NAULI MPYA: ushauri wangu kwa selikari na Sumatra

NAULI MPYA: ushauri wangu kwa selikari na Sumatra

Naibili

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2011
Posts
1,878
Reaction score
1,060
serikali kupitia sumatra wametangaza nauli mpya mwezi huu na zimeanza kutumika tangu tarehe 12/4 l, kwa mujibu wa sumatra ni kuwa kupanda kwa bei kumefuata taratibu zote, hii si hoja yangu.
ushauri wangu:
Nadhani imefika wakati watu wa sumatra waanze kufanya kazi zao kwa ufanisi ili waitendee haki hela wanazilipwa kutokana na kodi zetu,
kuna namna nyingi zinaweza kufanywa na serikali na kupunguza gharama kubwa inayotumiwa na wananchi hasa wa kipato cha chini ambao asilimia kubwa wanaishi chini ya dola moja,

kwanza wanatakiwa kuifungua stend ya makumbusha. hii itasaidia wale wote wanaotumia bara bara ya mandela rd na morogoro rd badala ya kulipa 800 au zaidi watapanda gari moja hivyo kutumia 400, huu ni kama mfano maana zipo stend nyingi zikitumika zinaweza kupunguza nauli zinazo lipwa mara mbili wakati inaweza kutumika nauli moja.

jambo la pili ni kuanzisha ruti mpya, kwa mfano posta-kawe via kibaki rd, kawe-temeke via mandela rd. na nyingine nyingi itawasaidia watu kulipa nauli moja.

jambo la tatu, kudhibiti ukatishwaji wa ruti hasa nyakati za asubuhi na jioni, gari nyingi hubadili ruti na kwenda kwingine huku wakibadili nauli na kufanya kati ya 1000 na 2000 hii inawaumiza wananchi wengi hasa wale wa mbagala, mbezi ya kimara, tangi bovu na tegeta ... n.k,

yako mambo mengi serikali inaweza kufanya bila kupunguza nauli iliyowekwa na wananchi wakapata unafuu, mengine mtaongezea wadau mimi ntaendelea baadae.

naomba kuwasilisha
 
jambo la tatu, kudhibiti ukatishwaji wa ruti hasa nyakati za asubuhi na jioni, gari nyingi hubadili ruti na kwenda kwingine huku wakibadili nauli na kufanya kati ya 1000 na 2000 hii inawaumiza wananchi wengi hasa wale wa mbagala, mbezi ya kimara, tangi bovu na tegeta ... n.k,

Hapa umeongea jambo ambalo kwa sasa ni tatizo kubwa.

Nauli zimepanda na mwananchi anaumizwa tena na ukatishwaji wa ruti. Mimi nashauri SUMATRA wapige marufuku tabia hiyo, pia wapige marufuku kondacta na wapiga debe kuita watu kuingia kwenye daladala ili watu waingie wenyewe kwa kusoma ruti ya gari (kama mtu hawezi kusoma basi aulize mwenyewe ili kusaidiwa).

Kwa sasa hali ni mbaya mida hasa ya jioni

MTONGANI - KAWE ruti: ukipanda Mtongani wanapiga debe mwisho magomeni/studio lakini cha ajabu watu wakishashuka hapo magomeni/studio wanaanza kupakia tena mpaka Kawe. HII SIO SAWA

kwahiyo kwa nauli ya sasa inamlazimu mtu atumie Tsh 1000 kufika kawe BADALA ya Tsh 600 halali.
 
asante saana bagain tukiunganisha mawazo yetu na sumatra wakaacha kukaa ofisini wafanye kazi yao, hata kawe-kariakoo huwa wanafanya kawe-magomeni nyakati za jioni hivyo kusababisha usumbufu pamoja na gharama kubwa kwa abiria wa maeneo hayo.
 
Last edited by a moderator:
Kwa wakazi wa mbagala hususani ruti ya k'koo mb'gala, kwa nyakati za jioni kuanzia saa moja hadi saa mbili,usiku ni muda wa mateso kwao. Kwani muda huo gari huwa hazionekani kabisa. Serikali kupitia vyombo vyenye mamlaka juu ya jambo hili vilitazame kwa ukaribu zaidi ili kuepuka gharama zisizositahili kwa abiria. Kwani wengi hulazimika kuunganisha magari pasipo na ulazima wa kufanya hivyo.
 
