Natokwa Damu Ukeni Na sio Hedhi

Sawa... ntamuona Dr
Nahitaji kuandika ila naona nimetingwa kidogo, kwa ufupi nenda hospitalini ukafanyie physical examination kwa kutumia vaginoscopy ambao dakatari atachunguza kama kuna mabadiliko yoyote katika cervix, au kuta za uke wako na kama atakuta kuna mabadiliko basi itambidi achukue sampuli kidogo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Naomba niandike kwa undani zaidi kwa hapo baadae maana kuna kazi imenitinga kidogo hapa mkuu.

Ila kwa dalili za mwanzo hapo inaweza kuwa una tatizo au unaelekea kupata cervical cancer.
 
Pole sana binti, kwa maelezo yako nahisi hiyo ni moja ya dalili za saratani ya shingo ya kizazi.
Kumbuka saratani ya shingo ya kizazi yaweza kutibika iwapo itagundulika mapema.PAP TEST (PAPANICOLAOUS TEST);Pap-Smear ni test ambayo hutumika kuchunguza mabadiliko ya chembe zilizoko katika mlango wa kizazi ili kugundua mabadiliko yanayotokea katika chembe hizo na hivyo kuwahi kuyakabili mapema.
mnanitisha jmn... Cancer tena
 
Ahsante sana
Hatukutishi mkuu, hiya nimeyajibu kutokana na maelekezo uliyo yatowa pale mwanzoni.
Na pia yaweza kuwa ni hisia tu mkuu, hiyo haupaswi kuogopa zaidi nakushauri uende hospital ili ukapate uhakika kutoka kwa wataalamu.
Pia nahisi tiba na vipimo vya saratani ya shingo ya uzazi hutolewa bure kabisa.
 
Haya, ebu elezea pia kuhusu hiyo picha nilio iambatanisha hapo chini tafadhali....
IMG_20190902_092018_095.jpeg
 
Don't google your symptoms , please go to hospital for right check up and treatment.

Thank me later.
 
Kijana fuata ushauri huu wa mdau hapa chini...

Usiache kumwambia msichana wako afanyiwe physical examination haswa ya ndani ya via vyake vya uzazi...

Nahitaji kuandika ila naona nimetingwa kidogo, kwa ufupi nenda hospitalini ukafanyie physical examination kwa kutumia vaginoscopy ambao dakatari atachunguza kama kuna mabadiliko yoyote katika cervix, au kuta za uke wako na kama atakuta kuna mabadiliko basi itambidi achukue sampuli kidogo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Naomba niandike kwa undani zaidi kwa hapo baadae maana kuna kazi imenitinga kidogo hapa mkuu.

Ila kwa dalili za mwanzo hapo inaweza kuwa una tatizo au unaelekea kupata cervical cancer.
 
hapana,
Damu ya kawaida ila nyepesi
Hapo shida yako inaweza kuwa imesababishwa na vitu vingi..
Ungeenda hospitali ukafanye vipimo kama utrasound ,ukafanye screening ya kansa ya mlango wa kizazi...

Kama damu inatoka nyingi fanya uende leo leo ili wakupe vidonge vya kukata damu usijepata anemia..

NB. Usiende hoaptali ndogo utapotezewa muda bure..
MUHIMU ZAIDI... pima mimba kwanza
Inawezekana ikawa ni abortion tu
 
Unatumia vidonge vya uzazi wa mpango??
Damu inatoka ya rangi gani? Kuna mabonge?
Je kama angetumia hizo dawa za kupanga uzazi kutoka damu kama hivyo ni kawaida? Isingekua na uhusiano na hiyo cervical cancer wanayo iongelea wadau? Kuna mtu nimekutana nae anashida kama ya mleta mada..
 
Je kama angetumia hizo dawa za kupanga uzazi kutoka damu kama hivyo ni kawaida? Isingekua na uhusiano na hiyo cervical cancer wanayo iongelea wadau? Kuna mtu nimekutana nae anashida kama ya mleta mada..
Damu kutoka ukeni kama sio hedhi SIO kawaida.
Lakini dawa za uzazi wa mpango husababisha mzunguko wa hedhi unakuwa haueleweki (irregular) sababu dawa zile zinafanya kazi kwenye hormone zinazocontrol mzunguko wa hedhi kwahio mtu anaweza kutoka damu katikati ya mzunguko..
Hii inaweza kuwa moja ya sababu..
Lakini kuna sababu nyingi tu za mtu kutoka damu ukeni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom