Natamani Hiki Nachokiwaza Kitimie!!

Natamani Hiki Nachokiwaza Kitimie!!

sembo

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
4,350
Reaction score
3,451
1. NMB inasitisha mkataba wake wa "vijisenti kadhaa" katika timu ya Azam FC. Wanainunua Ndanda FC, wanaibadili na kuwa NMB FC na kuwekeza mabilion.. Hii inawatangaza vyema, hadi kuwa the leading bank in EAC.

2. Bilionea wa Kihaya Rugemalira anaanzisha timu, anawekeza mara 5 ya hela alizompa prof. tibaijuka [zaidi 9 Bilion].. Hii inamtangaza vyema na anapata madili ya kuzalisha umeme nchi mbali mbali..

3. Serikali kupitia makampuni yake inagutuka na kuanzisha timu za soka, ambazo zinahamasisha raia kuhusu mambo mbali mbali.. Mf. mwaka 2015 akisoma bajeti, Mwigulu anadai mapato yameongezeka mara 4. Hii ni baada ya TRA FC kuwahamasisha raia..

Nadhani sasa imefika mda katika ligi yetu tuwe na timu kama;
1. Mkombozi Bank FC
2. TRA FC
3. VIP Engineering SC
4. NMB FC
5. Tatu Bomba FC
6. Konyagi SC [ikianzishwa hii nahama Simba Sc..hehe] n.k

Hizi timu zitaleta changamoto kubwa katika ligi yetu tofauti na hii mitimu ya majeshi.

NB: Hongera Azam FC, Kagera / Mtibwa Sugar na Mwadui FC kwa mnayoyafanya.
 
Mawazo yako ni mazuri...sijui una umri gani maana unachowaza ni kitu ambacho kilikuwepo huko nyuma. ...mashirika na makampuni yote makubwa pamoja na wizara za serikali zilishawahi kuwa na team za mpira wa miguu, netball na michezo mingi tuu. ...lilipoanza wimbi la upunguzaji wafanyakazi na ubinafsishaji ndio ukawa mwisho wa hizi team
 
Mawazo yako ni mazuri...sijui una umri gani maana unachowaza ni kitu ambacho kilikuwepo huko nyuma. ...mashirika na makampuni yote makubwa pamoja na wizara za serikali zilishawahi kuwa na team za mpira wa miguu, netball na michezo mingi tuu. ...lilipoanza wimbi la upunguzaji wafanyakazi na ubinafsishaji ndio ukawa mwisho wa hizi team

Mkuu mi sio wa kile kizazi kilichoshuhudia timu ya tukuyu ikipanda ligi kuu na kuchukua ubingwa, au kipindi cha timu za bandari, sigara, pamba, reli zikiwatesa simba na yanga. Nadhani sasa ni mda muafaka wa kuzirudisha hizo timu. Pia ni vyema tukawapa sapoti watu binafsi wanaowekeza nguvu na mali zao katika soka. Mfano Kajumulo au zayumba (mmiliki wa african lyon) walikuja vizuri sana, ila fitina zikawaondoa mchezoni na sasa hawajulikana wako wapi.
 
Mkuu mi sio wa kile kizazi kilichoshuhudia timu ya tukuyu ikipanda ligi kuu na kuchukua ubingwa, au kipindi cha timu za bandari, sigara, pamba, reli zikiwatesa simba na yanga. Nadhani sasa ni mda muafaka wa kuzirudisha hizo timu. Pia ni vyema tukawapa sapoti watu binafsi wanaowekeza nguvu na mali zao katika soka. Mfano Kajumulo au zayumba (mmiliki wa african lyon) walikuja vizuri sana, ila fitina zikawaondoa mchezoni na sasa hawajulikana wako wapi.

Hizo Fitina Ndizo Zilizofikisha Soka Letu Hapa Lilipo, Hayo Mambo Yanafanyika Kwa Wapenda Soka Sio Kwa Mafisadi Wa Nchi Hii.
 
Ongezea na hii:
natamani barabara ya msimbazi ipanuliwe mita 20 kuanzia mwisho wa barabara.
 
1. NMB inasitisha mkataba wake wa "vijisenti kadhaa" katika timu ya Azam FC. Wanainunua Ndanda FC, wanaibadili na kuwa NMB FC na kuwekeza mabilion.. Hii inawatangaza vyema, hadi kuwa the leading bank in EAC.

2. Bilionea wa Kihaya Rugemalira anaanzisha timu, anawekeza mara 5 ya hela alizompa prof. tibaijuka [zaidi 9 Bilion].. Hii inamtangaza vyema na anapata madili ya kuzalisha umeme nchi mbali mbali..

3. Serikali kupitia makampuni yake inagutuka na kuanzisha timu za soka, ambazo zinahamasisha raia kuhusu mambo mbali mbali.. Mf. mwaka 2015 akisoma bajeti, Mwigulu anadai mapato yameongezeka mara 4. Hii ni baada ya TRA FC kuwahamasisha raia..

Nadhani sasa imefika mda katika ligi yetu tuwe na timu kama;
1. Mkombozi Bank FC
2. TRA FC
3. VIP Engineering SC
4. NMB FC
5. Tatu Bomba FC
6. Konyagi SC [ikianzishwa hii nahama Simba Sc..hehe] n.k

Hizi timu zitaleta changamoto kubwa katika ligi yetu tofauti na hii mitimu ya majeshi.

NB: Hongera Azam FC, Kagera / Mtibwa Sugar na Mwadui FC kwa mnayoyafanya.

Hizi ndoto za bia ni shida
 
Mkuu Sembo umeisahau Panone FC, Mbeya City
 
Hapana mi natamani kila mkoa ungekuwa na timu ya mpira....hizo kampuni ziwe sponsors tu!!!
 
Back
Top Bottom