KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
Kipindi cha siku za usoni kati ya mwaka 2004 na5 niliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na dada mmoja lakini baadae baada ya kumgundua ni mbwa mwitu aliyejitanda ngozi ya kondoo niliamua kuachana naye.Kwa ujumla tabia yake ilikuwa mbaya!!!!!. Kwa sasa ninaye mpenzi wangu ninayempenda sana anayejiheshimu na tunathaminiana.Hivyo basi ktk hali isiyokuwa ya kawaida kwa siku chache zilizopita nimegundua kuwa mpenzi wangu huyu wa sasa ameanza urafiki na yule dada tuliyeachana naye hapo awali.Nikizikumbuka tabia za awali za yule dada zisizokuwa na chembe ya staha nipo tayari kuachana na huyu mpenzi wangu endapo nitakapomweleza juu ya urafiki wao asikubali kuachana naye. NAOMBA nieleweke wazi kuwa simkatalii urafiki wake na huyo dada kwa sababu niliwahi kuwa naye la hasha!!!!!!