamlipa,ila lazima ajue kutoka kwenye soko la nje ya nchi,asihofie ushindani wa shuka za viwandani,huku Zanzibar watu wananunua mavitu ya ajabu bei kubwa kweli na wakati vya viwandani vipo,kazi za mkono wenzetu wanazihusudu saaana,tena uzuri wa shuka hizi mie nilikuwa napiha hela ile mbaya kwakuwa nilikuwa na deal na maharusi saaana,nachukua Order then namuambia mfumaji kwamba fuma jina la maharusi.Basi ukiwapelekea aisee wanafurahi sana unakula tenda tena.Maana order maalum ya Mfumo wa mjazo inaweza kufika mwezi mmoja mpaka miwili kuifuma inategemea na aina ya Copy yenyewe.Na rangi zenye kutoka sana ni Nyeupe,maroon na Zambarau
Ilikuwa wastan wa shuka 20 kwa wiki naagiza na zinaisha zote.

Mjanja aanze na website then ahakikishe anakuwa na aina zote za nguvu,apenye soko la nje.Mtaji wake ni wakawaida sana.Mwaka 2000 ilikuwa Tsh: 12,000 kwa jumla,ambapo mie nilikuwa nauza 25,000
Majuzi tu kuna family friend walitaka wife awasaidie kwa kumuomba saana, kwa ajili ya Harusi,akafuma mwenyewe akalamba 75,000.Wakali gharama halisi za Nyuzi na Shuka plain haikuzidi 25,000.

Ukizoe shuka hizi sio siri,kama teja unakuwa,yaani haya mashuka ya madukani hununui,mie mpaka leo sijui shuka hizi za madukani za kupack ni bei gani.All my shukaz ni kama hizo.


Mjanja aanzishe
 
Ambacho sintosahau wakati nipo Mdogo.Maana nilikuwa mchafu na mvivu saana kufua.
Basi Mother alinifumia shuka jeusi,halafu kwenye Copy akafuma kwa neno BATA MCHAFU
Aisee,hili neno lilikuwa linanizingua,maana mie mwenyewe nilikuwa nacheka sana,na siku ya kupewa shuka jipya nilicheka kweli,ila siku zilivyozidi kwenda madogo wakaanza kuzingua,basi nilianza kubadilika ado ado,maana nikilala ninalo,nikiamka ninalo.
Na wakati huo wadogo zangu wengine ndio walikuwa wanajifunza kusoma na kuandika,basi hawaoni cha kusoma zaidi ha hilo neno,nilikuwa natembeza kichapo ila dingi akirudi namie nakula changu.Basi usafi ulianza taratibu.
 
Zanzibar Spices mbona umetembea sana na huu uzi zaidi ya mwenyewe alieuanzisha?ama mnataka kutupiga cheusi-chekundu?
 
Last edited by a moderator:
Hahaha,hapana wakuu.
We angalia numbeR ya mhusika,mie hata sijui anapotoka na anapokaa.
Ila nimechangia kwa kuwa mie niliifanya hii kwa miaka mingi,na hata hivyo siifanyi tena,nimeacha miaka ya 2004.

Na mie siwezi kuweka Copy Simple kama hizo zake.Namshukuru mungu sana biashara zangu huwa sikurupuki hata siku moja.
All my biashara zipo kwenye mtandao,hata vi Suzuki Carry vyangu na bodaboda mkuu,nina website zangu kwa biashara hiyo na nimesajili kampuni ya usafiri hata kama ninavyo vichache ili inipe moyo niweze kuongeza juhudi katika hilo namie niwe na mascania makubwa,naendelea kumuomba mungu.

Lengo ni kumpa Moyo mleta mada,kwanza Mie all my life nipo Zanzibar na mie huwa sijifichi kusema biashara zangu,maana is my life.Ila mleta mada aliileta kijuujuu saana ndio nikampa njia ya kuweza kuwa bora zaidi.
Muungwana anaweza kukunyima pesa ila hawezi kukunyima ujuzi wa biashara husika.
 
Hahaha,hapana wakuu.
We angalia numbeR ya mhusika,mie hata sijui anapotoka na anapokaa.
Ila nimechangia kwa kuwa mie niliifanya hii kwa miaka mingi,na hata hivyo siifanyi tena,nimeacha miaka ya 2004.

Na mie siwezi kuweka Copy Simple kama hizo zake.Namshukuru mungu sana biashara zangu huwa sikurupuki hata siku moja.
All my biashara zipo kwenye mtandao,hata vi Suzuki Carry vyangu na bodaboda mkuu,nina website zangu kwa biashara hiyo na nimesajili kampuni ya usafiri hata kama ninavyo vichache ili inipe moyo niweze kuongeza juhudi katika hilo namie niwe na mascania makubwa,naendelea kumuomba mungu.

Lengo ni kumpa Moyo mleta mada,kwanza Mie all my life nipo Zanzibar na mie huwa sijifichi kusema biashara zangu,maana is my life.Ila mleta mada aliileta kijuujuu saana ndio nikampa njia ya kuweza kuwa bora zaidi.
Muungwana anaweza kukunyima pesa ila hawezi kukunyima ujuzi wa biashara husika.

Noted with thanks mkuu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom