Naomba ushauri

Naomba ushauri

dontgiveup

Member
Joined
Nov 10, 2014
Posts
22
Reaction score
5
Habari wana JamiiForums. Nina mchumba mwanajeshi ambaye kwa sasa yupo mkoa tofauti na mimi.

Uchumba wetu una miaka miwili sasa.

Mwanzoni tulikuwa tunawasiliana vizuri lakini ghafla mawasiliano yakawa magumu kwa upande wake, kwani wakati mwingine nikimpigia simu hapokei na nikimtumia meseji anajibu kwa wakati anaojisikia yeye.

Nikimuuliza kwa nini anafanya hivyo anajibu kuwa yupo bize na kazi, na ninapomuuliza kuhusu hatima ya mahusiano yetu, ananiambia kuwa yeye bado ananipenda na anachofahamu ni kwamaba mimi ndo mkewe na kwamba mwezi Disemba mwaka huu anakuja ili akamalishe taratibu za ndoa.

Lakini kinachonipa wasiwasi kwake ni suala la mawasiliano kwani naweza nikimpigia simu huwa anapokea kwa nadra sana na mara nyingi mpaka nianze mimi kumtafuta kwenye simu.

Je huyu mtu yuko serious kweli?

Nahitaji ushauri wenu tafadhali.
 
Hivi wana MMU kuna ile sheria ya mwanajeshi kutokuoa miaka 6 (kama sikosei) ya mwanzo wa ajira, bado inatumika?
 
Hivi wana MMU kuna ile sheria ya mwanajeshi kutokuoa miaka 6 (kama sikosei) ya mwanzo wa ajira, bado inatumika?

nadhani ipo bado mana mimi binafsi nilitaka kwenda jeshi.....nikaambiwa hakuna kuoa wala kuolewa mpaka baada ya miaka 5......
 
Hivi wana MMU kuna ile sheria ya mwanajeshi kutokuoa miaka 6 (kama sikosei) ya mwanzo wa ajira, bado inatumika?

hyo bado ipo lakn haina mkazo sana vijana wanajichukulia kinyeji tu lakn ukioa chin ya miaka hyo mkeo anakuwa hatambuliki kisheria. Ukipata tatizo husikilizwi cos upo nje ya sheria...
 
dontgiveup kwan ww unafanya kaz gani?
Inamaana hakuna wanawake wengne mpaka ukaoe mjeshi?

Kama na ww ni askari bora kidogo lakn kama ww ni raia aiseee nakuonea huruma.
Pressure+stress+migogoro ya hapa na pale hvyo vitakuwa ndg zako...
 
Last edited by a moderator:
Habari wana jf. Nina mchumba mwanajeshi ambaye kwa sasa yupo mkoa tofauti na mimi. Uchumba wetu una miaka miwili sasa. Mwanzoni tulikuwa tunawasiliana vizuri lakini ghafla mawasiliano yakawa magumu kwa upande wake, kwani wakati mwingine nikimpigia simu hapokei na nikimtumia meseji anajibu kwa wakati anaojisikia yeye. Nikimuuliza kwa nini anafanya hivyo anajibu kuwa yupo bize na kazi, na ninapomuuliza kuhusu hatima ya mahusiano yetu, ananiambia kuwa yeye bado ananipenda na anachofahamu ni kwamaba mimi ndo mkewe na kwamba mwezi Disemba mwaka huu anakuja ili akamalishe taratibu za ndoa. Lakini kinachonipa wasiwasi kwake ni suala la mawasiliano kwani naweza nikimpigia simu huwa anapokea kwa nadra sana na mara nyingi mpaka nianze mimi kumtafuta kwenye simu. Je huyu mtu yuko serious kweli? nahitaji ushauri wenu tafadhali .


Take care na huyo mchumba wako, inawezekana kabisa kapata msichana mwingine ambaye anamkeep bize huko aliko. Wanajeshi wengi vijana ndivyo walivyo, kuna kesi nyingi za namna hii nimeishakutana nazo. Kaa chonjo ... saaa mbaya, asije akkauletea magonjwa......

Kaa kimya, usimtafute kabisa.... Ukion na yeye ametulia hakutafuti, wiki 2, 3, mwezi 1, 2 ... nk. basi jua huna mchumba hapo... tafuta anayekufaaa
 
Habari wana jf. Nina mchumba mwanajeshi ambaye kwa sasa yupo mkoa tofauti na mimi. Uchumba wetu una miaka miwili sasa. Mwanzoni tulikuwa tunawasiliana vizuri lakini ghafla mawasiliano yakawa magumu kwa upande wake, kwani wakati mwingine nikimpigia simu hapokei na nikimtumia meseji anajibu kwa wakati anaojisikia yeye. Nikimuuliza kwa nini anafanya hivyo anajibu kuwa yupo bize na kazi, na ninapomuuliza kuhusu hatima ya mahusiano yetu, ananiambia kuwa yeye bado ananipenda na anachofahamu ni kwamaba mimi ndo mkewe na kwamba mwezi Disemba mwaka huu anakuja ili akamalishe taratibu za ndoa. Lakini kinachonipa wasiwasi kwake ni suala la mawasiliano kwani naweza nikimpigia simu huwa anapokea kwa nadra sana na mara nyingi mpaka nianze mimi kumtafuta kwenye simu. Je huyu mtu yuko serious kweli? nahitaji ushauri wenu tafadhali .

Mawasiliano ni kitu cha muhimu katika mahusiano yeyote, lakini pia hutegemea jinsi mlivyoweka msingi wa mawasiliano yenu, lakini pamoja na hili baadhi ya kazi ni changamoto kimawasiliano( kazi zinazohusiana na ulinzi, afya, n.k).

Iwapo amesema mwenyewe mwezi "disemba" mwaka huu atakuja kufanya taratibu hizo kwanini uwe na hofu, zimebaki siku takribani tatu tu ili kufika mwezi huo ' mchumba' wako aliokuahidi. Inawezeka haikuwa kama zamani lakini kama umevumilia kwa takribani miaka miwili sidhani kama utadhindwa kwa siku chache zilizobaki, angalau kuonana ana kwa ana na kuzungumza.
 
Hapo ni sawa na hujaoa kabisa!!Hii sheria huwa inawaumiza wengi maana unakuta mtu amempromise mwenzie lakini mtu kukaa anasubiri miaka yote hiyo kwa sasa ni ngumu
 
Mwezi Dedemba si ni wiki ijayo.msubiri aje mzungumze ana kwa ana uajua ana mawazo gani!Kuwa na mpenzi mwanajeshi inabidi uvumilie maana wana sheria zinazowabana wakati mwingine.
Kumbuka MVUMILIVU HULA MBIVU..........Lakini usivumilie sana mpaka zikaoza!
 
dontgiveup kwan ww unafanya kaz gani?
Inamaana hakuna wanawake wengne mpaka ukaoe mjeshi?

Kama na ww ni askari bora kidogo lakn kama ww ni raia aiseee nakuonea huruma.
Pressure+stress+migogoro ya hapa na pale hvyo vitakuwa ndg zako...

huyu ni msichana
 
Last edited by a moderator:
Pole sana unajua mahusiano ya mbali kinachokibeba ni mawasiliano yakiwa hafifu lazima penz litayumba Inawezekana akawa mume wa mtu huyo ila yote kwa yote vunja ukimya zungumza nae kwa mara ya mwisho halaf kaa kimya umuone atajibuje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom