Natafuta mteja wa kuku chotara Sasso

Natafuta mteja wa kuku chotara Sasso

sisame

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2016
Posts
365
Reaction score
321
Wanajamvi salamu!
Mimi ni mfugaji mdogo, nipo Morogoro.
Naanza kwa kumtambulisha Sasso kwa ufupi; Sasso ni kuku chotara wa nyama asili yake ufaransa, na hutokana na jamii ya broiler. Ni kuku anaejaza nyama sana.
Najipanga kuzalisha Sasso kati ya 200 na 300 kila mwezi, wakiwa na umri wa miezi mitatu, kwa matumizi ya nyama. Hivyo natafuta mteja ambae tutaweza kuingia mkataba nikamzalishia kwa ubora wa hali ya juu na kumpelekea kwa bei tutakayokubaliana
Pia naombeni michango yenu namna ya kuingia sokoni!! Nipo tayari kuzalisha hata nikipata mteja wa kuku hamsini kila wiki ninamudu.
Karibuni wanajamvi!
 
hao wapo kujaza nyama wakimaliza wapige picha
 
Kapicha basi tuwaone walivyojaa nyama maana sikuhizi sura hata mbuzi anayo tatizo ni .........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom