Naomba kazi ya kusimamia shamba

Naomba kazi ya kusimamia shamba

Bolingo Ya Telephone

Senior Member
Joined
Jun 29, 2020
Posts
114
Reaction score
119
Wakuu,

Kweli nimeamini kuishi hapa Duniani ni gharama sana inatubidi tupambane haswa ndipo mambo yasituendee kombo. Kwanza kabisa mimi bado ni kijana mdogo tu umri wangu ni kati ya 26 na 28, nimeamua kuchukua hatua hii baada ya kuona mambo hayaendi sawa kabisa.

Kwasasa nafanya kazi/sijui niite ni kibarua kwenye kampuni flani binafsi kwa mkataba ila malipo yake ni madogo sana kiasi kwamba unajikuta unapata hela ya kula tu tena kwa kuunga unga, usipopiga bajeti kali kama chenga za Pele basi utajikuta hoi kabisa.

Malipo yake ili utoboe mwezi itakubidi ujibane haswa halafu mbaya zaidi Kampuni ina masharti makali haswa huwezi kupata hata nafasi ya kusema uende ukatafute hata kibarua ya aina yoyote ufanye kwa ajili ya kujiongezea kipato cha kujikimu. Kila siku ni wewe na kazi kazi na wewe na bado huko nyumbani wanakutegemea kwakweli ni inakua vigumu mno kwa kijana kuweka akiba hata kidogo kwa ajili ya maisha yake ya baadaye tena kwa sisi vijana wa kiume kulingana na taratibu na tamaduni zetu inafika wakati itakubidi utafute mwenza kwa ajili ya kuanzisha na kujenga familia sasa kwa hali kama hii inakua ni taabu kweli kweli.

Naomba kama kuna mtu ana mpango wa kulima kilimo biashara na anahitaji mtu wa kusimamia shamba hilo na kuhakikisha shamba linakua salama basi niko tayari tuwasiliane tufanye kazi pamoja kwa makubaliano, tunaingia mkataba na ningependa kwenye mkataba wetu iwe kama ifuatavyo:-

1) Ukubali kuwa mwenyeji wangu huko
2) Unitafutie na unihakikishie mahali pa kujistiri; ukipata ka single room kadogo kabisa itapendeza zaidi ila hapa utakua unalipia kodi ya hako kageto
3) Ukubali kunilipa robo ya mapato yote yatakayopatikana kwenye mauzo ya mazao yote shambani, kwani nitakua shambani kama kibarua na wakati huo huo pia nipo kama msimamizi/muangalizi wa shamba
4) Mazao yawe ni ya muda mfupi isiyozidi miezi minne
5) Kwenye msosi nitajisimamia mwenyewe (ila ukipenda pia unaweza kunipiga tafu siku moja moja- hii ni nje ya mkataba)

Wakuu, mpaka nimeamua kuchukua hatua kama hii ya kuleta bandiko humu ni kuwa niko serious kweli kweli na haya maisha, nitafanya kazi kwa kufuata maelekezo yako.

Nitafanya kazi kwa bidii haswa ili tuweze kufanikiwa kwa pamoja kwani najua endapo nitazembea na kusababisha kufeli katika hazima yetu hiyo basi tutaumia sote haswa wewe na hata mimi kwakuwa nitakua nimechoma miezi yangu minne bila lengo kusudiwa kutimia hakika sitokubali kitu kama hicho kitokee!

Wakuu, kwa utii na unyenyekevu wa hali ya juu kwenu, naomba kama kuna aliyeguswa na bandiko hili na ana mpango kama huu basi anitafute PM ili tubadilishane mawasiliano kusudi tuweze kuwasiliana tuongee kwa mapana zaidi, ningependa tuanze msimu wa mwezi wa kumi/kilimo cha kumuagilia au hata ya kutegemea rehema za Mwenyezi Mungu pia siyo mbaya. Ahsante sana!

Kwa vijana wenzangu, najua mimi ni mmoja tu kati ya vijana maelfu kwenye Jamhuri yetu hii tukufu ya Tanzania ambao tunapitia hali kama hii ila tusife moyo/tusikate tamaa chamsingi tuendelee kuchapa kazi na tuwe waaminifu. Mtu akikupa kazi yake kuwa muaminifu kwani tabia njema ni silaha.

Tupambane haswa kwa imani iko siku kwa imani nasi tutafanikiwa tu!
 
Mkuu nimesoma bandiko lako ila kwa tabu sana, jifunze kuweka paragraph.
 
Kazi unayofanya ni ipi ? Sio lazma utaje jina la kampuni !

Huo mshahara unaouita mdogo haukutoshi Ni sh ngapi kwa mwezi ? Ili tukusaidie kimawazo !!
Kumbuka Kuna ambao hata huo mshahara mdogo hawana, shukuru kwa kidogo ulichonacho !

