Naomba kuuliza

Hold on

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2023
Posts
484
Reaction score
1,130
Nauli kutoka iringa kwenda dodoma ni bei gani?
 
kuna mzigo unataka kusafirisha nini mkuu,kabla hajakupiga kizinga unataka kujihakikishia kabisa
Hapana ni mm mwenyewe tu kuna kazi naenda kufanya mikoa iyo so nataka kuandaa dodos so nauli ya hapo tu ndio sijajua ila mikoa mingine nimepata
 
Hapana ni mm mwenyewe tu kuna kazi naenda kufanya mikoa iyo so nataka kuandaa dodos so nauli ya hapo tu ndio sijajua ila mikoa mingine nimepata
Ingia LATRA.GO.TZ
Hata 20 sidhani kama inafika
 
Nauli ni 15,000/= kwa zile basi zenye injini nyuma mfano Nani Kaona, Malewa, Lwangilo, Mbutta, nk. Ila ujiandae kushinda kutwa nzima kwenye hilo gari. Yaani unapanda saa 2 asubuhi, unafika Dodoma saa 10! Maana hizo chombo kila kituo zinasimama, na hazijawahi kuwa na haraka.

Ukipanda private pale Kihesa kwa Mzee Mgaya, utalipia pia 15,000/=, na utafika mapema Dodoma. (Wastani wa masaa 3 mpaka masaa 3 na nusu hivi.)

Kwa basi kubwa nzuri kama Shabiby, basi jiandae kulipa 18,000/=. Na ukipanda hilo basi, hutaingia kwenye 18 za wale Wamasai wa Migori na Izazi! Ambao kila kituo njia nzima utawakuta wanashuka/wanapanda.
 
Asijichanganye akapanda hizo nani kaona 😂😂
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…