Nani kama baba!?

Siri ya sifuri

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
2,613
Reaction score
2,258
Habari wakuu?leo naombeni kwa pamoja tujadili umuhimu au ukuu wa baba ndani ya familia, mara nyingi nimekua nisikia watu wakihoji nani kama mama!? mara zote jibu langu huwa ni baba, kwanini? kwasababu yeye ndio kimbilio la familia nzima kuanzia mama hadi watoto, kwa kawaida mama huwa mwepesi kupokea taarifa za yeyote kwenye famillia, iwe shida,maombi,pendekezo au jambo jingine lolote, mama hujaribu kwa uwezo wake kuweka mambo sawa, iwapo likitokea lililo nje ya uwezo wake hulipeleka kwa baba bila kufikiria kama atalimudu au la, kwa baba ndio mwisho wa mtatizo yote, hastahili kushindwa, mama yupo kwa niaba ya baba, iweje tena awe zaidi ya anaemwakilisha? karibuni wakuu,weledi, tujadili kwa hoja.
 
Baba ni mwalimu
Mama ni mwanafunzi

Mwalimu anafundisha na kuelewa masomo machache
Mwanafunzi anasoma na kuelewa masomo yote

Baada ya muda wanafunzi huwa na maisha mazuri kushinda walimu wao..

Waheshimu Baba na Mama yako
 
Mother's day utawaona wanapost miphoto na mama zao, siku ya fathers day huwasiki hata kutoa hongera. Mama akifariki familia utaiona bado ipo imara lakini baba akifariki utaiona familia inavyo anguka. Baba ni kisiki cha mpingo, ukikubali au ukikataa hio ni hali halisi.


Ndukiiiii πŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈ
 
Kwa wengine tuna stori tofauti kabisa
 
ukitaka kujua umuhim wa baba kweny famly.. uliza single mother

asikwambie mtu baba ndio kila kitu kwenye family baba akiwa vizr family yte itakuwa vizr

iyo furaha watoto wanayoipata kwa mama mpaka kusema mama ni bora kuliko baba inaanzia kwa baba yan baba anawapa watoto furaha kupitia mama tu
 
mama ako sio ndugu yako,baba ako ndo mchizi wako
 
Wamama wanajifariji tu lakini steringi wa yote ndio sie kinababa. Wanazunguuka weee kisha wanarudi.
 
Ni kweli, hakuna mwanamke mjanja mbele ya mwanaume. Ulishawah jiuliza hii dunia tungeishi wanawake tupu tungekuaje.

Wakina baba wana roho nzuri SNA tatizo lao moja tu kuchepuka kwenye ndoa zao.

Sisi wanawake hata tuwe na mil5 kwenye pochi na bado utamwomba mwanaume pesa ya matumiz na atakupa kiroho safi.

Ila muombe mwanamke hela hats 400 ya daladala kila MTU atajua.

Nawapenda SNA wakina baba, hasa mume wangu wanamchango mkubwa SNA kwenye familia tofauti na mama.
 
Ilikua siku baba akisafiri nyumba inakua kama imemwagiwa maji hata akipita paka nje nyumba nzima mnatetemeka!! Lkn mshua akiwepo hata tembo akipita mna hakika mdingi atamteketeza ndani ya sekunde tu. Baba ndio amani ya nyumba
 
Baba ni mwalimu
Mama ni mwanafunzi
Mwalimu anafundisha na kuelewa masomo machache
Mwanafunzi anasoma na kuelewa masomo yote
Baada ya muda wanafunzi huwa na maisha mazuri kushinda walimu wao..
Waheshimu Baba na Mama yako
Asante mkuu
 
Inafikirisha sana.
 
hapo ndipo tulipomezwa, mkuu.
 
ubarikiwe mkuu, na hilo la kuchepuka ongea na kaka atakuelewa tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…