Nape, muungwana akivuliwa nguo huchutama

nguruka wa kig0ma

JF-Expert Member
Jan 16, 2020
2,946
2,929
Nilikusikia ukijibu hoja ya Dkt Albanie alipokutaka uwaombe radhi Watanzania kwa kuwafungia bunge live.

Ulikataa kwa hoja za kisiasa sana.
Kumbuka watanzania walilalamikia jambo hili na kukulalamikia Sana.
Wakati ule uliziba masikio kwakuwa ulijiona upo salama kwa kuwa ulikuwa mikononi mwa Magufuli.

Kama kila kitabu na zama zake, basi tambua hii siyo zama za Magufuli tena.
Waombe radhi watanzania hutakuwa umekosea, badala yake utakuwa umejiweka ktk nafasi nzuri hata kwa utawala huu.

Mbona ulitembelea magoti kuomba msamaha tena na machizi kwa mwenda zake, au uliogopa kupotezwa?

Nilivyomuelewa Rais huyu hahitaji kusifiwa,kupambwa na kutukuzwa kama mlivyomfanyia mwendazake,bali anataka unyenyekevu kwa mnaowatumikia na uchapaji kazi.

OMBA RADHI BILA KUJALI NANI ALISHIRIKI KTK HILO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom