hi wana JF, hivi karibuni nilimsikia waziri wa nishati na madini akiongea kwenye TV kupitia taarifa ya habari ya ITV saa mbili usiku akisema kuwa bei ya mafuta imeshuka chini ivo anaagiza Tanesco kushusha bei ya umeme na kuagiza pia Sumatra kushusha nauli ya daladala na magari yaendayo mikoani ili na sisi wananchi tupate nafuu ya ushukaji bei ya mafutai, mpaka sasa Tanasco wameshusha nauli kwa shilingi nane ila hawa Sumatra sijui wamegoma ama vipi? na waziri ametoa kauli hatujaona kama anafatilia hili liweze kutekelezwa, tunamuomba tena atupe mrejesho kitu gani kinasuburiwa hapa, kuna siku tena nimemsikia afisa wa sumatra akisema spare za magari zimepanda juu ivo wanafidia kwenye kushuka bei ya mufuta nikavunja moyo na kukosa matumaini.
kama Sumatra wanapita humu tunaomba mrejesho wa nauli kushaka kuanzia tarehe moja.
kama Sumatra wanapita humu tunaomba mrejesho wa nauli kushaka kuanzia tarehe moja.