Naomba Mnijuze Tafadhali


MJ hao wanaotoa support na ushauri ndo wale wanaoINFLUENCE maendeleo ya wengine kwa juhudi zinazotambulika pande zote.Hii haotokei kwa bahati bali kwa juhudi za mshauri na mshauriwa.

Hawa wengine kinachojalisha ni UWEPO wao tu basi.Ye mwenyewe unaweza kuta sio mjanja kiviiile kwahiyo hawezi kua na mawazo endelezi kwa mfanyabiashara mkubwa ila uwepo wake unabadilisha kila kitu.Alafu kuna wengine wana vyote viwili....sasa hawa ndo wanaweza
kumfanya mtu atoke kwenye 0 mpaka kwenye 100 ndani ya muda mfupi.
 

Kama ni hivyo Lizzy, nadhani kungekuwa na watu matajiri sana ambao kila kitu kinawakuta nyumbani wameuchapa usingizi!!
 
Kama ni hivyo Lizzy, nadhani kungekuwa na watu matajiri sana ambao kila kitu kinawakuta nyumbani wameuchapa usingizi!!
Hahhahhaha....Mzee DC bwana!Hilo la kulala kila kitu kijilete chenyewe hata kanisani hakipo...
Swala ni kwamba baadhi ya watu wanaweza kusukuma biashara za watu zikaenda vizuri kuliko kawaida iwapo juhudi zipo kwa upande wa mwenye biashara.
 
MJ hao wanaotoa support na ushauri ndo wale wanaoINFLUENCE maendeleo ya wengine kwa juhudi zinazotambulika pande zote.Hii haotokei kwa bahati bali kwa juhudi za mshauri na mshauriwa.

hapa Lizzy nakubaliana na wewe kabisa yaani ni ukweli usiopingika. Aksante kwa kunifafanulia vizuri


.............Hapa kwenye UWEPO hapo, Lizzy hapo kwenye uwepo hapo ndipo ninapopataka mimi............kama wapo ambao kwa UWEPO wake tu kwenye maisha ya mkaka huyu, anamfanya mkaka awe tajiri, afanikiwe na kuwa njema kwenye mambo yake, je hakuna ambao UWEPO wao hufanya kinyume??
 
Mpenzi unataka mzee DC aje kunitoa nishai hapa...kwanza sio uwepo unaleta tu utajiri bila mtu kua mhangaikaji.Kinachotokea ni kwamba baraka zinamzunguka yule mtafutaji....kama ni biashara wateja wanaongezeka au mawazo mazuri ya kujiendeleza yanapatikana....kama kazi nayo inachachamaa unashangaa ulikuwa hupewi safari ila ghafla bosi amekua rafikiyo..maadui zako wanaanza kukuona kwa mwanga tofauti na mambo kama hayo.

Kinyume chake kipo sana...na watu wa aina hii maranyingi hata wenyewe unakuta wana kitu kinachowafanya wachukiwe hata na watu wasiowajua na bila sababu kabisa.Sasa na wewe ukijihusisha nao watu wanaanza kukuona tofauti...amini inatokea wala sio kidogo.Inawezekana ni laana za kifamilia zinazomfuata na kumfanya aonekane waGIZA...au mwenye/anaesambaza NEGATIVE energy kama yule rafiki yako anavyotambua.Na hawa wengine wao ni MWANGA tu...au wasambazaji wa POSITIVE energy!Popote waendapo ni kupendwa tu.. kufurahisha watu n.k. Mtu kama huyu anaweza kumfanya bosi aliyekuja na mihasira yake kazini akarelax/kuziondoa.Yani wanakufanya utake kutabasamu bila sababu!!
 


Lizzy na MJ1,

Inawezekana lakini pia kuna uwezekano wa kufanya conclusion bila kuangalia factors nyingine (tena ambazo zinaweza kuwa muhimu) ila zimefichwa/zimejificha kwenye background.

Naomba kama ingewezekana watafutwe wanawake na wanaume wa namna hiyo ili tukate mzizi wa fitna kwa kufanya randomized trial na kufikia conclusion kama kweli watu wa namna hiyo wanavuta biashara au la. Kama wanavuta basi tuwatumie kama asset ili tujikwamue na umasikini!!


