Vox Populi Vox Dei
Member
- Jun 30, 2013
- 21
- 14
Ndugu zangu wana JF, mimi ni Mwalimu Idara ya Sekondari katika Wilaya X.Tarehe 20 Januari 2014 nilichaguliwa kwa kura nyingi kuwa mwakilishi wa Chama cha Walimu idara ya Sekondari Wilaya katika uchaguzi wa kuziba nafasi zilizokuwa zimeachwa wazi.
Tangu siku hiyo ya uchaguzi sijawahi kushirikishwa katika shughuli yoyote ile ya chama ikiwa ni pamoja na kuambiwa majukumu na mipaka yangu ya kazi hiyo ya uwakilishi,sijui nianzie wapi na niishie wapi katika kuwawakilisha wapiga kura wangu katika chama hicho cha walimu.
Chama kiko mikononi mwa watu watatu tu ambao ni Katibu wa Wilaya,Mwenyekiti na Mhazini.
Je Wana jf,katika mazingira kama haya kuna sababu yoyote ya mimi kuendelea na nafasi hiyo ilhali siitendei haki? Naombeni ushauri wenu!
Tangu siku hiyo ya uchaguzi sijawahi kushirikishwa katika shughuli yoyote ile ya chama ikiwa ni pamoja na kuambiwa majukumu na mipaka yangu ya kazi hiyo ya uwakilishi,sijui nianzie wapi na niishie wapi katika kuwawakilisha wapiga kura wangu katika chama hicho cha walimu.
Chama kiko mikononi mwa watu watatu tu ambao ni Katibu wa Wilaya,Mwenyekiti na Mhazini.
Je Wana jf,katika mazingira kama haya kuna sababu yoyote ya mimi kuendelea na nafasi hiyo ilhali siitendei haki? Naombeni ushauri wenu!