Mimi ni kijana niliyehitimu masomo yangu ya chuo kikuu mwaka huu nina umri wa miaka 24, wakati nikiwa chuo nilibahatika kukutana na wasichana wawili wazuri sana ambao kwa nyakati tofauti niliweza kuwaeleza hisia zangu kwao. Niliwa bado chuon mmoja alinikubalia na tukaanza uhusiano ila baada ya muda nilihisi ananisaliti na nilifuatilia nikagundua kuwa ni kweli nilipomweleza aliniomba msamaha na kutokana na uzuri wake na namna nilivyokuwa nimemtambulisha kwa marafiki zangu sikuweza kumuacha nililazimika kendelea naye. Ila toka hiyo hali hiyo itokee hisia zangu kwake zilipungua sana na niliamua kumuacha ila alikuwa akilia sana na kunisisitiza kuwa nisimwache kutokana na roho ya huruma niliendelea kuwa naye ila sina hisia naye hata kidogo ingawa ni mzuri sana na anaonesha kunipenda sana.
Kwa upande wa huyu mwingine alipomaliza shahada yake ya kwanza alijiunga na masters na tuliendelea kuwa marafiki kama kawaida na tulifika hatua ya kuelezana hadi baadhi ya siri zetu, na huwa aliyokea kuniamini sana, kama ilivyokawaida nilijaribu kujieleza hisia nilizonazo kwake na alinikatalia kwa kigezo kuwa yupo na mchumba wake, sikuchoka kumsisitiza ila kinachoniumiza ni kuwa nampenda sana huyu dada wa pili ila nikimtumia SMS huwa hajibu nikimpigia simu akipokea huwa haongei sana, nimejaribu kutumia kila njia nimeahindwa ila nampenda sana, naombeni wana jf nifanye nini jamani nakosa raha kabisa. Huyu niliyemtongoza na akanikubalia yeye ananipenda sana ila mimi sina hisia kwake, but huyu wa pili anayesoma masters yeye kwa miaka mitatu yote niliyokuwa nilimtongoza ananikatalia ila nampenda sana na huwa nakosa raha kwa kuwaza namna ya kumpata. Naomba mnisaidie plz.
Kwa upande wa huyu mwingine alipomaliza shahada yake ya kwanza alijiunga na masters na tuliendelea kuwa marafiki kama kawaida na tulifika hatua ya kuelezana hadi baadhi ya siri zetu, na huwa aliyokea kuniamini sana, kama ilivyokawaida nilijaribu kujieleza hisia nilizonazo kwake na alinikatalia kwa kigezo kuwa yupo na mchumba wake, sikuchoka kumsisitiza ila kinachoniumiza ni kuwa nampenda sana huyu dada wa pili ila nikimtumia SMS huwa hajibu nikimpigia simu akipokea huwa haongei sana, nimejaribu kutumia kila njia nimeahindwa ila nampenda sana, naombeni wana jf nifanye nini jamani nakosa raha kabisa. Huyu niliyemtongoza na akanikubalia yeye ananipenda sana ila mimi sina hisia kwake, but huyu wa pili anayesoma masters yeye kwa miaka mitatu yote niliyokuwa nilimtongoza ananikatalia ila nampenda sana na huwa nakosa raha kwa kuwaza namna ya kumpata. Naomba mnisaidie plz.