Halafu wewe MJ1, kwa nini umekomalia wanawake tu wakati duniani ni wawili wawili?????

Mzee DC
 

Hahhahh....tutumie tulichonacho kupata tutakacho ehhhh?!
Ngoja nifanye kautafiti kangu mwenyewe alafu ntakuja kuwaambia!
 
Hahhahh....tutumie tulichonacho kupata tutakacho ehhhh?!
Ngoja nifanye kautafiti kangu mwenyewe alafu ntakuja kuwaambia!

Kwani wewe unaonaje? Kwa nini tuendelee kuogelea kwenye tope la umasikini wakati kuna wenzetu wachache sana wamebarikiwa kuzaliwa na nyota za mvuto/mnato kiasi cha kumwezesha mtu kuwa tajiri with little efforts?

Tuache kulia lia wakati uchumi tumeukalia. Tufanye utafiti na tukiona matokeo ni mazuri sana basi tunaanza hata ku-export hiyo bidhaa!!
 

ni kweli kabisa babu kuna factors nyingi tu ndo maana nawaomba watu waliosema wao imewatokea waje wadadavue......MTM, TF na the Boss

Hahahhahha babu mie ninasikiaga kwa wanawake tu ndo maana sehemu ya pili ya swali langu nikauliza kama na wanaume wako wa aina hii..............nijitwalie wangu fasta
 

Kabla ya kuhangaika na kujitwalia au kutwaliwa kwa nini usisumbue akili yako kuona kama P-value (ushaidi wa hiyo dhana) zinalipa?
 


Mie binafsi siamini kama kuna connection yoyote hapo, ingawa hata mie Ex-bf wangu ananisumbua akidai alivyokuwa na mie mambo yake yalikuwa shwari yaani alikuwa na bahati ya kufanikiwa mambo yake especially immedeately baada ya kukutana faragha(hope mnaelewa namaanisha nini). So anadai baada ya kuachana nami mambo yake hayafanikiwi sana
 
We Dark City,bidhaa gani unayotaka ku-export hapo?Ushindwe na ulegee tena unyong'onyee kabisa!We ungekuwa na jamaa au ndugu albino jamii ingekutenga kwani usalama nduguzo hao ungekuwa mashakani.

Mimi najaribu kulifikiria kwa upande wa pili pia,labda hawa wanaume wanataka kutumia madai yao(kuwa tunawasababishia bahati) kama njia ya kupata watakacho na si vinginevyo.Strawberry1 inabidi utafakari hiyo hoja ya x-bf wako,kwasababu experience yangu ni kwamba no need ya "kufungua mipaka ya south",hata kuwa naye tu kama close friend,cha msingi muwe in peace and harmony,yaani moyo wako usiwe na kinyongo naye.
 
Kweli sina uhakika na hili..Nadhani ni trend ya maisha tu!..wakati wa furaha, misukosuko, mafanikio, huzuni n.k.

Ambacho ninafikiriaga ni kutokumuumiza binadamu mwenzangu kiasi kwa kwamba akasononeka na hii nahisi ni mbaya. kuumiza huku ni kwa makusudi na kwa kuridhia tena bila kumjali binadamu mwenzio.
 
Mwanajamii1 kwenye mpira wa miguu kuna kitu kinaitwa 'a winning manager',kwa mfano makocha kama Ferguson na Mourinho wanajulikana kama winning Managers wakati ambapo kocha kama Wenger anaitwa a good coach but not a winning manager,na tofauti ya makocha hawa huwa inajionyesha kwenye mechi ngumu na muhimu ambapo saa ingine kina Ferguson huwa wanashinda kimiujiza na Wenger huwa anashindwa kiajabu tu. Haya mambo yapo ndo maana vijana wa kijiweni wakagundua neno 'zali'.
 
MJ1,
Kuna ukweli wa "kiimani zaidi' kwamba wapo watu wenye bahati na mikosi.Haijalishi ni mwanamke au mwanaume.Ikitokea ukakutana na mwenye bahati basi utadandia hiyo bahati. Ukikutana na yule mwenye mikosi yake ya kuzaliwa basi ndio hivyo.

Mwisho wa yote, kila mtu anatakiwa kujitahidi kuhangaika kwa juhudi. Hata ndege anayekula bila kulima ana kazi ya kufungua mdomo na kudonoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…