Wakati ukisubiri kupata kazi, nina hakika ukiamua unaweza pata 50,000. Endapo ungeahidiwa kwenda interview mkoa tofauti na uliopo bila shaka ungetafuta nauli yenye thamani zaidi hata ya 50,000 popote na ukaipata.
Sasa basi, hiyo 50,000 hapo ulipo fanya hivi. Tafuta kijana asiye na kazi wa mtaani. Mnunulie jiko la kuchomea mahindi, mkaa, kiti na mahindi ya kuanzia angalau 50 hivi.
Mahindi mabichi 50 = 250x50 = 12500/=
Jiko la kuchomea mahindi na mkaa wa kuanzia 20,000/=
Kiti cha kukalia cha Plastic 13,000/=
Hivyo 12,500+20,000+13,000= 45,500.
50,000 -45,500 = 4500
Hiyo 4500 utaitumia kama nauli ya kuafatilia mahindi.
Mauzo..
Day 1
Mahindi 50 x 500 = 25,000
Siku ya kwanza wewe na kijana msichukue faida yoyote.
Siku ya pili ongeza kiasi cha Mahindi na kufikia 80 yenye gharama ya 20,000. Inayobakia nunua Mkaa na usafiri.
Siku hiyo mtauza mahindi 80x500 = 40,000/=..
Siku ya tatu muwe na target ya kuuza mahindi 100 x500 =50,000 ambayo ndiyo itakayokuwa target yenu ya kila siku.
Kwa mauzo ya gross profit ya 50,000 kwa siku mkitoa gharama za uendeshaji mnaweza kubakia na 20,000 kama net profit. Hapo mkigawana kila mmoja ni sawa na 10,000 x30 @ mwezi ni sawa na 300,000.
300,000 x vijiwe vitatu mjini una profit ya 900,000 ambayo ni sawa na mshahara wa mtumishi Serikalini mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 6 au 9 kazini.
MUHIMU: Kufanikiwa si rahisi sana kama nilivoonesha hapo juu, lakini kila aliyefanikiwa alianza kwa mipango ya mezani kama nilivyoonesha hapo juu.
Kila la kheri mkuu.!