Kwa wakazi wa mbagala hususani ruti ya k'koo mb'gala, kwa nyakati za jioni kuanzia saa moja hadi saa mbili,usiku ni muda wa mateso kwao. Kwani muda huo gari huwa hazionekani kabisa. Serikali kupitia vyombo vyenye mamlaka juu ya jambo hili vilitazame kwa ukaribu zaidi ili kuepuka gharama zisizositahili kwa abiria. Kwani wengi hulazimika kuunganisha magari pasipo na ulazima wa kufanya hivyo.

kweli mkuu tatizo la kukatisha ruti limekuwa sugu kana kwamba hakuna uongozi
 
saa 1 : 00 kamili usiku ukiwa mwenge kuja tegeta nauli sh 1000 wananchi walishazoea hali hii
 
Daladala ni huduma ya kijamii ambayo kitaratibu ilitakiwa kutolewa na serikali
Hivyo kupunguza kupanda kwa garama wangeziondolea ushuru
Pia wangeondoa VAT unapoingiza daladala
Huduma wanayo toa inasukum$a mbele taifa kwa watu kuwahi $akazini na shule

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
saa 1 : 00 kamili usiku ukiwa mwenge kuja tegeta nauli sh 1000 wananchi walishazoea hali hii
basat tuendelee na utaratibu huo?
unaddhani ni wananchi wote wanamudu bei hiyo?
jaribu kupita kilwa rd nyakati za jioni utaona watu wengi wakitembea kwa mguu kuanzia maeneo ya kamata, puma energe mpaka mivinjeni na kuendelea, watu wengi wanatembea , sijui ni ugumu wa maisha au ni gharama za nauli?
 
Last edited by a moderator:
basat tuendelee na utaratibu huo?
unaddhani ni wananchi wote wanamudu bei hiyo?
jaribu kupita kilwa rd nyakati za jioni utaona watu wengi wakitembea kwa mguu kuanzia maeneo ya kamata, puma energe mpaka mivinjeni na kuendelea, watu wengi wanatembea , sijui ni ugumu wa maisha au ni gharama za nauli?
wabongo mmezoea kulalamika vitu vingi tu vinapanda kiholela lakini shilingi mia tu mnaongea sana maisha bora hayapatikani kwenye nauli leo ving'amuzi hamuongelei vimepanda hachana na serikali ya ccm ndio dawa
 
Last edited by a moderator:
wabongo mmezoea kulalamika vitu vingi tu vinapanda kiholela lakini shilingi mia tu mnaongea sana maisha bora hayapatikani kwenye nauli leo ving'amuzi hamuongelei vimepanda hachana na serikali ya ccm ndio dawa

vipi kaka mwenzetu unatoka nchi gani?
kama wewe ukikaa kimya nani atasema, mabadiliko yanaanza na wewe ndugu.
 
basat tuendelee na utaratibu huo?
unaddhani ni wananchi wote wanamudu bei hiyo?
jaribu kupita kilwa rd nyakati za jioni utaona watu wengi wakitembea kwa mguu kuanzia maeneo ya kamata, puma energe mpaka mivinjeni na kuendelea, watu wengi wanatembea , sijui ni ugumu wa maisha au ni gharama za nauli?
kama hawamudu mbona wanatoa? utaratibu huo ambao si rasmi umewekwa na wafanyabiashara na wananchi wanakosa umoja na kuwa na msimamo.
 
Last edited by a moderator:
vipi kaka mwenzetu unatoka nchi gani?
kama wewe ukikaa kimya nani atasema, mabadiliko yanaanza na wewe ndugu.
sio nauli mkuu huku vijini kwa umbali wa mbagala to mwengi ni km 18 kwa huku kijijini ni sh 1500 we wa mjini unalia je wa kijijini afanye nini? Hizo siasa za maneno tu je wewe ungekuwa na daladala utafanya nini wakati vyakula na bia vinapanda bei kila siku wabongo hawaongei na bar mnajaa lakini nauli mnaongea! Acheni hizo angalieni mmejikwaa wapi?
 
Back
Top Bottom