kabiriga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 1,163
- 1,213
Nimekuwa naonana nae kwenye mizunguko yangu hapa na pale,na kila nikikutana nae hapendi kunisalimia kwambali atasogea napengine tutapeana mikono na kuulizana nambo mawili matatu na ata akiwa ng'ambo ya barabara atanisihi nisubiri avuke ilimradi tumesalimiana kwa karibu.Juzi wakati nipo kwenye foleni ktk benki moja mjini kwetu nilimkuta pia akiwa mbele yangu kama mtu wa tano hivi alipogeuka na kuniona akatoka kule alikokuwa na kurudi nyuma nilikokuwa pamoja na kusalimiana aliniambia kuwa akitoka atanisubiri nje anamazungungumuzo nami.tulipotoka tulisogea kama hatua miambili hivi ,akaaza kwa kuniomba samahani kwa kuchelewesha muda wangu kisha sikukudhani kama angalisema haya."unajua kaka nakupenda na nimelazimika kukwambia ukweli kwani nimeona nateseka kila nikikuona".nilipigwa na butwaa kisha nikamwambia kuwa mimi nina mchumba haiwezekani nikaanzisha mahusiano nae kwa sasa.ndipo akasema haidhuru "naomba basi nizae nawewe".sikuwa namajibu ya haraka ndipo nilipomwambia kuwa haiwezekani bado aliendelea kusisitiza nifikilie vizuri kisha nimpe jibu.Waungwana naomba ushahuri wenu.