Chakwale
JF-Expert Member
- May 17, 2015
- 1,086
- 1,601
Wakuu habari..
Kama kichwa cha habari hapo kinavyojieleza, karibu mwezi mzima sasa nimekuwa nikiota nakula chakula ndotoni na watu mbalimbali ninao wafahamu na nisiowafahamu.
Hali hiyo inanikera sana mana ukiamka asubuhi tumbo linakuwa limejaa then linakuwa kama MTU mwenye gas tumboni hata kama Jana yake usiku niwe nimelalia chai na kipande kidogo tu cha mkate.
Kingine ni kwamba nalala saana na hata nikiamka bado nakuwa mzito kuamka mwili bado unataka kubaki kitandani tofauti kabisa na mwanzo.yaan ningekuwa KE unaweza sema labda ukapime ujauzito.
Hali hii ya kuota ota ndoto za kula chakula sijui nalishwa usiku inanikosesha raha,na hivi mambo yangu hayaendi naanza kuihusisha hali hii na mambo yangu ya kipato na kiuchumi kwenda mrama.Kama kuna yeyote ameshawahi kutana na hali kama hii alikabiliana nayo VP ili kuitatua mana naona naanza kupata fikra za kishirikina sasa,ukimjulisha na sisimizi kibao wasiotaka kuondoka nymbani kwangu hata ukiwawekewa dawa za kuwauwa or kuwamwagia maji,basi imani ya mambo ya kishirikina inaongezeka.
Nakumbuka Marehem Bibi yangu nilipokuwa Mdogo aliwahi kuniambia ukiona kwako or mtaani kuna sisimizi wengi ujue hiyo ni ishara ya mwaka huo kuwa na njaa,sasa napata kigagaziko nikiunga dots za matukio.
Kwa vile humu ni kisiwa cha Maarifa na kuna wakubwa,najua ntapata Elimu ya kunisaidia iwe ya Kisayansi, Kimila,Kidini, Kiganga nk kuwa inapotokea hali kama hiyo unatakiwa ufanyaje.
Asante...
Kama kichwa cha habari hapo kinavyojieleza, karibu mwezi mzima sasa nimekuwa nikiota nakula chakula ndotoni na watu mbalimbali ninao wafahamu na nisiowafahamu.
Hali hiyo inanikera sana mana ukiamka asubuhi tumbo linakuwa limejaa then linakuwa kama MTU mwenye gas tumboni hata kama Jana yake usiku niwe nimelalia chai na kipande kidogo tu cha mkate.
Kingine ni kwamba nalala saana na hata nikiamka bado nakuwa mzito kuamka mwili bado unataka kubaki kitandani tofauti kabisa na mwanzo.yaan ningekuwa KE unaweza sema labda ukapime ujauzito.
Hali hii ya kuota ota ndoto za kula chakula sijui nalishwa usiku inanikosesha raha,na hivi mambo yangu hayaendi naanza kuihusisha hali hii na mambo yangu ya kipato na kiuchumi kwenda mrama.Kama kuna yeyote ameshawahi kutana na hali kama hii alikabiliana nayo VP ili kuitatua mana naona naanza kupata fikra za kishirikina sasa,ukimjulisha na sisimizi kibao wasiotaka kuondoka nymbani kwangu hata ukiwawekewa dawa za kuwauwa or kuwamwagia maji,basi imani ya mambo ya kishirikina inaongezeka.
Nakumbuka Marehem Bibi yangu nilipokuwa Mdogo aliwahi kuniambia ukiona kwako or mtaani kuna sisimizi wengi ujue hiyo ni ishara ya mwaka huo kuwa na njaa,sasa napata kigagaziko nikiunga dots za matukio.
Kwa vile humu ni kisiwa cha Maarifa na kuna wakubwa,najua ntapata Elimu ya kunisaidia iwe ya Kisayansi, Kimila,Kidini, Kiganga nk kuwa inapotokea hali kama hiyo unatakiwa ufanyaje.
Asante...