Jibane kula hata Mara moja kwa siku ,,,fanya servings, matumizi yasio ya lazima acha !
Mfano ;
- mademu
-pombe
- anasa /outings n.k
-mtu wa pamba kila saa
- kusaidia ndg wasio na Tija, na hawajawahi Kuna na msaada kwako

Baada ya miez sita fungua hata genge lako komaa , !!! Hili la mashambani sijui usimamiz unajidanganya, kilimo kimekengeuka Sana now days , Ni ngumu Sana kumshawishi mtu amwage hela zake huko
 
Kazi unayofanya ni ipi ? Sio lazma utaje jina la kampuni !

Huo mshahara unaouita mdogo haukutoshi Ni sh ngapi kwa mwezi ? Ili tukusaidie kimawazo !!
Kumbuka Kuna ambao hata huo mshahara mdogo hawana, shukuru kwa kidogo ulichonacho !

Jibane kula hata Mara moja kwa siku ,,,fanya servings, matumizi yasio ya lazima acha !
Mfano ;
- mademu
-pombe
- anasa /outings n.k
-mtu wa pamba kila saa
- kusaidia ndg wasio na Tija, na hawajawahi Kuna na msaada kwako


Baada ya miez sita fungua hata genge lako komaa , !!! Hili la mashambani sijui usimamiz unajidanganya, kilimo kimekengeuka Sana now days , Ni ngumu Sana kumshawishi mtu amwage hela zake huko

Nashukuru kwa ushauri wako
 
Kwa hesabu ndogo mi naona bora udundulize af uje uwekeze mwenyewe kwenye kilimo hicho.
Nnachowaza ni kuwa ili mtu akuamin na muwekeze pamoja hatamwaga mapesa mengi zaidi.
Atafanya kama kuweka m1/2/3 hivi.Sasa kwa mtaji huo mnaweza kupata faida labda ya m10(japo kilimo kwasasa ni changamoto kupata faida hiyo)
Sasa umesema faida igawanywe robo..kwo 10÷4=2.5m
Ambapo umetumia miez 4+2(mpaka kuuza mazao yote)=miez 6
Miez6÷2.5m=~4.5K
Kwo tukizingatia mambo utayopitia na faida yake(ambayo siyo uhakika) BORA UTAFUTE(SAVE) MTAJI WAKO THEN KOMAA KIVYAKO!
 
Huu Uzi naamini hakuna alowahi kulima walau eka 1! Naona tu hesabu zenu😀😀! Kwamba uwekeze 1/2m upate 10m!😀.Mtoa mada usijaribu kulima..kilimo kinataka hela nzuri siyo ya mawazo. ! Utajuta!
 
Kwa hesabu ndogo mi naona bora udundulize af uje uwekeze mwenyewe kwenye kilimo hicho.
Nnachowaza ni kuwa ili mtu akuamin na muwekeze pamoja hatamwaga mapesa mengi zaidi.
Atafanya kama kuweka m1/2/3 hivi.Sasa kwa mtaji huo mnaweza kupata faida labda ya m10(japo kilimo kwasasa ni changamoto kupata faida hiyo)
Sasa umesema faida igawanywe robo..kwo 10÷4=2.5m
Ambapo umetumia miez 4+2(mpaka kuuza mazao yote)=miez 6
Miez6÷2.5m=~4.5K
Kwo tukizingatia mambo utayopitia na faida yake(ambayo siyo uhakika) BORA UTAFUTE(SAVE) MTAJI WAKO THEN KOMAA KIVYAKO!

Dah! Kazi kweli kweli mkuu
 
Kuna wazo ningekupa ulifanye la kuingiza 20-15 tsh kwa siku
Kwa mtaji mdogo wa kuanzia.

Ila inahitaji muda wa kutosha.
Mazingira ya sehemu uliopo.
Aina ya watu waliopo katika mazingira hayo.
Uweke vyeti vyako pembeni ili ufanikiwe na toa aibu ya fulani atanionaje.


Think again kuna watu wanaishi vizuri bila ya mshahara.
 
Kuna wazo ningekupa ulifanye la kuingiza 20-15 tsh kwa siku
Kwa mtaji mdogo wa kuanzia.

Ila inahitaji muda wa kutosha.
Mazingira ya sehemu uliopo.
Aina ya watu waliopo katika mazingira hayo.
Uweke vyeti vyako pembeni ili ufanikiwe na toa aibu ya fulani atanionaje.


Think again kuna watu wanaishi vizuri bila ya mshahara.

Sawa Mkuu,nashukuru sana;baadaye ukipata nafasi unidokeze kidogo kuhusu hiyo issue!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom