Taarifa hazijakamilika, hiyo siyo namna ya uuzaji gari. Halafu inaonekana ina matatizo mengi maana hata tairi la nyuma upande wa kulia takriban nati tatu hakuna hapo. Si majanga hayo.
Usiangalie nati ya Sh. mia tano. Tambua kuwa hata gari ambalo limetoka japan leo hukutwa na mapungufu kadhaa madogo madogo mfano, kutokuwepo jeki na wheel spanner, vioo kutopanda na kushuka, betri kutofanya kazi, kutokuwepo na tairi la spea, speedometer kutofanya kazi na mengine kadhaa
Ndg weka picha na specifications za hiyo gari. Hebu elezea hiyo gari yako vizuri. Ulinunua lini, ilianza kutumika hapa Bongo lini, iko kwenye hali gani, tatizo lake ni nini, kwa nini unaiuza, kuna guarantee yoyote? Mbona umetuonyesha ubavu wa gari tu kisha unatarajia serious buyer? Hujaweka contacts zozote na wala kama kuna mazungumzo...biashara za siku hizi hasa humu JF kila kitu huwekwa wazi. Asante
Mi nina gari iko kwenye km 220000 kwa sasa na iko poa sana.Gari ni matunzo tu,kurepair,kuserviice kwa wakati na mafuta masafi.Hata kama ni km 10000 kama hamna matunzo mazuri,litakuwa bovu tu.
Mi nina gari iko kwenye km 220000 kwa sasa na iko poa sana.Gari ni matunzo tu,kurepair,kuserviice kwa wakati na mafuta masafi.Hata kama ni km 10000 kama hamna matunzo mazuri,litakuwa bovu tu.
Kuna watu wamekariri kwamba ubora wa gari ni kilomita chache,watu na namna hiyo kuwaingiza mkenge ni rahisi sana,kwa sababu wao hawanunui gari wananunua ODMT.
Vimeo kama hivo unanunua mil 9 lakin matengenezo mil 6, inabid uwe na namba za sim za mafund kila angle ya jiji, kidum cha maji Kwa ajili ya engine kuchemsha, kamba ya kuvutia gari, tochi, wire wa ku bust betri, Faida pekee utayokuwa nayo hutaishi kwa wasiwas wa kuibiwa Gar yako!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.