munyakwiringa
Member
- Apr 14, 2015
- 65
- 8
Habari zenu wadau:
Mimi ni moja ya vijana wachache waliojisomesha wenyewe tangu darasa la pili mpaka darasa la saba na baadae kujiunga na masomo ya kidato cha cha kwanza mpaka cha nne kwa miaka miwili, nilipo maliza nilijiunga na mafunzo ya kupiga picha kwa maana ya Video & TV Production ambapo nilifanya vizuri katika masomo yangu na kuanza kujishughulisha na kazi za uandaaji wa shughuli mbalimbali zihusuzo taaluma yangu. Baadae nilionwa na shirika flani baada ya kupitia kazi zangu wakaamua kuniajiri na kwakweli kwao nilikua muwazi kuwa kingereza bado ni shida kwangu kutokana na mapito ya kudunduliza elimu yaliyonikuta katika maisha.
Wakanambia nisitishwe sana na mawasiliano ya kingereza kwani kikubwa ni outputs za kazi wanazonipa na si kuongea kingereza without output (najaribu kuongea kidhungu ukinikosoa ndo kuelewa kwenyewe) kunasiku tulitembelewa na wageni ofisini na watu wote wakajitambulisha kwa CV za hatari mie nikawaambia hicho kidogo nilichonacho na wale wageni walikua marafiki zangu zaidi pamoja na kuwa sinaujuzi wa kuongea kingereza kwa ufasaha lakini nilipata kibari kuriko mtu mwingine ofisini.wenzangu waliosoma wakasema sina lolote kwakua sijui kingereza cha kuongea kwa ufasaha.lakini mpaka sasa nipo kwenye taasisi hiyo kwa mwaka wa tatu naelekea wanne sasa.
Inawezekana unataaluma yako lakini humudu kuongea kingereza kama mimi nilivyokua naanza kazi kwenye taasisi hiyo. Jiamini maana taaluma ni bora zaidi kuliko kuongea ongea kingereza nakukifanya kama taaluma.
Wadau naomba kuwasilisha naamini yuko mtu atasaidika na hii
Mimi ni moja ya vijana wachache waliojisomesha wenyewe tangu darasa la pili mpaka darasa la saba na baadae kujiunga na masomo ya kidato cha cha kwanza mpaka cha nne kwa miaka miwili, nilipo maliza nilijiunga na mafunzo ya kupiga picha kwa maana ya Video & TV Production ambapo nilifanya vizuri katika masomo yangu na kuanza kujishughulisha na kazi za uandaaji wa shughuli mbalimbali zihusuzo taaluma yangu. Baadae nilionwa na shirika flani baada ya kupitia kazi zangu wakaamua kuniajiri na kwakweli kwao nilikua muwazi kuwa kingereza bado ni shida kwangu kutokana na mapito ya kudunduliza elimu yaliyonikuta katika maisha.
Wakanambia nisitishwe sana na mawasiliano ya kingereza kwani kikubwa ni outputs za kazi wanazonipa na si kuongea kingereza without output (najaribu kuongea kidhungu ukinikosoa ndo kuelewa kwenyewe) kunasiku tulitembelewa na wageni ofisini na watu wote wakajitambulisha kwa CV za hatari mie nikawaambia hicho kidogo nilichonacho na wale wageni walikua marafiki zangu zaidi pamoja na kuwa sinaujuzi wa kuongea kingereza kwa ufasaha lakini nilipata kibari kuriko mtu mwingine ofisini.wenzangu waliosoma wakasema sina lolote kwakua sijui kingereza cha kuongea kwa ufasaha.lakini mpaka sasa nipo kwenye taasisi hiyo kwa mwaka wa tatu naelekea wanne sasa.
Inawezekana unataaluma yako lakini humudu kuongea kingereza kama mimi nilivyokua naanza kazi kwenye taasisi hiyo. Jiamini maana taaluma ni bora zaidi kuliko kuongea ongea kingereza nakukifanya kama taaluma.
Wadau naomba kuwasilisha naamini yuko mtu atasaidika na hii