Natafuta chumba cha kupanga DAR

PSPA Pure'12 udsm

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2013
Posts
834
Reaction score
450
Wanajamvi Heshima Mbele!

Nafanya kazi maeneo ya Mikocheni.

Natafuta chumba cha kuishi maeneo jirani kama vile Mwenge, Kawe, Kijitonyama, Kinondoni,Sinza, Magomeni, mbezi beach. Au sehem ambapo nitapata usafiri wa moja kwa moja hadi kazini kwangu.

Chumba kiwe na umeme na maji au km maji hamna yawe yanapatikana jirani.
Sio lazima kiwe self -contained.

Bei ni 25,000/= hadi 30,000!

Kwa mwenye Taarifa tuwasiliane kupitia 0718-257680.
 
Hizo sehemu ulizotaja na hy pesa..mh labda mabondeni au nyumba choka. Mbaya.Kama hy bajeti ni fixed jaribu maeneo ya Mbagala,Gongo la mboto, Kimara, Banana na sehemu za mbali kidogo.
 

hiyo bei ndugu!!! Umetoka mkoa gani kwani?
 

baba jipange upya ndo uje dar.
 
Mwambieni ajipange kwa sh ngap siyo kumzodoa. Msaidieni
 
mwananyamala utapata nadhani
 
Mbona mmeshtuka wadau, vyumba bei maeneo hayo
 
GREAT THINKER jaribu kuwa wastaarabu basi pale mtu anapohitaji kitu mfahamisheni kwa usahihi na sio kumkejeli. Si kila kitu unazaliwa unakijua!
 
GREAT THINKER jaribu kuwa wastaarabu basi pale mtu anapohitaji kitu mfahamisheni kwa usahihi na sio kumkejeli. Si kila kitu unazaliwa unakijua!

ok. ni hivi, hayo maeneo uliyoyataja kuwa unataka chumba ni Prime Areas za Dar.

Pia, kwa hivyo vigezo ulivyosema ni vigumu kupata kwa bei ya 30,000 kwa mwezi. hata huku tabata hupati. Jipange mkuu at least kuanzia elfu 70 na zaidi.
 
ushauri..kwa kawe unapata kaka angu ila kwa mikocheni kisichoself tu kinaanzia 50
 
Hizo sehemu ulizotaja na hy pesa..mh labda mabondeni au nyumba choka. Mbaya.Kama hy bajeti ni fixed jaribu maeneo ya Mbagala,Gongo la mboto, Kimara, Banana na sehemu za mbali kidogo.

acha wehu...kimara unailinganisha na mbagala?...hiyo cash aliyonayo aje kwenu mikocheni chama uswahilini kwa wauza gongo
 

Mkuu hiyo hela na hayo maeneo aisee nakuonea huruma czan km utapata chumba kizuri,ata km utapata unaweza ukahama kwa kero
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…